Wabunge wa CHADEMA watoka nje kususia hotuba ya Rais Kikwete

Kama wao kweli wanajua kususa wasuse Posho bungeni tuwaone kama kweli wamepania.

Wasusie nini posho wakati kazi tuliyowatuma kufanya wameifanya. Kwani hiyo posho anawalipa Kikwete na Riz 1? Si ni pesa yetu tunawalipa kufanya kazi ya kuwakilisha matakwa yetu na kufikisha msimamo wetu humo mjengoni. Na huo ndio msimamo wa wananchi wote ambao kura zao zimeibiwa na tume. Bado wananchi wataanza kumkimbia Jk hadi katika vilio, viwanja vya michezo na mikutano ya hadhara. Ni hatari kuji associate na mtu asiyekuwa mwaminifu!!!!!
 
sasa hao wabunge wa chadema kama hawamtambui rais napia hata serikali yake hawaitambui,je wanaingie bungen kufanya nini?wangesusia kabisa bunge mpk malengoyao yatimie,ila kwa style hii ni sawa nakujambia mtoni,hakuna walifanyalo,unaingia bungen unampiga swali wazir alieteuliwa narais ambae humtambui huoni kama unatwanga maji kwenye kinu?unamtambua wazir ila aliemteua wazir humtambui,ama kweli hawa chadema wana akili kama zayule juha wakale abunuwas,wowote iwavyo PoSHO TAMU KAKA, ila nawewe sikulaum,UKIPENDA CHONGO UTASEMA NI KENGEZA

Wewe ulitaka wasusie bunge ili wasituwakilishe kweli makengeza yako hayawezi kuponywa hadi pale mwizi fisadi atakapong'olewa. Tena waambie wakuongezee PoSHO khe khe khekheeeeeeeeeeee. Si ndio kazi uliyopewa tena kwa fweza zetu. Uzuri wake angalau unafahamu huu mrija unakuja katwa si muda mrefu.
 
chadema; matendo yenu mengi nayaafiki lakini hili sina hakika nalo. mnakotaka kuipeleka nchi yetu wala siko:nono:
 
Political Immaturity.
kishongo nadhani umekurupuka kujuddge kuwa ni political immaturity, hiyo ni kuiamsha jamii ya kimataifa itake kujua kulikoni? lakini CUF ya leo ilipitia haya haya. hongera wewe ambaye ni politically matured!
 
Wewe unaishi sayari gani yaani Kikwete awasaidie wabunge wa Chadema kurudi bungeni mbona hakuwasaidia mwaka huu nafikiri unaota.

Bora nibaki nikiota wewe ubaki na uchadema badala ya utanzania kwa sababu ukweli nimeueleza wazi na utasimama daima. Kama kweli wako serious wasirudi tena bungeni na wala wasichukue posho na wasiende kuchukua hela za kununua magari maarufu 'mashangingi', na wasishirikiane kwa vyovyote na serikali ya JK. otherwise, ni kula matapishi yao wenyewe.
 
Nitachoona mimi walichofanya ni sahihi mno kuliko wangebaki na kumsikiliza. Elewa unaposema humtambui kiongozi hauna sababu ya kumsikiliza. Kama wangebaki na kumsikiliza tungewauliza walikuwa wanamsikiliza nani ikiwa wao walishasema hawamtambui rais?
 
Mmh! lakini jambo lililofanyika pale bungeni ni utovu wa nidhamu kwa mamlaka iliyoko madarakani.

wewe umeenda shule ila hujasoma, nasema hivi kwa sababu unashindwa kuielewa hoja ya Dr. Slaa. Chadema hawadai kusinda uchaguzi wa
rais ila wanazikataa chakachua zilizoipa 61% ccm, YES Mh Kikwete ni mshindi ila kwa less than 61. hamna personal problems kati ya Dr. Slaa
na Rais Kikwete.
 
Political Immaturity.
Mwenye political immaturity ni yule anayejisifia watanzania watakuja kwake kumlilia,jana alisema watanzania watamlilia huku akiwa na furaha,hivi rais wa nchi anaona fahari anapoliliwa?watanzania hali inapozidi kuwa mbaya JK anajawa furaha manake ataliliwa zaidi?JK aliingiza suala la udini kwenye kampeni leo anaomba asaidiwe kulifuta,hivi kama si JK+MKAPA kuhubiri udini watanzania wasingeutizama uchaguzi from religious angle.From now dini itakuwa central issues kwenye chaguzi JK ametupeleka wapi jamani?CCM +JK walishangilia kuondoka chadema bcs walijua wamepata mwanya wa kuiuza nchi KUMBE NO!Mnyukano kama kawa
 
Naamini hii ni transcription rasmi ya taarifa ya Dr Wilbroad Slaa……


Ndugu zangu Watanzania, pamoja na ndugu zangu wote waliokuwa wanafuatilia matukio ya bungeni leo. Aaah... ni kweli nimepata watu wengi wakiulizia, aah.. ni kwanini wabunge wa CHADEMA walitoka ndani ya ukumbi wa bunge, wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano alipoanza kutoa hotuba yake.

Hivi wabunge wa Chadema si wana uongozi wao na msemaji wa makubaliano ya caucas yao ni ama Mwenyekiti wa chama ama Mnadhimu wa wabunge (Party Whip). Hatua ya Dr Slaa kuliongelea hili sio uthibitisho kuwa hatua hii ni shinikizo lenye kujali maslahi yake (EGO) na sio maoni ya wabunge wa CHADEMA? Katibu wa chama anawezaje kuwa msemaji wa msimamo uliotolewa na kikao cha wabunge ambacho yeye sio msemaji wake?

Eeenh... moja ni kwamba CHADEMA ni chama chenye msingi, kinachofuatilia, eenh na kuhakikisha kwamba daima kiko consinstent yaani kinatekeleza kile ambacho kinasimamia, aah kwa kuwa tulikwisha kukataa kutambua matokeo ya uchaguzi, na vilevile baada ya kukataa kutambua matokeo tulikataa vilevile kumtambua rais aliyepatikana kwa mchaka.. eenh kutokana na mchakato huo ambao hatuutambui, basi ni dhahiri kabisa aah matendo yetu yaendane na kile tunachoamini.

Nini msingi wa CHADEMA…ni miaka mitano sasa najaribu kupata jibu ya swali hili nashindwa?

Wabunge wetu wapo kwenye forum ambayo inasimamia kile ambacho CHADEMA inakiamini. Bunge ni mahali ambapo wabunge wana nafasi ya kubeba bendera ya CHADEMA, na mahali pa kwanza pa kuonyesha kwamba hatumtambui rais ni dhahiri basi ni kwamba ni ndani ya bunge.

I hope kuna kitu mnakiaamini ziadi ya kuwa ninyi ndio wateule wa kutawala nchi ya Tanzania na sio wengineo kama ambavyo baadhi ya wagombea wenu walivyokuwa wakijinadi kwa kuchakachua tafsiri za maandiko matakatifu……..

Kitendo cha leo kilianzia asubuhi, kwa wabunge wetu kutohudhuria hafla ya kumuapisha Waziri Mkuu, kwa sababu isingekuwa na maana kwenda kuhudhuria hafla ambayo inasimamiwa na rais ambaye kimsingi hatumtambui, lakini vilevile ni ishara kwa watanzania kwamba bado eenh tunataka maelezo ya kina kutoka serikali kuhusu kauli tulizokwishakuzitoa.

Kama hamumtambui Rais iweje mpige kura ya hapana kwa uteuzi wake na sio kutoshiriki katika hatua hiyo kwani Waziri Mkuu huyo ni mteule wa Rais msiyemtambua?

Hizi ni ishara muhimu katika siasa, kupelekea kuipeleka kwa serikali kwamba kuna malalamiko ya msingi ambayo tunayo kuhusu mchakato wa uchaguzi, na ni dhahiri kwamba kama serikali ni makini, kama serikali ni sikivu basi itasikiliza kauli hiyo ya wenzetu ambao huko bungeni. Lakini kauli hizo hazitaishia pale, kama tulivyokwishakutoa katika press conference yetu, tulisema tutatumia forum ndani ya bunge, na forum nje ya bunge kupiga kelele mpaka serikali itusikilize.

Kwangu hii ni ishara ya kuwa mnadhani kuwa siasa za DRAMA na EMMOTIONS ndizo zilikuwa mtaji wa mafanikio yenu katika uchaguzi huu na sio siasa za engagement kama ambavyo mlikuwa mkizifanya katika miaka kumi iliyopita na hivyo kuwajengea imani njema miongoni mwa baadhi ya watanzania wengi wao wakiwa bado wanajitambulisha kama CCM haohao ambao mnaonysha sura ya kuwa wao ni maadui zenu……I hope u have what it takes to be 100% protest party in a conservative socity like ours ambayo in miaka 50 ya kuwa shaped na fikira na mitazamo ya CCM…..

Lakini pia sidhani, siamini na wala sitegemei kuona serikali MAKINi inakubali kuwa blackmailed kama ambavyo mnafanya….Hiyo itakuwa ni serikali joga na sio serikali makini. Kwangu mimi ingawa serikali hii na kwa miaka iliyopita ilikuwa na mapungufu mengi sana lakini naamini na natambua kuwa ilijitahidi kwa kiasi kikubwa kuwa sikivu hata kama sio kwa kila kitu mlichotaka ama watanzania walikitaka.

Lakini hivi tangia lini matendo ya wabunge 47 ya kumvunjia heshima kiongozi wa wabunge 250+ yakaweza kushinikiza siasa za usikivu ama umakini na sio vice versa? Kama miaka 15 ya siasa kama hizo kati ya CUF na CCM ambao ni wazi historia na mgawanyiko wa kijamii wa zaidi ya miaka 50 uliwafanya kuwa na nguvu sawa kiushawishi zilishindwa hadi upande moja ulipolazimika kuwa na uthubutu wa kumheshimu mwenzie ndipo tunaona yanayotokea Zanzibar. Hivi ninyi ambao ukweli ni kuwa ushawishi wenu umegawanyika katika asilimia 10 ya wafuasi na 15 ya washabiki, na wenzenu ni dhahiri wana ushawashi wa zaidi ya asilimia 60, mnategema kweli kuna uwezekano wa kufanikiwa kulazimisha UMAKINI mnaoujengea mazingira kwa style hii? Ama wenzetu mnategemea mgawanyiko wa kijamii ambao umekukuzwa sana na harakati za uchaguzi utastawi na kuwawezesha kuongeza political base ya kuilazimisha CCM kusalimu amri hivi karibuni?

Ni nini tunachokihitaji ? Tunahitaji, aah, demokrasia ya kweli katika nchi yetu, tunahitaji uchaguzi ambao utaendeshwa kwa misingi ya misingi ya demokrasia ya kweli.

Nadhani the best way ni kuanza na demokrasia ya kweli katika CHADEMA. Angalao kufanya uchaguzi mmoja bila ya uchakachuaji wa aina moja ama nyinge kama uzoefu unavyoonyesha. Nasema hivi kwa kuwa hata kama serikali iliyopo madarakani italeta mabadiliko ya aina gain, kama CHADEMA na vyama vingine hamjaweza kuheshimu na kujenga utamaduni wa demokrasia ya kweli katika platform zenu basi daima hamtaweza kuenga imani ya kuwepo kwa demokrasia ya kweli hadi pale demokrasia hiyo itakaporidhisha maslahi yenu binafsi na kukandamiza maslahi ya wengine ambao mnadhani kuwa demokrasia ya sasa inawapendelea.


Tunahitaji tume huru ya uchaguzi. Eenh.. tunahitaji sheria mbovu ziweze kurekebishwa, ili chaguzi zisiendelee kuchakachuliwa kama ilivyotokea safari hii. Kwa hiyo haya ni mambo ya msingi ambayo hakuna mtu yeyote atatuambia tusiyadai, kwa sababu tumelalamika mara nyingi juu ya kat.. ya marekebisho ya katiba, serikali imekuwa si sikivu haitaki kusikiliza, tumedai kuhusu tume huru, serikali imekataa kutusikiliza,

Hapa nakubaliana nanyi asilimi mia moja, Katiba mpya ni muhimu sio kuwa ndio utakuwa ukombozi wa mtanzania lakini zitaondoa ama kupunguza athari za siasa za hisia ambazo zinawezeshwa na utata wa uhalali wa utungaji na ubadilishaji wa katiba yetu…….Tume huru pia ni muhimu laki uhuru huo usiwe hadi pale tu "mtakaporidhika" kwa misingi ya maslahi yenu bali uhuru ambao utawaruidhisha watanzania kwa msingi wa maslahi ya watanzania wote wakiwemo wale walio CCM na wale tusio waamini ninyi nyote….

tumedai marekebisho ya sheria mbalimbali ambazo ni kandamizi serikali haitusikilizi,

Hivi katika sheria arobaini ambazo Jaji Nyalali alizitambua kama sheria kandamizi ni ngapi zimeondolewa, kubadilishwa ama zimebaki? Hivi mnaposema sheria kandamizi ni zipi hizo? Zitajeni tuzijue na kuzielewa sio kutuburuza tu kuwa kuna sheria kandamizi……

Itaendelea..........
 
JK itamchukua muda sana kuelewa kitendo cha Chadema kutoka nje ya ukumbi ndiyo maana badala ya kusikitika alianza kuponda mwishowe.Lakini he got touched ndiyo maana hata speech yake hakuimalizia maana nadhani aliwazia kila kitu in the eyes of wote alio waalika wakiwemo mabalozi nk .Hapo picha ime haribika and something need to be done haraka .
 
Jamani kama kila anayetumia haki yake ataitwa mjinga, BASI NITAWAITA WAJINGA WATU WOTE WALIOWEKA ALAMA YA VEMA KWA CCM. Hao wote hawakufanya vizuri lakini nashindwa kuwapa jina la ujinga kwani ilikuwa ni haki yao.
Sasa basi kila anayeshutumu haki ya wana Chadema kutoka nje ya bunge kwa kuwaita wajinga huyo kwangu ni MJINGA NAMBA MOJA Maana hakika ni mwana CCM.
 
Wabunge wa CHADEMA kwa pamoja wametoka nje kususia hotuba ya Rais sasa hivi.

mbowe_chadema.jpg

wabunge-chadema.jpg


Tutarajie na haya yakijirudia -haaaaaaaaaaaaa CCM mbele kwa Mbele-na ina wenyewe!

Lowassa anaweza kusema jambo kuhusiana na historia hii iliyopita !

 
JK itamchukua muda sana kuelewa kitendo cha Chadema kutoka nje ya ukumbi ndiyo maana badala ya kusikitika alianza kuponda mwishowe.Lakini he got touched ndiyo maana hata speech yake hakuimalizia maana nadhani aliwazia kila kitu in the eyes of wote alio waalika wakiwemo mabalozi nk .Hapo picha ime haribika and something need to be done haraka .


Miaka mitano hiyooooooooooooooo! Uwezekano wa yale yale kujirudia ni zaidi ya 80% mpaka dakika hii.
 
Na sa iv wakitoka ni burn ya miezi 4, maana hyo itakuwa disobedience, ya hali ya juu.. na wakijichanganya tu wataisoma no.. hata democrasia inamipaka, acheni ujuha ukawa uchaguzi umeisha, msiendelee na ligi za mchangani...
 
Back
Top Bottom