mwengeso
JF-Expert Member
- Nov 27, 2014
- 9,219
- 6,650
Kwamba ili Serikali ya Awamu ya Sita ikamilishe miradu ya kimkakati, ilianza wakati wa Serikali ya Awamu ya Tano na kuboresha Huduma za Jamii (Afya, Elimu, Maji nk) ni kuweka tozo kwenye miamala ya simu, ati ni TOZO SHIRIKISHI.
Hakuna ubishi kuwa mmewagusa watu wa kipato cha chini ambao hutegemea miamala ya simu kwa shughuli zao za maendeleo na kijamii. Hao ndio wapiga kura ambao Serikali ya Awamu ya Tano iliwajali na kuadabisha mafisadi.
Mmemhujumu Rais Samia Suluhu Hasan kupitisha sheria hiyo. Kuanza kutekelezwa kwa hiyo sheria haraka haraka bila Kanuni na Taratibu kuwekwa wazi, ni ushahidi wa hoja yangu.
Wakati mnapata malipo na marupurupu mengi yasiyo na kodi, mtambue mmewakosea wapiga kura na mtaadhibiwa kama Wabunge kwenye sanduku la kura. Mmekichimbia kaburi chama chenu.
Hakuna ubishi kuwa mmewagusa watu wa kipato cha chini ambao hutegemea miamala ya simu kwa shughuli zao za maendeleo na kijamii. Hao ndio wapiga kura ambao Serikali ya Awamu ya Tano iliwajali na kuadabisha mafisadi.
Mmemhujumu Rais Samia Suluhu Hasan kupitisha sheria hiyo. Kuanza kutekelezwa kwa hiyo sheria haraka haraka bila Kanuni na Taratibu kuwekwa wazi, ni ushahidi wa hoja yangu.
Wakati mnapata malipo na marupurupu mengi yasiyo na kodi, mtambue mmewakosea wapiga kura na mtaadhibiwa kama Wabunge kwenye sanduku la kura. Mmekichimbia kaburi chama chenu.