Wabunge wa CCM mnawachezesha Watanzania "kwata" la akili!

Sipendi sana mazingaombwe:

Chama chenu
Serikali yenu
Sera zenu
Sheria mtunge nyinyi
Vyombo vya usalama vyenu
Watendaji mteue nyinyi
Majaji wote mmeteua nyiyi
Wakuu wote wa vyombo vya usalama mmewatua nyinyi
Mwanasheria Mkuu wenu
DPP wenu
Ikulu yenu
Bunge lenu
Mawaziri wote wenu
Manaibu wote mawaziri wenu

LAKINI MNA UJASIRI WA KURUKA KIMANGA KANA KWAMBA SERIKALI IMEUNDWA NA CHADEMA na wapo watu katika akili timamu kabisa wanafurahia haya maonesho yenu!! Kama kweli leo mmefunguka na kukombolewa kifikra basi fungeni kamili! Fungeni na mtoke kwenye giza na kuja kwenye mwanga. Hamhitaji kusubiri 2015! Jiuzuluni leo hii ili mjipe nafasi na kuhesabiwa! Vinginevyo, watacheza kwata wale wenye kuamini mnaweza kuwapigisha kwata la akili!!


HAYA YALIKUWA 2008 - SIKILIZENI KWA MAKINI WANAYOSEMA WABUNGE WA CCM HALAFU MSEME KAMA LEO WAMEFUNGUKA?


Well said MM. CDM tusirudie tena makosa ya 2010 kuwaingiza watu kama Shibuda. Yeyote anayetaka kuingia kwenye historia ya mabadiliko ni lazima atoke hadharani sasa ili ahesabiwe.
 
Makelele yooote yale. Wana uwezo wa kuleta hoja binafsi kuziba mianya ya sheria na kuongezea nguvu sheria dhaifu. Au kama Mwanakijiji alivyosema, wana weza kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu. Hivi si katika bunge la mwaka jana tu Serukamba alimtolea macho Zitto akimkoromea eti "wapinzani wana nongwa kungangania" wabunge waondolewa kwenye bodi za wakurugenzi kwenye mashirika ya umma. Leo hii ndo anajifanya kukoremea serikali yake? Wabunge wa CCM ni wanafiki wa kutupa!

Serukamba is the last one to decry impotence in CCM and its government..
 
MM wewe ni mchokozi sana, nimesikiliza kwa makini haya yanayozungumzwa sasa na hizi clip za 2008 ulizotuwekea nikaumia sana. Hawa watu (wabunge wa CCM ni wanafiki, na hawapaswi kuaminiwa kirahisi kama wanavyotaka iwe sasa. Matendo yao hayapo pale midomo yao ilipo. Cha kushangaza sasa asilimia kubwa ya wale waliokuwepo bungeni 2008 bado wapo humo sasa. Sijui na sisi wapiga kura tuna matatizo gani?????

Sasa ukipitia ule Mjadala, wa Mpango wa Miaka Mitano ndio aibu tupu!. Watu walikuwa wanaongea utadhani matatizo ya wananchi yameshatatuliwa kabisa wakati ukitoka tu nje ya Bunge sukari ilikuwa ni Tsh. 2300/=! (Mwaka jana). Nadhani umefika wakati wa kuwapinga kile wanachokisema sasa, kwa kujikita kwenye misimamo yao ya awali iliyopo kwenye Hansard za Bunge.
 
Kura ya kutokuwa na imani itatu cost sisi wananchi pia, inamaana bunge lote linavunjwa tunaanza moja. Hapana sikubaliani na hoja ila noana kuna haja rais avunje hii baraza abadilishe safu tena.

Bunge haliwezi vunjwa mazee ila Mawaziri ndio watapangaranishwa au kufukuzwa, kuhusu cost mbona marehemu Baba wa taifa alishasema democrasia ni aghali hivyo tuvumilie tuu, wenzetu Kenya kuipata democrasia waliyonayo na wanaitumia hivi sasa wao walimwaga damu kwanza na kwa nini sie tuogope cost? Naamini hoja ya kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu kama ingekuwa leo ni 2014 ingepita haraka sana bila ubishi lakini kwa hivi sasa ni vigumu sana kwani wengi wa wabunge wa CCM bado hawapendi kumuudhi aliyewaweka hapo lakini
 
I love JF. Hakika MM umenena ya msingi. Tunahitaji muda kuwaamini hawa wabunge wa chama cha mapinduzi ili tujuwe kama kweli wameamua kukipindua chama chao. Maana tulishawahi kuwa na G55, vilevile tulishakuwa na wapambanaji wakati wanaopambana nao ni mabosi wao... KUWASHINDA NI NGUMU. Wengine walitaka kuanzisha CCJ lakini bado wapo kule kule... Siyo wa kuwaamini kirahisi hawa
kwangu mimi ccm wote ni wachumia tumbo waliokosa nafasi yaani ni midokozi tu
 
Bunge haliwezi vunjwa mazee ila Mawaziri ndio watapangaranishwa au kufukuzwa, kuhusu cost mbona marehemu Baba wa taifa alishasema democrasia ni aghali hivyo tuvumilie tuu, wenzetu Kenya kuipata democrasia waliyonayo na wanaitumia hivi sasa wao walimwaga damu kwanza na kwa nini sie tuogope cost? Naamini hoja ya kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu kama ingekuwa leo ni 2014 ingepita haraka sana bila ubishi lakini kwa hivi sasa ni vigumu sana kwani wengi wa wabunge wa CCM bado hawapendi kumuudhi aliyewaweka hapo lakini

Ili hili litokee, labda ipigwe kura ya kutokuwa na imani na rais.
Kinachopendekeza ni kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu. Matokeo yake ni baraza la mawaziri kuvunjwa
 
Niliwahi sema mara kadhaa....huwezi kuwa na akili timamu ukafurahia matendo ya CCM na viongozi wake......lazima uwe kichaa
 
Mwanakijiji,
Hii yote inaitwa tishia Nyau yaani mtu mzima huwezi kumtisha kwa paka isipokuwa mtoto mdogo ndiye ataogopa Paka..Hawa wabunge kabla ya uchaguzi wa Arumeru na huu wa Ubunge wa EA walisema wazi ktk vijikutano vyao bunge lililopita, kwamba wasipopewa ongezeko la posho za kukaa, watapiga kura ya kutokuwa na imani na serikali ya JK au yeye mwenyewe JK avunje Bunge tusiwe na wabunge kabisa ati lijulikane moja.

Sasa ktk harakati zao za kuzua mbinu wamekuja na hii mpya kurudia yale yaliyokwisha semwa miaka mitano iliyopita. Na wajinga wengi wataigia lakini kinachogombewa hapa ni Posho tu hakuna jipya kwa sababu hao mawaziri wanavuta posho kubwa serikali ktk vikao vyao vya kiwizara wakati wabunge wengine hawana pa kuvuta isipokuwa posho hizi..Hakuna mbunge yeyote hapo amesimama kwa maslahi ya Taifa bali kuchumia tumbo tu - Hatudanganyiki!
 
CDM wasiingie kwenye mtego wa kelel zao, shida ni kuzima moto wa upinzani- of course naamnisha CDM, maana wengine wameamua kuwa wapinzani butu!!
 
Angalia watu walichozeshwa kwata jana!!! na miye na ujanja wangu wote nikakaa naangalia TV tangu dakika ya mwanzo ya kipindi cha Bunge kuona 'mawaziri nane waliojiuzulu" usiku wa kabla yake!! Kumbe ni kupigishwa kwata!

THE BEST KITAKACHOTOKEA NI Rais kuamua kufanya reshuffle au kuvunja baraza which as I said before WON'T change the fundamental problem.
 
Angalia watu walichozeshwa kwata jana!!! na miye na ujanja wangu wote nikakaa naangalia TV tangu dakika ya mwanzo ya kipindi cha Bunge kuona 'mawaziri nane waliojiuzulu" usiku wa kabla yake!! Kumbe ni kupigishwa kwata! THE BEST KITAKACHOTOKEA NI Rais kuamua kufanya reshuffle au kuvunja baraza which as I said before WON'T change the fundamental problem.

inahitaji elimu ya uraia kwa kwenda mbele maana hata bunge likivunjwa uwezekano wa ccm kurudi na majority upo. hili vuguvugu ni la watu wa mijini tu ambao hawafiki hata 20% ya population.
 
Angalia watu walichozeshwa kwata jana!!! na miye na ujanja wangu wote nikakaa naangalia TV tangu dakika ya mwanzo ya kipindi cha Bunge kuona 'mawaziri nane waliojiuzulu" usiku wa kabla yake!! Kumbe ni kupigishwa kwata!

THE BEST KITAKACHOTOKEA NI Rais kuamua kufanya reshuffle au kuvunja baraza which as I said before WON'T change the fundamental problem.

Mkuu mwanakijiji,kumbuka watawala wetu wakishayapata madaraka hugeuka kuwa miungu watu,hii ni mbaya hatari sana.wanaonesha dharau kwa watz,wanajeuri na wamelewa madaraka huu ni utovu wa nidham kwa watz,naumia sana na inanipa shida kuelewa dhana hasa ya wanayoyafanya ni kwa kusudi gani,demokrasia inanyongwa hakuna haki,viongozi wezi na hawana utu je kuna tofauti gani kuwachukua wezi ambao wamethibitika na mahakama pale ukonga ama segerea na kuwa uongozi sioni tofauti,nadhani kama wabunge wa ccm wanadhani hawajaridhika kama sisi wananchi tusivyoridhika waombe kuitishwa kikao cha dharura baada ya siku 14 ili wapige kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu,ili kama kuwatoa mawazisi imeshindikana liundwe baraza jipya la mawaziri japo mwanakijiji umeshauri waende mbali zaidi,bt kwanza waanze na hili la wm halafu wakiona tatizo zaidi vonoco na rais itaweza kupgwa.so wakasaini ile karatasi mhm kama wanania njema
 
Ktk suala la kujiorodhesha kwenye karatasi ya Zitto wamezidi kujiachia uchi zaidi. Hawana lolote la kusaidia nchi hii. Unafiki wao sasa umefika kikomo. Nani atawaamini tena? Labda zumbukuku kama wao. Hata wakichaguliwa watu wa darasa la saba wanaweza anglau kufanya maamuzi ya maana kuliko hawa wabunge wa CCM. Hawa wanadhalilisha sana wasomi. Wasomi gani hawa wanaona nchi inazama wanazama nayo kwenda kufa nayo wakati wana uwezo wa kuinusuru? Ndo maana wanashinda kwenye ushirikina tu wakipigwa chale mwili mzima na mtu ambaye hata darasa moja hana. Kuwa CCM ni kuwa msaliti wa Taifa. Ukereketwa gani huu wa kupofusha macho na kupumpaza akili? Hawa watu wanasafiri sana kwenda nchi za watu, hakuna hata moja wanaweza kuiga na kulifanya hapa nyumbani. Kazi yao kubwa ni kusifia nchi zilizoendelea utadhani maendeleo yameshuka yenyewe. Hawa ni watu wa kumwagiwa tindikali wote maana ni hasara na mzigo mkubwa kwa nchi yetu.
 
Back
Top Bottom