Wabunge wa CCM oneni aibu basi

mshale21

JF-Expert Member
Apr 8, 2021
2,050
4,904
Mifumo ya chama chenu enyi wabunge wa CCM, inaonekana kuwajenga katika misingi ya ushabiki, kuimba na kupiga mapambio juu ya watawala na viongozi wenye mamlaka mbalimbali.

Hebu tujikumbushe maneno ya 'BWEGE' kdogo, "UMESHIBA-NDIYO, UNA NJAA-NDIO" yaan wabunge mbumbumbu Kila kitu ndiyo limradi pendekezo au muswada umetoka kwa mtawala!

Hamjui mko hapo mjengoni il kutafakari badala ya wananchi kwa maslah ya taifa letu? Badala ya kujikita kwenye agenda zinazoshikilia mustakabali wa taifa letu mnajikita kwenye Legacy kuwa agenda ya nchi, mara vijembe kwa watu wanaosimama na kuwakosoa mfano CAG na MBOWE, mnageuza Bunge kuwa sehemu ya kufanyia propaganda na vichekesho mpaka Rais wa JMT anawaweka bayana kuwa mijadala inayoendelea bungeni haina afya!!! Shame on you!

Hitimisho
Kosa si kosa ila kosa kurudia kosa, jikiteni kwenye agenda znazoleta tija kwa maslah mapana ya nchi yetu, wote tunaipenda nchi yetu, tunaumia Sana mnapokwenda tofaut na majukum yenu ya kikatiba.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU IBARIKI AFRICA.
 
Unasahau au unajisahaulisha makusudi?

Wabunge waliopo bungeni hawajatokana na wananchi Bali ni wabunge wa magufuli aliowaanda kumsifia, kumshangilia na kumpigia vigelegele!

Mama Samia analijua vyema hili kuwa, wabunge wanamwakilisha magu na siyo wananchi ambao hawakuwapigia Kura ya kuchaguliwa!
Kifupi wananawakomeaha wananchi kwa ni hawakuwachagua!
 
Unasahau au unajisahaulisha makusudi?
Wabunge waliopo bungeni hawajatokana na wananchi Bali ni wabunge wa magufuli aliowaanda kumsifia, kumshangilia na kumpigia vigelegele!
Mama Samia analijua vyema hili kuwa, wabunge wanamwakilisha magu na siyo wananchi ambao hawakuwapigia Kura ya kuchaguliwa!
Kifupi wananawakomeaha wananchi kwa ni hawakuwachagua!
Una point
 
IMG_7099.jpg


Ngoma inapigwa MTANDAONI, wapangaji wa mjengoni wana DEMKA
 
Back
Top Bottom