Wabunge wa CHADEMA vipi?

mtz flani

Member
Aug 31, 2011
36
7
hawa jamaa ni wanamapinduzi na hakuna anayebisha kuhusu hilo, lakini kuna issue wamefanya na haijanipedeza. nawauliza kwa nini walituhadaa kukataa posho za vikao then wakarudi kwa mlango wa nyuma wakachukua? je ilikuwa ni propaganda ya kujitafutia umaarufu wa kisiasa?
 
................Mimi ni mwanachama wa CDM damu,naunga mkono hoja mkuu,ni bora watoe tamko juu ya hili,ama sivyo ni doa kwa chama...
 
Tumeshaelezwa kwa maelezo marefu na ya kueleweka na Mhe Zito Zuberi Kabwe, tatizo hatusomi au hatuelewi.
Amefafanua kuwa fomu ya kusaini kwa ajili ya mahudhurio na posho ni moja. Hivyo kuonesha umehudhuria kikao lazima usaini. Ukisaini moja kwa moja unapata posho. Alifafanua kuwa walishapeleka ombi kuwa fomu hizo zitenganishwe, labda sasa bado hawajalifanyia kazi. Usiposaini inaonesha hukuhudhuria, na usipohudhuria sijui mikutano mitatu unafukuzwa.
Kwa upande wake Zito ameeleza kuwa yeye hawatamfukuza kwani kuna njia nyingi ambazo ataonesha kuwa alihudhuria hata bila kusaini. Mojawapo ni uchangiaji. Kwa vyovyote huo ulikuwa uamuzi mgumu aliouchukua, TUNAMPONGEZA KWA DHATI.
Ni uamuzi ambao wengine wanapaswa kufuata. Ila la Muhimu labda wapiganie hizo fomu zitenganishwe ili kuwafahamu nani ni Shibuda type na nani sio.
 
hawa jamaa ni wanamapinduzi na hakuna anayebisha kuhusu hilo, lakini kuna issue wamefanya na haijanipedeza. nawauliza kwa nini walituhadaa kukataa posho za vikao then wakarudi kwa mlango wa nyuma wakachukua? je ilikuwa ni propaganda ya kujitafutia umaarufu wa kisiasa?

Nimeamini wewe ni MTZ Fulani maana kweli umekuja hapa na hoja ya kichovu mno.Posho hizi Mbowe kesha sema sana sana na kufafanua kwa undani .Posho hizo kuziacha kwa kususoa si jibu Chadema wanataka neno posho lifutwe kote na si kwao pekee so uelewe kwamba upupu wako hauna nafasi .Kaa tulia jenga hoja na upupu acha maji marefu hapa jamvini mkuu .
 
Tumeshaelezwa kwa maelezo marefu na ya kueleweka na Mhe Zito Zuberi Kabwe, tatizo hatusomi au hatuelewi.
Amefafanua kuwa fomu ya kusaini kwa ajili ya mahudhurio na posho ni moja. Hivyo kuonesha umehudhuria kikao lazima usaini. Ukisaini moja kwa moja unapata posho. Alifafanua kuwa walishapeleka ombi kuwa fomu hizo zitenganishwe, labda sasa bado hawajalifanyia kazi. Usiposaini inaonesha hukuhudhuria, na usipohudhuria sijui mikutano mitatu unafukuzwa.
Kwa upande wake Zito ameeleza kuwa yeye hawatamfukuza kwani kuna njia nyingi ambazo ataonesha kuwa alihudhuria hata bila kusaini. Mojawapo ni uchangiaji. Kwa vyovyote huo ulikuwa uamuzi mgumu aliouchukua, TUNAMPONGEZA KWA DHATI.
Ni uamuzi ambao wengine wanapaswa kufuata. Ila la Muhimu labda wapiganie hizo fomu zitenganishwe ili kuwafahamu nani ni Shibuda type na nani sio.

Mkuu kwa nini wengine nao wasifanye kama Zitto? Wangefanya hivyo posho za vikao zingeondolewa lakini wao wanazipenda na kuzitaka. Katika hili Wabunge wa CHADEMA akiwemo mbunge wangu niliyempigia kura, Ndg. John Mnyika, wameonyesha unafiki mkubwa wa NATAKA SITAKI. Wajivue Gamba la posho mbona mwenzao Zitto amejivua kwa kutosaini?
 
hawa jamaa ni wanamapinduzi na hakuna anayebisha kuhusu hilo, lakini kuna issue wamefanya na haijanipedeza. nawauliza kwa nini walituhadaa kukataa posho za vikao then wakarudi kwa mlango wa nyuma wakachukua? je ilikuwa ni propaganda ya kujitafutia umaarufu wa kisiasa?
Mkuu, mbona unataka kupotosha umma! CDM hamna Wanamapinduzi ni kikundi cha wasanii watupu pamoja na porojo
 
Ni heri wazichukue Hizo Posho kwa sababu wakiziacha zinaliwa na wanamagamba,Hoja ni KUFUTWA KWA POSHO NA SIO KUZIACHA.
Hakuna sababu ya wao awawaachie hao wezi jamani eleweni kuwa hoja ni kutaka kufutwa
 
RITZ ! uwe mwelewa wewe je unajua maana ya Usanii kweli wee..................
 
Wanachopigania ni posho zifutwe. Na si kuzigomea. Hata ktk mapinduz huwa hawaanz wote at once, ameshaanza Zito hope makamanda wote watafata. Labda mwanzoni hawakuwaza hiyo alternative ya kutokusaini form za mahudhurio.
 
Nilisikitika sana baada ya kusoma hiyo habari jana. Nashauri wabunge wa CHADEMA waliochukua posho watupatie ufafanuzi. Na kama kuna uwezekano wazirejeshe.

Bunge: Wabunge wa Chadema wamepokea posho


Wednesday, 31 August 2011 12:04


zitto%20bungeni%20bajeti.jpg
Zitto kabwe​

Ramadhan Semtawa na Fidelis Butahe
LICHA ya msimamo wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wa kuchukua au kutochukua posho za vikao, taarifa za Ofisi ya Bunge zinaonyesha kuwa wabunge wa chama hicho isipokuwa Zitto Kabwe, wamekuwa wakisaini fedha hizo hadi kuahirishwa kwa Mkutano wa Nne wa Bunge wiki iliyopita.

Juni 7, mwaka huu Zitto aliwasilisha barua Ofisi ya Bunge kukataa posho ya Sh70,000 (Sitting allowance), kwa siku akisema watumishi wa Serikali na wabunge, hawastahili kulipwa posho wanapohudhuria vikao rasmi vya uwajibikaji wao wa kawaida ndani ya Bunge.

Msimamo huo uliungwa mkono na Kambi Rasmi ya ya Upinzani Bungeni baada ya kiongozi wake, Freeman Mbowe kusema hilo limo kwenye Ilani ya Chadema ya mwaka 2010. Pia Mbowe alikataa kutumia gari la Serikali maarufu kama shangingi.
Hata hivyo, msimamo huo ulipingwa na baadhi ya wabunge huku Mbunge kutoka chama hicho, John Shibuda akienda mbali kwa kutaka badala yake, ziongezwe ikiwezekana hadi kufikia Sh500,000.

Kaimu Katibu wa Bunge John Joel, alisema jana kuwa ni Zitto pekee ambaye ameacha kusaini fedha hizo tangu alipotoa msimamo wake.

Akizungumzia kwa simu, Joel alisema wabunge wote wa Chadema wanachukua posho lakini, Zitto amegoma kusaini.
Joel alisema katika kumbukumbu, kila Mbunge wa Chadema aliyesaini wakati akiingia kikaoni ndani ya Bunge alilipwa posho na kuongeza kwamba hakuna aliyezikataa au kuzirudisha.
“Wabunge wote wa Chadema waliosaini wamekuwa wakipewa posho, ni Zitto pekee ambaye amekuwa akigoma kusaini posho hizo,” alisisitiza Joel.

Alipoulizwa kama pia Zitto alikuwa akiingiziwa, alijibu: “Zitto hakuwa akisaini na aliacha tangu alivyotangaza msimamo wake mwezi Juni”.

Alisema kwa utaratibu, kila mbunge anayesaini wakati akiingia bungeni kuhudhuria kikao hupewa posho yake ya kikao.
Hata hivyo, Spika wa Bunge, Anne Makinda aliwahi kumuonya Zitto kwamba, kama asingesaini mahudhurio ambayo ndiyo yanayotumika kuandaa posho hizo, angeweza kuchukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kusimamishwa ubunge.

Lakini, duru za kisiasa zinaonyesha ingekuwa ni vigumu kwa Spika kumfukuza Zitto baada ya kugoma kusaini kwani amekuwa akionekana bungeni huku akiibua hoja nzito ikiwamo ya kulishawishi Bunge kuunda Kamati Teule kuchunguza suala la Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo kurejeshwa kazini na mamlaka ya nidhamu ambayo ni Katibu Mkuu Kiongozi.

Pia Zitto aliwasilisha kusudio la kuomba Bunge liunde kamati teule ya kuchunguza tuhuma za ufisadi wa Kampuni ya Meremeta.

Msimamo wa Zitto
Juni 7, mwaka huu Zitto aliandika barua akisema posho hiyo haistahili kulipwa kwake, wabunge wengine wala watumishi wa umma kwa kuwa kuhudhuria vikao ni sehemu ya kazi zao.

Badaye, mara baada ya Chadema kutangaza msimamo huo, Spika Makinda alipinga uamuzi wa kususia posho akisema suala hilo lipo kisheria na kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kuamua kuliondoa.

Hata hivyo, akihitimisha hoja za wabunge katika hotuba yake ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya ofisi yake na zilizo chini yake, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alisema suala la posho lipo kwenye mchakato wa kuangaliwa upya na kwamba zile za vikao huenda zingefutwa.

Waziri Mkuu ambaye awali alionekana kupingana na Chadema, alisema Katiba inakataza suala la posho zisizo za msingi na kwamba utaratibu huo umeandaliwa kwa kufuata utaratibu mzuri bila ya kuathiri mazingira na mfumo uliopo ndani ya Serikali kwa watumishi wake.

Hata hivyo, Shiduda ambaye ni Mbunge wa Maswa Magharibi amepinga msimamo huo wa chama chake na kujikuta akiwa katikati ya mgogoro na baadhi ya viongozi wake kiasi hata cha kutishia nafasi yake ya uanachama.
 
unamaanisha nin?
Wabunge wa CDM ni wasanii wametudanganya Watanzania kuwa watagomea posho zote bunge cha kushangaza juzi ofisi ya katibu wa bunge imetoa taarifa kwenye vyombo vya habari kuwa hakuna hata mbunge mmoja aliekataa kuchukuwa posho wote wamechukuwa mpaka Mbowe, Msemaji mkuu wa kambi ya upinzani bungeni.
Hii ndio maana yangu kijana nadhani utakuwa umenielewa, kama wewe ni mateka wa CDM najua uwezi kunielewa
 
Tatizo la watu wengi, wanasikiliza kidogo na hata hicho kidogo wanachosikia wanachoelewa ni kidogo zaidi. Haya mambo yameongelewa hapa tena na tena lakini bado watu hawataki kuelewa.
 
Wabunge wa CDM ni wasanii wametudanganya Watanzania kuwa watagomea posho zote bunge cha kushangaza juzi ofisi ya katibu wa bunge imetoa taarifa kwenye vyombo vya habari kuwa hakuna hata mbunge mmoja aliekataa kuchuwa posho wote wachukuwa mpaka Mbowe.<br />
Hii ndio maana yangu kijana nadhani utakuwa umenielewa, kama wewe ni mateka wa CDM najua uwezi kunielewa
<br />
<br />
na kama na wewe ni mateka wa magamba, basi huwezi tegemea ukaongea mambo mazuri kuhusiana na makamanda!
 
Mkuu kwa nini wengine nao wasifanye kama Zitto? Wangefanya hivyo posho za vikao zingeondolewa lakini wao wanazipenda na kuzitaka. Katika hili Wabunge wa CHADEMA akiwemo mbunge wangu niliyempigia kura, Ndg. John Mnyika, wameonyesha unafiki mkubwa wa NATAKA SITAKI. Wajivue Gamba la posho mbona mwenzao Zitto amejivua kwa kutosaini?
kaka kuwa mwepesi kuelewa zitto kasema yeye hawezi fukuzwa kwa point ya kuwa anachangia sn hoja so ht asiposign bado anapakujitetea na hasard inarecord kama unavyojua zitto mara nyingi anchangia sn sasa wengine uchangiaji wao sio sawa na wa zitto so ni bora wasign kuliko kufukuzwa bugeni.... si chadema wote wanachangia sawa mkubwa ila kwa zitto inaeleweka ni mchagiaji kwa sn so haiwezekani waseme hakuudhuria bungeni kisa hukusign wakati hasard inaonyesha kuna sauti ya zitto... point kubwa hapo form zitenganishwe.
 
ofisi ya katibu wa bunge imetoa taarifa kwenye vyombo vya habari kuwa hakuna hata mbunge mmoja aliekataa kuchukuwa posho wote wamechukuwa.<br />
<br />
<br />
hata kama ni ushabiki, punguza kidogo uongo, habari iko hapo juu na haijasema hayo unayoyasema!
 
hata kama ni ushabiki, punguza kidogo uongo, habari iko hapo juu na haijasema hayo unayoyasema!
Wewe ni CDM-Kata unafuata mkumbo tu, ujui chochote nitajie basi wabunge wawili tu wa CDM ambao hawajachukuwa posho bungeni
 
Wabunge wa CDM ni wasanii wametudanganya Watanzania kuwa watagomea posho zote bunge cha kushangaza juzi ofisi ya katibu wa bunge imetoa taarifa kwenye vyombo vya habari kuwa hakuna hata mbunge mmoja aliekataa kuchukuwa posho wote wamechukuwa mpaka Mbowe, Msemaji mkuu wa kambi ya upinzani bungeni.<br />
Hii ndio maana yangu kijana nadhani utakuwa umenielewa, kama wewe ni mateka wa CDM najua uwezi kunielewa
<br />
<br />
umeisoma barua ya Zito, ametoa ufafanuz vizur sana. Kwanin unakuwa mgumu.
 
kama kweli walimaanisha kile walichosema basi wangezikataa hizo posho halafu tumuone huyo mpuuzi wa kuwafukuza!nawaambia nchi ingewaka moto na mapinduzi yakweli yangeanzia hapo. but what happened?i don't support watu waoga ambao hawawezi even to stand kwenye maamuzi yao.kama zitto aliweza kwa nini wao washindwe?kama point ni kuwa zitto anachangia sana mijadala bungeni wengine wanabaki wasikilizaji sasa wana tofauti gani na zana nzima ya sitting allowance? maana kama kukaa tu na kulipwa posho basi hao ndio mwake!jamani vijana wezangu tuwe na uthubutu wa kuhoji pale tunapoona mapungufu sio kuwa na mapenzi ya upofu.kama tutashindwa kuwahoji sasa hivi wakiwa hawapo madarakani tutaweza kweli wakikamata dola?kumbukeni,tunataka kuwaondoa magamba madarakani kwa sababu wameshindwa kusimamia misingi ya utawala bora na mambo yenye maslahi kwa taifa.tuna Rais anayetoa amri zisizotekelezeka na pia kupuuzwa na watendaji wake,hatutaki kuona kitu kama hicho kikitokea kwa watu ambao tunaamini ni mbadala wa hawa magamba!
 
Back
Top Bottom