johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,763
- 141,628
Wakati wa awamu ya 5 kila mbunge akisimama ilikuwa ni lazima amsifie Hayati Magufuli kwamba, hakopi fedha na miradi mikubwa yote unatumia fedha za ndani.
Leo kila mbunge aliyesimama amempongeza Rais Samia kwa kwenda nchi za nje na kufanikiwa kututafutia riziki. Nasema ni wabunge wa CCM kwa sababu katika Bunge hili CHADEMA ina mbunge mmoja tu.
Nilichojifunza, ukiwa kiongozi usiwaamini sana wabunge wa CCM, wako kimaslahi zaidi. Wanaweza kukuingiza chaka kwa sifa zao za usoni siyo moyoni.
Mlale unono!
Leo kila mbunge aliyesimama amempongeza Rais Samia kwa kwenda nchi za nje na kufanikiwa kututafutia riziki. Nasema ni wabunge wa CCM kwa sababu katika Bunge hili CHADEMA ina mbunge mmoja tu.
Nilichojifunza, ukiwa kiongozi usiwaamini sana wabunge wa CCM, wako kimaslahi zaidi. Wanaweza kukuingiza chaka kwa sifa zao za usoni siyo moyoni.
Mlale unono!