Wabunge wa CCM ni wasaliti, Wamenunuliwa na majangili? - Uhuru

masopakyindi

Platinum Member
Jul 5, 2011
17,849
13,136
Katika kuonyesha kutofurahishwa kwa kusitishwa kwa Operation Tokomeza, wananchi wengi sasa wameanza kuamini kuwa ni vigogo, wengine ndani ya CCM na wabunge ndio wanaofadhili au kuneemeka na biashara haramu ya kuua tembo-rasilmali ya nchi.

Kwa mujibu wa gazeti la Uhuru , leo tarehe 6 Nov 2013, limasema,

"Wabunge CCM ni wasaliti-Wasomi
  • Waponda Operesheni Tokomeza kusitishwa
  • Waitaka CCM kuchunguza wasio wazalendo

WANANCHI wa kada mbalimbali, wakiwemo wasomi nchini, wamewashukia baadhi ya wabunge wa CCM, wakisema ni wasaliti na wanakwenda kinyume na malengo ya Chama na serikali.

Pia, wamekishauri Chama kuwa umefika wakati wa kuwachukulia hatua kali viongozi wake, wakiwemo mawaziri na wabunge, ambao watabainika kwenda kinyume na dhamira yake katika kuwatumikia Watanzania.

Kauli hizo zilitolewa kwa nyakati tofauti kutokana na mambo yanavyoendelea ndani ya Bunge, ikiwemo hoja mbalimbali za wabunge zinazowasilishwa, ambazo zingine zinadaiwa kuwa na sura ya maslahi binafsi zaidi.

Waliyasema hayo jana wakati wakizungumza na Uhuru, kutoa maoni kuhusu mwenendo wa Bunge na mustakabali wa rasilimali za taifa, wakiwemo wanyama, ambao wako kwenye hatari ya kutoweka kwa sasa.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Mohamed Bakari, alisema tatizo la uwajibikaji kwa baadhi ya viongozi ndiyo inayolifanya taifa lishindwe kufikia malengo.
Alisema baadhi ya viongozi ndani ya Bunge na Baraza la Mawaziri, wameshindwa kuwajibika kikamilifu, hivyo wamebaki kuwa watengeneza mizengwe dhidi ya wengine, ambao wameamua kulitumikia taifa.

Pia, alieleza kushangazwa na hatua ya baadhi ya wabunge kuungana kupinga Operesheni Tokomeza, ambayo ilikuwa na lengo zuri la kulinda rasilimali za taifa kutokana na kushamiri kwa wimbi la majangili. Alisema operesheni hiyo imekuwa na mafanikio mazuri, na kwamba ambao ilipaswa kuendelezwa, lakini baadhi wameamua kuipinga.

ìWapo waliopinga operesheni hii ya kudhibiti ujangili, hapa inawezekana kuna baadhi ya viongozi wanahusika na biashara ya nyara za taifa, hivyo ikiendelea mambo yao yatakwama, jambo ambalo ni hatari,î alisema Bakari. Kutokana na hilo, amesema ni vema CCM ambayo ndio imeshika dola ikafanya maamuzi magumu ya kuwaondoa viongozi wote wasaliti na wanaokwenda kinyume na dhamira ya Chama.
Pia, alisema changamoto nyingine za kimtazamo kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, jambo ambalo limewafanya baadhi ya viongozi kushindwa kushirikiana katika utekelezaji wa majukumu, hivyo kurudisha nyuma maendeleo.

Naye Mkuu wa Idara ya Sayansi na Utawala wa Umma katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Benson Bana, alisema hakurajia kama wabunge wangefanya maamuzi ya kupinga Operesheni Tokomeza, kwani lengo lake lilikuwa zuri.
Alisema wabunge walitakiwa kuwa mstari wa mbele kuunga mkono jitihada za serikali, ikiwa ni pamoja na kujitokeza kushiriki kwenye maeneo yao.
ìKitendo cha kupinga kinawafanya watu wahoji uzalendo wa wabunge wetu kwa sababu hakuna asiyefahamu madhara ya ujangili. Kupinga ni sawa na kuhujumu uchumi, jambo ambalo ni fedheha,î alisema.

Dk. Bana alisema operesheni hiyo ilikuwa nzuri na ilikuwa na mustakabali wa kulinda maslahi ya taifa, hivyo hakukuwa na sababu ya kubeza jitihaza hizo.
ìKama ningekuwa nachunguza kuhusu biashara hii, ningeanza kuangalia mienendo ya wabunge wote waliopinga na maslahi waliyonayo katika biashara hii, kimsingi maslahi ya taifa yanatakiwa yalindwe kwa gharama yeyote.

ìUmefika wakati wabunge wajielekeze katika kusimamia mambo ya msingi na yenye kulinda maslahi ya taifa, hakuna jambo zuri lisilokuwa na madhara na changamoto zilizojitokeza katika operesheni hiyo zilitakiwa kutatuliwa na mambo yakaendelea na si kuisitisha wakati tembo wanazidi kuuawa kila kukicha,î alisema.

Naye Johnson Mwakijambili, alisema viongozi wanapaswa kuacha unafiki mbele ya wananchi na badala yake wawajibike ili nchi isonge mbele. Pia, alishangazwa na hatua ya baadhi ya mawaziri kushindwa kuitetea Operesheni Tokomeza, ambayo ilipewa baraka katika vikao halali.

“Mawaziri wahudhurie vikao ili wasikilize hoja badala ya kutoroka, ndio haya mambo yanayofanya washindwe kutetea hoja na shughuli wanazokubaliana bungeni,” alisema.
 
CHADEMA igeni mfano huu tubadilike kwa kukabiliana na viongozi wabadhilifu wa rasilimali fedha za Chama kwani wanakwamisha. malengo ya Chama
 
Chadema igeni mfano huu tubadilike kwa kukabiliana na viongozi wabadhilifu wa rasilimali fedha za Chama kwani wanakwamisha. malengo ya Chama

Tubadilike..tangu lini wewe ukawa chadema? Ya chadema waachie chadema wenyewe!
 
Katika kuonyesha kutofurahishwa kwa kusitishwa kwa Operation Tokomeza, wananchi wengi sasa wameanza kuamini kuwa ni vigogo, wengine ndani ya CCM na wabunge ndio wanaofadhili au kuneemeka na biashara haramu ya kuua tembo-rasilmali ya nchi.

Kwa mujibu wa gazeti la Uhuru , leo tarehe 6 Nov 2013, limasema,
Ha ha haa mnafiki masopakyindi, hayo yangesemwa na Mh. Msigwa ungetokwa na mapovu ila kwa kuwa ni UHURU poa tu, utaunga mkono...TAIFA LA WANAFIKI waliolewa bendera ya kijani!
 
Last edited by a moderator:
Mmh, hao wabunge wenyewe wanajua hata kama wamenunuliwa? Sidhani.

Huwa nahisi wao kila wanalotetea wameaminishwa ni kutetea chama cha kiendelee kuwepo madarakani (Brain washed), wakikipinga na wao wanakuwa kwenye hati hati ya kupoteza madaraka yao.
 
Chadema igeni mfano huu tubadilike kwa kukabiliana na viongozi wabadhilifu wa rasilimali fedha za Chama kwani wanakwamisha. malengo ya Chama

Unataka Chadema waige nini toka kwa hawa wabunge na mawaziri majangili? Imedhihirika kuwa mtu kama Lukuvi ni jangili wa meno ya Tembo kwani msaidizi wake alikamatwa kwenye operation TOKOMEZA na yeye akawa mstari wa mbele bungeni kutaka operation isimamishwe kwani ingeendelea naye angetiwa mbaroni!!!Serikali inabidi ifanye uamuzi mgumu kuhusu majangili hawa na wala isiwaonee aibu!!!
 
Mmh, hao wabunge wenyewe wanajua hata kama wamenunuliwa? Sidhani.

Huwa nahisi wao kila wanalotetea wameaminishwa ni kutetea chama cha kiendelee kuwepo madarakani (Brain washed), wakikipinga na wao wanakuwa kwenye hati hati ya kupoteza madaraka yao.
Mkuu wabunge hao wala hawaitendei haki CCM ni masilahi yao binafsi.

Kusitisha Operation Tokomeza ni usaliti na tunaona kwenye luninga Wachina wanavyo vuna pembe kama wako kwao.
 
Ha ha haa mnafiki masopakyindi, hayo yangesemwa na Mh. Msigwa ungetokwa na mapovu ila kwa kuwa ni UHURU poa tu, utaunga mkono...TAIFA LA WANAFIKI waliolewa bendera ya kijani!

Mkuu Mag3, huyu jamaa masopakyindi ni mnafiq ajabu.
Mimi hata sijui anasimamiaga wapi.
Kweli ni kundi la Wanafiq waliolewa bendera ya kijani...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mag3, huyu jamaa masopakyindi ni mnafiq ajabu.
Mimi hata sijui anasimamiaga wapi.
Yaani anasubiri Mpaka Gazeti la Uhuru ndo limwambie kuwa wabunge wa CCM ni wasaliti plus Brain washed...ajabu sana aisee...
Kweli ni kundi la Wanafiq waliolewa bendera ya kijani...
 
Last edited by a moderator:
Katika kuonyesha kutofurahishwa kwa kusitishwa kwa Operation Tokomeza, wananchi wengi sasa wameanza kuamini kuwa ni vigogo, wengine ndani ya CCM na wabunge ndio wanaofadhili au kuneemeka na biashara haramu ya kuua tembo-rasilmali ya nchi.

Nnyambala, naona sasa unaelekea tunakoelekea wengine. Hii nchi ni ya kila mtu, tunapolalamikia maovu tuwe kitu kimoja. Rushwa na ujangili vinaathiri kila mtu, regardless anatoka chama gani.

OUT OF TOPIC
Hivi wewe na Simiyu yetu mpo chama kimoja?
 
Mkuu wabunge hao wala hawaitendei haki CCM ni masilahi yao binafsi.

Kusitisha Operation Tokomeza ni usaliti na tunaona kwenye luninga Wachina wanavyo vuna pembe kama wako kwao.

Kinachogomba hapo ni namna hiyo operesheni ilivyoendeshwa. mimi siamini kwamba kwa hali ilivyo sasa hivi, serikali hii inao uwezo wa kupambana na majangili, wauza madawa ya kulevya, na wengine kama hao. tatizo ni kwamba kuna wazito ndani ya biashara hizo. na hao ndio wanafanya operesheni ya kweli iwe ndoto. kinachoweza kufanyika ni vurugu tu hasa kuwaumiza watu wasio na uwezo wa kutoa rushwa. hata ukiangalia tatizo la wenye malori, utaona kwamba kisiki ni kwamba kuna vigogo waliojiingiza huko. wamehujumu reli ili wafaidike. na hiyo inafanya iwe ngumu sana kuchukua hatua stahiki. kilichotakiwa ni uongozi wa juu uwe tayari kabisa kupambana na rushwa na ufisadi kwa nguvu zote. lakini kwa kuwa mafisadi na wala rushwa wamejipenyeza katika mfumo mzima wa serikali, tutabakia kupiga kelele na kulalama tu
 
Ha ha haa mnafiki masopakyindi, hayo yangesemwa na Mh. Msigwa ungetokwa na mapovu ila kwa kuwa ni UHURU poa tu, utaunga mkono...TAIFA LA WANAFIKI waliolewa bendera ya kijani!
Mkuu tumia asilimia ndogo tu ya akili yako ya kuzaliwa na utueleze maudhui ya mada, kama inaunga mkono ujangili au la!
Nisingependa kukuingiza kwenye yale makundi ya watu wasio na uwezo wa kuchambua mada, ila wasindikizaji kwa vibwagizo.
 
Mkuu Mag3, huyu jamaa masopakyindi ni mnafiq ajabu.
Mimi hata sijui anasimamiaga wapi.
Yaani anasubiri Mpaka Gazeti la Uhuru ndo limwambie kuwa wabunge wa CCM ni wasaliti plus Brain washed...ajabu sana aisee...
Kweli ni kundi la Wanafiq waliolewa bendera ya kijani...

Sijisumbui kukuita mkuu, maana hustahili!
Maana nyie masalia ya F4F mna taabu sana.

Nakupa changamoto moja na iku keep busy mchana huu, hebu tafuta mada moja humu JF ambayo nimeunga mkono mafisadi, majangili au wezi wa EPA etc.

Tatizo la watu kama ninyi ni kuwa na akili za kuandamana tu kama Lema.
 
Nnyambala, naona sasa unaelekea tunakoelekea wengine. Hii nchi ni ya kila mtu, tunapolalamikia maovu tuwe kitu kimoja. Rushwa na ujangili vinaathiri kila mtu, regardless anatoka chama gani.

OUT OF TOPIC
Hivi wewe na Simiyu yetu mpo chama kimoja?
Tupo pamoja mkuu.
Watu wanachoshindwa kuelewa ni ukweli kuwa hata wana CCM damu damu wanaudhika sana na ufisadi ndani au nje ya chama chao CCM katika hali yoyote ile.
Likini siye wenye ngozi ngumu, tumeamua kubaki ndani ya chama hadi kieleweke.
Hakuna mwana CCM anapenda kuibiwa!

Mii ni mwana CCM damu damu, [MENTION]Simiyi yetu[/MENTION] changamoto hiyo, lakini naamini tupo pamoja.
 
Kinachogomba hapo ni namna hiyo operesheni ilivyoendeshwa. mimi siamini kwamba kwa hali ilivyo sasa hivi, serikali hii inao uwezo wa kupambana na majangili, wauza madawa ya kulevya, na wengine kama hao. tatizo ni kwamba kuna wazito ndani ya biashara hizo. na hao ndio wanafanya operesheni ya kweli iwe ndoto. kinachoweza kufanyika ni vurugu tu hasa kuwaumiza watu wasio na uwezo wa kutoa rushwa. hata ukiangalia tatizo la wenye malori, utaona kwamba kisiki ni kwamba kuna vigogo waliojiingiza huko. wamehujumu reli ili wafaidike. na hiyo inafanya iwe ngumu sana kuchukua hatua stahiki. kilichotakiwa ni uongozi wa juu uwe tayari kabisa kupambana na rushwa na ufisadi kwa nguvu zote. lakini kwa kuwa mafisadi na wala rushwa wamejipenyeza katika mfumo mzima wa serikali, tutabakia kupiga kelele na kulalama tu
Mkuu na mimi ninao walalamikia ni hao vigogo ndani ya hiyo biashara, lakini kusitisha zoezi kunaleta hisia kuwa kuna wana CCM wanaohusika na ndio wapigaji kelele wakuu.
Cha kufanya ni kwamba kama kuna walioonewa watetezi wao wangewasiliana na wansheria ili sheria ichukue mkondo wake on isolated cases.

Lakini kusimamisha operation hii mimi naichukulia kama uhujumu.
 
CHADEMA igeni mfano huu tubadilike kwa kukabiliana na viongozi wabadhilifu wa rasilimali fedha za Chama kwani wanakwamisha. malengo ya Chama


Usipotawaja chadema utajamba?yaani topic haziendani kabisa du kweli watu ni watupu mbaya,hamsaomi kazi kupost tu uchafu wenu,
GOD BLESS YOU
 
Sijisumbui kukuita mkuu, maana hustahili!
Maana nyie masalia ya F4F mna taabu sana.

Nakupa changamoto moja na iku keep busy mchana huu, hebu tafuta mada moja humu JF ambayo nimeunga mkono mafisadi, majangili au wezi wa EPA etc.

Tatizo la watu kama ninyi ni kuwa na akili za kuandamana tu kama Lema.
sasa wewe unapoambiwa achana na flan ni mwizi nawe unasema siyo mwizi, na unapomshuhudia anaiba unakubali kweli ni mwiz nimeshuhudia, unaambiwa tena achana naye hutaki inaonyesha na wewe ni mwizi, kama hupendi wizi ungeachana naye na ikibidi toa taarifa polis
 
Sijisumbui kukuita mkuu, maana hustahili!
Maana nyie masalia ya F4F mna taabu sana.

Nakupa changamoto moja na iku keep busy mchana huu, hebu tafuta mada moja humu JF ambayo nimeunga mkono mafisadi, majangili au wezi wa EPA etc.

Tatizo la watu kama ninyi ni kuwa na akili za kuandamana tu kama Lema.

Mara ngapi nimeshakwambi, Nenda pale Coet UDSM, zamani ilikuwa inajulikana kama Faculty of Electrical and Computer Systems Engineering halafu kaniulizie ndo ujue kama mie ni F4F au vp.
Btw, sihitaji kuitwa Mkuu na mtu mnafiq kama wewe
 
Operation iendelee kuwepo maana inasaidia kulinda maslahi ya wananchi, ikiaachwa hivi hawa Wachaga wataifilisi hii nchi.
 
Back
Top Bottom