Leo wabunge wa mkoa wa DSM pamoja na mkurugenze mkuu wa NHC watafanya mkutano na wakazi wa Ubungo NHC. Wabunge hoa watataka kujua ujenzi unao endelea hapa ubungo kama umefata taratibu zote za ujenzi maana sasahivi ukipita katikati ya haya magorofa ni hatari tupu, vile vile wabunge watataka kufahamu kuusu uzwaji wa magorofa ya zamani maana mswada ulisha pitishwa bungeni tangu mwaka 2005 kama wakazi wa ubungo wauziwe izo nyumba. Wapangaji wa ubungo NHC wamejikusanya kwa wingi wakiwasubiri wiongozi hao wafike ili kikao kianze. Kama Msechu hakishindwa kujieleza vizuri, wabunge hao wamepanga kukwamisha bajeti nzima ya wizara ya mama Tibaijuka!