Uchaguzi 2020 Wabunge wa CCM mpya ni mkakati maalum wa kubadili katiba, Paul Makonda na Alexander Mnyeti ni kishindo kikuu

Tetesi

Members, wasibezwe hili kundi la CCM mpya na waongeaji watapita kwa kishindo kikuu kwa lengo maalum bungeni kubadili katiba na Kuongeza muda wa Rais kutawala

Kauli ya Rais mstaafu Mwinyi sio mara moja au kwa bahati mbaya anapenyeza kauli ya kubadili Katiba kuhusu ukomo wa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

Watu wafuatao ndio watakaoendesha bunge na kuwa waongeaji wakuu bungeni. Hakuna atakaye nyanyua mdomo wake kuwapinga watu wafuatao bungeni:

Paul Makonda
Cyprian Musiba
Alexander Mnyeti
Mchungaji Gwajima
Tulia Ackson

Waliotajwa wataingia bungeni kimkakati na siyo kwa bahati mbaya. Hoja zao ndio zitakuwa za mwisho kwa maamuzi ya Taifa.

Paul Makonda, Alexander Mnyeti, Mchungaji Gwajima na Cyprian Musiba msiwachukulie kirahisi na kuwadharau, Hao watu ni wajenga hoja wazuri tena za kulazimisha utake usitake lazima uwaunge mkono ili ubaki salama kwenye CCM mpya.

Hakuna cha mpasuko wala ufa CCM. Sauti ni moja tu yenye nguvu na kuheshimiwa. Hakuna mwenye uwezo wa kumpinga Mwenyekiti wa chama wala kunyanyua mdomo kuhoji maamuzi ya Mwenyekiti.

Mwenyekiti amepitishwa kwa asilimia 100%. Hii inampa nguvu ya kuaminiwa na yeyote atakaye ongea kuhusu kura za maoni kwa upande hasi hasa za ubunge basi atafute Maisha mengine nje ya bunge na CCM mpya.

CCM ni moja na yenye nguvu zaidi, Wapinzani tafuteni mbinu mpya, CCM imempa mamlaka ya asilimia 100% Mwenyekiti kwa kupiga kura za ndio Dodoma, Sauti yake ni sauti kuu. Hakuna mwanachama atakaye tenda nje ya Maamuzi ya Chama

Wapinzani msisubiri eti CCM kutakuwa na mpasuko ili mpate hoja za ubunge, Bunge linakwenda kuwa la kimkakati kupitisha hoja maalum ya ukomo wa Rais madarakani.
Hakuna aliyetumwa.... so that's nonsense na hao wote hasa waliozaliwa 1982 watachinjiliwa mbali !!
 
Hakuna aliyetumwa.... so that's nonsense na hao wote hasa waliozaliwa 1982 watachinjiliwa mbali !!
Kama mwaka 1982 ameutaja kwa ndimi ya maji ni sawa ila kama ni kwa ndimi ya moto, tegemea ambacho hujakitarajia.

Tukumbuke Jiwe ana ndimi mbili, moja ya maji na nyingine ya moto na zote zina nena ukweli na ukweli usio mkweli.
 
Hii iwe funzo kwa waasisi wa katiba mbovu inayompa mamlaka yasiokuwa na ukomo mtu mmoja kwenye nchi.Pia vyama kutokuwa na nguvu ya kumdhibiti rais.
Kwa kweli Tanzania inapitia kipindi kigumu labda Mungu aingilie kati huko mbeleni kwa kupindua meza kibabe.
Nyerere alituachia katiba mbovu kabisa. Katiba ya kumfanya mtu mmoja kuwa kama mungu mtu. 🤦‍♂️
 
Jamani Mh. Rais kasema wazi, hawezi ongeza muda, muda wake ukiisha anaondoka zake, kwanini mnamsemea maneno ya uongo, lini Mh. Rais kasema anataka kuongeza muda? Huku ni kuchafuana, acheni hizo plz
Anasema mdomoni lakini matendo ni tofauti kabisa
 
Dalili zinaonekana, mtu kama Musiba anataka kwenda bungeni kufanya nini?!

Amesifia kwenye gazeti lake ameona hiyo haitoshi sasa anataka kupeleka mapambio yake bungeni, hilo bunge lijalo linaweza kuwa la hovyo zaidi ya lile lililopita la Ndugai.
Usukumanisation?
 
Wafanye wanavyofanya watu watazoea na wakishazoea.

Hakuna watu wajinga kabisa.Vitu vyote vizuri vita perish kwa muda mfupi sana.Na hii ndio tabia kuu ya Binadamu..
 
Maswala yote yahusuyo corona na hili la kuingia uchumi wa kati kutangazwa muda mfupi kabla ya uchaguzi imekoleza sana umaarufu wa Magufuli. Magu sio level za akina Mbowe na Zitto, wapinzani msitegemee kuambulia chochote october. Magu hana nia ya kuongeza muda though personally ningetamani afanye hivyo ili atusogeze hadi uchumi wa juu if possible, nchi ilishachezewa sana hii. Kwa wavivu wote wa kujituma kazini povu litawatoka.
 
35 Reactions
Reply
Back
Top Bottom