Wabunge wa CCM wakataa Kuunga Mkono hoja ya Kujadili Mgomo wa Madaktari

Mhhh ina maana bungeni leo wapo CCM tuu au wapiganaji wetu wa Chadema , CUF n.k hawakupaswa kuunga mkono HOJA??? :shock::shock::shock:
 
Ndugulile, Mnyika wataka bunge lijadili kwa dharura mgomo wa madaktari bungeni; Ndugai akiuka kanuni kuilinda serikali.Mbunge wa Kigamboni Ndugulile na Mbunge wa Ubungo Mnyika wametaka miongozo ya spika kuwezesha hoja ya mgomo wa madaktari kujadiliwa kwa dharura bungeni.

Ndugulile aliomba muongozo wa Spika kwa mujibu wa kanuni 47 ili mjadala uhahirishwe kuwezesha kujadili kwa dharura kuhusu mgomo wa madaktari.


Mnyika kwa upande wake alitaka muongozo kwa kuwa kwa siku mbili mfululizo kambi ya upinzani imetaka suala la mgomo kujadiliwa bungeni ikiwemo kwa hoja ya dharura ya Naibu Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Zitto Kabwe ambayo iliungwa mkono siku chache zilizopita.

Mnyika alisema kwamba hoja hiyo ilipoungwa mkono Spika Makinda alisema kwamba serikali itatoa kauli kwa mujibu wa kanuni ya 49. Mnyika alisema kwamba kauli ya serikali haitakidhi haja kwa kuwa kauli hiyo inahusu jambo linaloihusu serikali wakati ambapo suala la mgomo linawahusu wananchi hivyo wabunge kama wawakilishi wa wananchi ndio wanaostahili kuwasilisha hoja.

Mnyika alisema pia kuwa kwa mujibu wa kanuni ya 49 iliyotumiwa na Spika, kauli ya serikali itawasilishwa wakati ambao Spika ataona unafaa wakati ambapo mgomo ni jambo la dharura na wananchi wanaendelea kufa na bunge halipaswi kusubiri. Mnyika aliendelea kusema kwamba kwa mujibu wa kanuni ya 49 kauli ya serikali halipaswi kuzua mjadala hivyo ikiwasilishwa haitajadiliwa wakati ambapo suala la mgomo wa madaktari linapaswa kujadiliwa ili hatua za dharura ziweze kuchukuliwa na bunge.

Kutokana na maelezo hayo Mnyika akaomba muongozo wa Spika ili wabunge waweze kuwasilisha hoja ya dharura.
Akitoa muongozo kuhusu maelezo ya Ndugulile na Mnyika Naibu Spika Job Ndugai alidai kuwa masuala waliyoeleza ni ya msingi lakini hayawezi kujadiliwa kwa kuwa wabunge wote wawili hoja zao hazikuungwa mkono.

Ndugai alifanya hivyo makusudi akijua kwamba wabunge wote wawili waliomba muongozo ili wapewa fursa ya kutoa hoja kwa mujibu wa kanuni.

Njia hii ya kuomba muongozo ili kupewa fursa ya kutoa hoja iliwahi kutumiwa pia bungeni na Mbunge wa Bumbuli Januari Makamba kuhusu suala la mgomo wa wauza mafuta ambao Ndugai bila kuungwa mkono lakini Ndugai alitoa muongozo wa kumpa nafasi Makamba kuwasilisha hoja na hatimaye hoja ikaungwa mkono.

Uamuzi huo wa Ndugai ulizua minong'ono miongoni mwa wabunge kuhusu Ndugai kukiuka kanuni kwa ajili ya kuilinda serikali dhidi ya mgomo wa madaktari kujadiliwa bungeni.
PM
 
Watanzania wenzangu hivi wooote tunaukumbuka huu wimbo????

Tanzania, Tanzania, NAKUPENDA KWA MOYO WOTE (!!!!?????????)
nchi yangu Tanzania, jina lako ni tamu sana (!!!!!!?????)
NILALAPO NAKUOTA WEWE, NIAMKAPO NI HERI MAMA WE (!!!!!!!!??????)

Mkuu huu wimbo ulikoma maana yake baada ya uongozi wa Nyerere !
 
Kweli uzalendo ni kitu adimu sasa katika hii mihimili miwili ya dola- serikali na bunge!. Baada ya kujihakikishia posho nono za kukaa 'bure' bungeni a.k.a kwa kuchumia matumbo yao na si kuwapigania wapigakura wao, hawana zaidi cha kufanya!! wagonjwa kufa mahospitalini si issue kwao, after all wana uhakika wa kupelekwa India hata wanapopatwa na ukurutu! ndio wabunge tuliowachagua wenyewe kwa hiari yetu wenyewe ama kwa kuvutiwa na kanga na t-shirt ama pilau walizotufadhili wakati wa kampeni. Wa kujilaumu ni sisi wenyewe na wala si wao!.

tuko pamoja mwanaJF......
kama tuliweza kuwaweka hapo, vivyo hivyo tunaweza kuwaondoa hapo.........wakuamua ni sisi, hakuna wa kutuamulia juu ya hili!!!
 
Ukisikia nchi yenye laana usisahau tz tunahitaji ukombozi,kiroho,kimwili na kiakili na kadhalika,kila m2 kwa dini yake tufunge na kuomba,
 
Kuna kizungumkuti ndani ya serikali juu ya Mgomo wa madaktari na Ongezeko la posho za kusinzia Bungeni, haiingii akilini kwa bunge kulipuuza suala la mgomo na kuendelea kulaghai watanzania kuwa posho hazijaidhinishwa wakati watanzania wanakufa!

Hivi hali ya hospitali nyingine huko mikoani ipoje, kama serikali na vyombo vya habari wanapiga propaganda kwa kutuonyeshea JWTZ wakiwasili Muhimbili wakati mikoani hali ni tete!
 
  • Baada ya kipindi cha maswali na majibu kwisha,Speaker aka step down na naibu spika akachukua nafasi.
  • Kutokana na kanuni ya 47 ya bunge,ulikua wakati wasaa wa kuwasilisha mwongozo.
  • Wakajitokeza wabunge wawili kuomba mwongozo; 1.Ndungulile na 2.Mnyika-wote waliomba kujadili ishu ya madaktari kwani ni urgent.
  • Ndugai akakubaliana nao kwamba wametumia kanuni vizuri lakiniiiii hoja zao hazikuungwa mkono.
My take
Baada ya wabunge hao wawili kutoa hoja wabunge hawakuulizwa kama wanaunga mkono hoja.Ndugai ameizima hoja kiubabe.

Sio ubabe, walitakiwa kusimama wabunge wengi ndo ionekane hoja imeungwa mkono.Kuulizwa kama wanaafiki au la ni baada ya hoja kuungwa mkono na wabunge kuchangia hoja hiyo
 
Investment waliyoifanya Ccm katika miaka 50 ya uhuru imefanikiwa sana, kujenga umma uliobemendwa wenye kucheka kwenye hatari na usioweza kujitambua na kujieleza!
Ingekuwa kinyume, huu ulikuwa mda muafaka wa kutanua mipaka ya janga hili na kugusa Kada nzima tungeona kama bado wangeendelea kupiga danadana.
 
kichwa cha habari/mada imekaa kinafiki na kichuki chuki mno.hakuna mbunge aliesimama kuunga mkono hata wa upinzani kwa hiyo ni bunge ndio halijaunga mkono sio wabunge wa ccm.acha umbea,umekua sasa
 
....Mheshimiwa Ndugulile na Mnyika walitoa hoja ya dharura kujadili mgomo wa madaktari maana watanzania wanakufa, kwa maana kuwa waahirishe kazi nyingine za Bunge ili wajadili jambo hili la muhimu. Bahati mbaya hoja zao hazikuungwa mkono wa wabunge kwa kusimama.

Ndipo Naibu Spika Ndugai akasema ni kweli hoja zao zina nguvu na wamefuata kanuni ya 47 ya taratibu za Bunge, ila tatizo hazijaungwa mkono, kwa hiyo tunaendelea na kazi za kawaida.

Ndipo wabunge wakachekelea kwa vicheko vya raha mustarehe utadhani ni jambo la kufurahia. Na nina shaka kuwa serikali inawachezea madaktari, nawaomba endeleeni kukaza uzi kama kawaida. Madam Spika anachelewesha kuruhusu tamko la serikali juu ya hili akiwa na uhakika kuwa madaktari watarudi kazini.

Naomba kazeni buti.

Hii ni safi sana. wamejitengenezea kitanzi cha kujitundika 2015
 
wabunge wote wamekataa kwa sababu wote hawajaunga mkono,hakuna cha ccm wala cdm hapa,acheni kupotosha ukweli.wote tunaangalia bunge msidhani nyie tu ndo mna tv
 
....Mheshimiwa Ndugulile na Mnyika walitoa hoja ya dharura kujadili mgomo wa madaktari maana watanzania wanakufa, kwa maana kuwa waahirishe kazi nyingine za Bunge ili wajadili jambo hili la muhimu. Bahati mbaya hoja zao hazikuungwa mkono wa wabunge kwa kusimama.

Ndipo Naibu Spika Ndugai akasema ni kweli hoja zao zina nguvu na wamefuata kanuni ya 47 ya taratibu za Bunge, Kanuni hii inasema hivi;

KANUNI ZA KUDUMU ZA BUNGE, TOLEO LA 2007

47.-(1) Baada ya Muda wa Maswali kwisha, Mbunge yeyote anaweza kutoa hoja kuwa Shughuli za Bunge kama zilivyooneshwa kwenye Orodha ya Shughuli ziahirishwe ili Bunge lijadili jambo halisi la dharura na muhimu kwa umma.

(2) Hoja ya namna hiyo itakuwa ni maalumu na inaweza kutolewa wakati wowote hata kama majadiliano yatakuwa yanaendelea.
(3) Hoja itatolewa na Mbunge kwa kusimama mahali pake na kuomba idhini ya Spika kutoa hoja ya kuahirisha Shughuli za Bunge
kwa madhumuni ya kujadili jambo halisi la dharura na muhimu kwa umma.

(4) Iwapo Spika ataridhika kwamba jambo hilo ni la dharura, halisi na lina maslahi kwa umma, basi ataruhusu hoja hiyo itolewe kwa
muda usiozidi dakika tano na mjadala juu ya hoja hiyo utaendelea kwa muda ambao Spika ataona unafaa kwa kuzingatia mazingira ya suala linalojadiliwa.


Ila tatizo hazijaungwa mkono, kwa hiyo tunaendelea na kazi za kawaida.Ndipo wabunge wakachekelea kwa vicheko vya raha mustarehe utadhani ni jambo la kufurahia. Na nina shaka kuwa serikali inawachezea madaktari, nawaomba endeleeni kukaza uzi kama kawaida. Madam Spika anachelewesha kuruhusu tamko la serikali juu ya hili akiwa na uhakika kuwa madaktari watarudi kazini.

Naomba kazeni buti.


Hizi ni hoja za kujitafutia umaarufu tu. Watu tumeisha anza kumfahamu Mnyika ni mtu wa show off zaidi kuliko utekelezaji

 
Ah tanzaniaaaaaaaaaa tatizo letu wananchi sijui tumelogwa na kijani yaaani wakifika tu dah kwisha kazi si tuungane tukiondoe madarakani.wabunge waakuja tu siku ikifika 2015.we waache tu mwaka huu maswali watayakoma
 
Andika lugha sanifu ueleweke, vinginevyo ulichoandika ni uozo!

Lugha sanifu unayoitaka ww ni ipi? Hujaelewa nini, mbona hushughulishi akili yako yani unataka aandike lugha gani utayoilewa, labda aandike lugha yako ya kijaluo!
 
Na wewe funguka na uelewe!, kwenye hizo kanuni za kuduma wapi kanuni inasema lazima mwongozo/hoja iungwe mkono na wabunge?.......
 
Kanuni za bunge ziko makini kwenye hili la hoja za dharura. Lakini, bunge likiwa na kanuni bora halafu likawa na wabunge ambao hata wao wenyewe wanakiri kuwa wana uwezo mdogo wa kufikiri, hizo kanuni ni sawa na 'pini ya dhahabu kwenye pua ya nguruwe'. Swala la wabunge kupuuzia watu wanaokufa kwa kukosa huduma ni sugu hasa vijijini. Mi nadhanani ni jipya kwa wakazi wa dar ila sisi wa vijijini tushazoea.
Hii ilikuwa hoja ya msingi, au kwa vile imetolewa na upinzani? tusijisahau, upendo, amani na umoja vina maana kwenye hili. Serikali itazame hili kitaalamu zaidi pamoja na uzalendo ndani yake. Tusifanye maafa kama haya kuwa mambo ya kisiasa. Ni ayo tu.
 
Watanzania tunavuna tulichopanda wala tusione vibaya kwa hili lililotokea leo Bungeni.Kwani hao wabunge waliingiaje bungeni? Si walichaguliwa na wananchi?

Je wananchi wanaokufa kwa kukosa huduma kwa vile madaktari wameweka mguu chini kudai haki zao, mbele ya Wabunge wana thamani gani?

Mimi binafsi nafurahi kuona kwamba sura za kweli za hawa wawakilishi zinajitokeza.


NA BADO HATUJAONA KITU!
 
CCM chama cha majambazi na matajiri kimelaaniwa na Mungu,si muda mrefu na hao Panya wadogo wanaowashabikia wote si muda watakuwa na laana kama Panya mwenzao wakubwa CCM
 
Back
Top Bottom