Wabunge wa CCM kuonesha kutokuwa na imani na serikali lazima kuwe na matokeo

Nitakuwa wa kwanza kushangaa kama Pinda hata jiuzulu kutetea na kulinda hadhi yake

Kwa jinsi ninavyoijua mimi TZ hii ya ******, Pinda hatojiuzulu na wabunge watafyata mkia kila kitu kitaendelea kama ilivyo, hakuna viongozi responsible hapa, sahau.. ni ulaji tu....
 
Pinda hawezi kujiuzulu na Bunge la chama chake likabakua . Akijiuzulu LAZIMA Kikwete avunje na bunge ili wote waanze upya.
 
Asa mbona unawashtua mkuu?

Ukiwa unawastua kiasi hichi tutajua siku hizi hauko nasi.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Wabunge wa CCM wanagongana na serikali yao. Wanainyanyasa na kuimbua mbele za watanzania. Nimewahi kuandika huko nyuma kuwa ni jukumu la upinzani kudhoofisha serikali iliyoko madarakani ili ianguke na hata ikibidi ilazimike kuitisha uchaguzi mapema (early election). Nikasema wakati ule kuwa siyo jukumu la upinzani kuisaidia CCM kutawala. Sasa kinyume cha hilo nacho ni kweli. Jukumu la wabunge wa CCM ni kukitetea chama chao na hasa serikali yao isije kuanguka.

Kwa miezi ya karibuni sasa wabunge wa CCM wanaonekana kuwa na mgongano na serikali yao. Maneno yao makali na hata misimamo mikali dhidi ya mawaziri wa serikali hiyo ni mashambulizi ya wazi, dhahiri na yaliyopangwa. Upande mmoja ni wazi wapo ambao wanafanya hivyo kama sehemu ya political triangulation lakini wapo pia wanaofanya hivyo kama sehemu ya tofauti ya msingi kati yao na chama chao. Ni hawa wa kundi la pili ndio ambao hasa nawazungumzia kwani wale wengine wanafanya kwa ajili ya kugeresha wapinzani na kuwahadaa watanzania ili CCM izidi kutawala.

Hata hivyo kwa kundi hilo la pili ambalo kweli lina tofauti za msingi na serikali yao na wameonekana kuwa na uadui wa wazi na baadhi ya watendaji wa serikali (open hostilitiy) hawawezi kuwa hivyo bila kuwa na matokeo. Nina maana ya kwamba wabunge wa chama tawala wanapoamua kugongana na serikali yao kwa kuonesha kutokuwa na imani nayo basi lazima wawe tayari kuishi na matokeo ya msimamo huo.

a. Walipoamua kukataa bajeti ya Wizara ya nishati na Madini kwa maneno makali hadi kulazimisha serikali kuiondoa walionesha kutokuwa na imani na serikali. Kwamba, hawakuamini serikali ingeweza kuleta bajeti nzuri na yenye manufaa kwa wananchi na jinsi walivyomshambulia Ngeleja - mteuliwa wa RAis - walijionesha wazi kuwa wana matatizo na Kikwete mwenyewe.

b. Ilipokuja bajeti ya Uchukuzi navyo ilikuwa hivyo hivyo; walizungumza kwa ukali sana na wengine tulishangaza na kauli za baadhi ya wabunge hao wa CCM ambazo zilionesha wazi kuwa walikwua na tatizo na wizara hiyo na hata Waziri wake Bw. Omar Nundu.

c. Likaja suala la David Jairo - ambalo ukiangalia sana unaweza kuona kabisa kuwa linashambulia sehemu zote mbili; kwanza linashambulia upande wa wizara na pili upande wa Ikulu. Sasa maendeleo ya leo Bungeni yanatudhihirishia kuwa wapo wabunge wa CCM ambao kweli wanatofauti na serikali. Ni lazima iwe ni tofauti na serikali kwani naogopa kusema kuwa ni personal.

CAG aliitwa kufanya uchunguzi akafanya na akatoa ripoti yake kuwa hakuna utaratibu uliokiukwa na Ikulu kwa kutegemea taarifa ya CAG wakaamua kutangaza wanamrudisha Jairo kazini. Hili likanikumbusha jinsi CAG alivyoisafisha benki kuu kuhusu tuhuma za matumizi mabaya ya fedha kwenye ujenzi wa nyumba za magavana. Kwa wanaokumbuka pamoja na uzito wa jambo lenyewe CAG aliaminiwa kutoa taarifa na aliposema kuwa "value for money standard" na kuwa "hakuna taratibu iliyokiukwa" tukaambiwa tukubali kwani ulikuwa ni uchunguzi huru. Sasa CAG huyu huyu ameisaifisha serikali watu hawataki!

Well, haiwezekani wakatae na wakabakia. Hivyo lazima kuna matokeo na matokeo lazima yawe mazito vile vile.

a. Pinda kwa upande wake ameachiwa uamuzi mmoja tu. Kama alimshauri Rais Kikwete kuwa Jairo afukuzwe na kama aliamini kabisa kuwa - kutokana na taarifa alizokuwa nazo - kuwa Jairo hakupaswa kuendelea basi hawezi kubakia Waziri Mkuu tena. Nyerere aliweka standard kwenye sakatala la Tanganyika, Mwinyi na Mzee Malecela. Alisema Waziri Mkuu huwezi kumshauri Rais kitu naye akakataa halafu ukarudi na kumshauri kitu kingine juu ya jambo lile lile tena kwenye mambo ya msingi. Akasema Waziri Mkuu ukimshauri Rais jambo na amekataa na unajua uko sahihi unatakiwa kujiuzulu ili Waziri Mkuu mwingine aje na kutoa ule ushauri mwingine. Pinda, NI LAZIMA AJIUZULU kama aliamini msimamo wake wa awali kuhusu Jairo ulikuwa sahihi - na bila ya shaka akijiuzulu na baraza la mawaziri litavunjika.

b. Kikwete anaachiwa uchaguzi mmoja tu. Tayari Bunge limeonesha kutokuwa na imani na teuzi zake na maamuzi yake. Sina tatizo na wabunge wa upinzani kuonesha kutokuwa na imani huko lakini wabunge wa chama chake mwenyewe wanapofanya hivyo ni lazima arudishe nidhamu au awape matokeo. Nyerere tena alionesha kiwango; wakati fulani Bunge lilipomkatalia kupitisha mswada wake aliwaambia wazi kuwa ni jukumu lao kufanya hivyo lakini wakifanya hivyo basi atavunja Bunge waweze kurudi kwa wananchi. Ninaamini, wakati umefika kwa Kikwete kuwaambia wabunge wake kuwa yuko tayari kuvunja Bunge kama wabunge wake hawawezi kufanya kazi na serikali yake ili warudi kwa wananchi.

Bila ya shakahilo ni gumu kwani kwa kuvunja Bunge na yeye mwenyewe atatakiwa kurudi kugombea tena; swali litakuwa ni nani atarudi Bungeni au Ikulu. kama kweli wabunge wa CCM wanaamini serikali ina matatizo na hawana imani hivyo nayo basi wawe tayari kukutana na matokeo ya msimamo wao huo. Wawe tayari kurudi kwa wananchi. Hivyo Kikwete alitake Bunge kupiga kura ya kuwa na imani na waziri Mkuu au la. VEry simple. Kama wabunge wa CCM hawana imani na serikali yake watampigia kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu na hivyo Waziri Mkuu atatakiwa kujiuzulu; na Waziri Mkuu akijiuzulu Kikwete atangaze kuvunja Bunge kwani hawezi kuchagua baraza kutoka kwa wabunge wale wale na hivyo kama wanataka kuanza upya yuko tayari kuanza upya kabisa na uchaguzi mpya.

Ninachosema ni kuwa lazima kuwe na matokeo!!

I wish all of that could happen!!
 
Ni sheria na taratibu ziko wazi lakini naomba kuwaambia kuwa HAKUNA ATAKAYEJIUZULU NA MAISHA YATAENDELEA KAMA KAWAIDA NA tutanyamaza na kuendelea na mambo mengine ya uchaguzi wa Igunga tuko warahisi sana kusahau na Rais 5ml people ameshaligundua hilo anacheza karata zake vizuri kabisa.
 
Nitashangaa kama akijiuzulu, kwa tz hii hii, we subiri 2 wataitwa kwenye kikao cha magamba alaf uone, hakuna cha kuombana radhi wala kujiuzulu
 
Lakni JK mwenyewe aliwaaambia katikahotuba yakemja hataki wabunge wa ndio mzeee . Kama mamneno yale aliyasema kutoka moyoni basi naye atakuwa anafurahi.......

Nadahni kwa sasa comedy ya wabunge inazidi rating hata ile the comedy ya kina joti .

Kwanza ni vizuri tukijua kuwa kama ikija issue ya kura kuhusu imani na rais, kura zitapigwa in party lines, wabunge watatakiwa kupiga kura kwa misingi ya misimamo ya vyama vyao. Na sio kwa jinsi wanavyoona ni sahihi au si sahihi. Kwa hiyo hata siku moja usijetegemea kwa mahesabu ya idadi ya wabunge wa sasa kukajapigwa kura ya imani na rais.

Ukiangalia kauli za JK huwezi kusema ni kauli zenye vitendo, kwani wabunge wa CCM wanafanya exactly walichoambiwa na JK wasifanye.
 
Matokeo ya hii isue si mazuri kwao so ni ngumu sana hata kwa wao kupga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu maana itawa affect wao pia, tanzania ni zaidi ya nchi...
 
Nitakuwa wa kwanza kushangaa kama Pinda hata jiuzulu kutetea na kulinda hadhi yake

Kichwa kinanizunguka. hivi hiyo heshima yake atakayolinda ni ipi??? Labda tuseme ile ya kupigiwa king'ora barabarani na magari kuendeshwa mbio za kufa mtu, na watu wote kusimamishwa ili mkubwa apite kwanza. Lakini kama ni heshima nyingine ziliishadondoka siku nyingi na ndiyo maana hata luhanjo akasahau kuwa yuko waziri mkuu. Shughuli ipo hapo...
 
Mambo rahisi rahisi kwa serikali rahisi na serikali ina yachukulia rahisi rahisi na wananchi rahisi rahisi na wanachukua maamuzi rahisi rahisi kwa ishu wanazoziona wao kuwa ni rahisi rahisi tutawaliwe rahisi rahisi hivihivi mpaka tushike adabu nakujua kudai hakizetu kwanguvu na bado chekenichekeni tu kama Rais wenu Kilaza alivyo rahisi rahisi.
 
Hakuna cha matokeo; Kama ulisoma vizuri ile barua ya Jairo, ilisema "kama ilivyo kawaida yetu", na jana Luhanjo amesema hili suala hufanyika kila mwaka na siyo kwa wizara hii tu bali na wizara nyingine, hata alipokuwa katibu mkuu wa wizara walikuwa wakifanya hivyo hivyo. Unaona basi kuwa hii ni kawaida ya kila mwaka. Sasa je pesa hizo nani huzipokea? Ni wazi wapitishaji wa bajeti ndio huzipokea, na hao ni wabunge. Sasa leo watamhukumu vipi wakati pesa wamepolea wao? Ndiyo maana Luhanjo, Ngereja na Jairo wana jeuri; walishawanunua wabunge - yaani wanaijua bei wabunge!
Katika hali hiyo unatarajia matokeo gani? Wabunge wanalia kilio cha mamba machozi yanaishia baharini; hawana tofauti na yule aliyeanzisha thread akimwambia mbunge wake kuwa yale mablanketi na pilau ulivyotupatia tukakuchagua vimekwisha sasa ni wakati wa kuwatetea wananchi; akajibiwa kuwa pilau na mablanketi hayo yanaisha mwaka 2015 kwa sasa alie tu.
Haya ndiyo matokeo ya wabunge posho!
 
Kuna athari mbili kwa Kilichomtokea Jairo kupitia kwa Mh JK

1. Kuvurugika kwa mwenendo mzima wa bunge letu ...Kwani Haikuwa mategemeo yao kwa kilichotokea...Ni Kweli Pinda ajikague..!

Hili halinihusu sana kwa leo pia limeongelwa na wengi!

2. Mwenendo Mzima wa Heshima ya serekali mbele ya wanachi wake.

Hili niliongelee kidogo.

Wananchi wengi walitegemea kuwa alichosema PM ndio sahihi dhidi ya Jairo (Na ninaamini hivyo pia). Kwahiyo Matokeo ya Jairo kurudishwa kazini ni SHOCK KWA TAIFA ZIMA! Imekuwa kinyume kabisa na mategemeo ya Jamii. Hii ikiwa na maana kuwa HESHIMA YA SEREKALI inazidi kudidimia ... Hii ina maana gani! SEREKALI YA TANZANIA HAINA SIFA YA KUAMINIKA MBELE YA RAI WAKE na KUITII NA KUIHESHIMU linakuwa jambo gumu na lenye kutatiza umma wa Kitanzania!

Wanachi wataamua kujiongoza wenyewe... wasukuma mikokoteni ..wataaamua mambo yao..
Waendesha Pikipiki, Bajaji, Taxi, Daladala, Mabasi ya mikoani ..Wote watajiamulia mabo yao kwani SEREKALI HAIHESHIMIKI Na INATIA AIBU!

Makundi mabalimbali ya kijamii yatajiongoza yenyewee .. Wanafunzi, Wauzamitumba, wafanyakazi, Madaktari, waalimu wote hawa Watajiamulia mambo yao nk ..maana SEREKALI HAIJIHESHUMU NA HAIJABAKIZA CHOCHOTE KINACHOFAA KUHESHIMIKA...INATIA ABU TAIFA INALOLIOGOZA ....

Kwa udhaifu dhahiri wa kushindwa kuamua kinachotakiwa kuamuliwa na kushindwa kuchukua hatua sahihi ..SEREKALI HII INAIPELEKA NCHI HII KUTOKUWA NA UONGOZI .. Na hakuna asiyejua madhara ya jambo hili ...Kila mtu au kila familia itajiongoza yenyewe..Daladala ikipinda njia ... wauza mitumba wa sehemu hiyo ..wanaichoma Moto ...Polisi akimshika mwananchi .. polisi anachomwa moto pamoja na kituo chake...Nk

Namsihi Mheshimiwa JK na serekali yake ...wasifanye mzaha na maisha ya Watanzania!!
 
Sidhani kuwa Rais anatakiwa kukubali kila pendekezo linaloletwa kwake na Waziri Mkuu. Naamini kabisa kuwa marais waliopita kumekuwa na wakati ambapo rais amekataa mapendekezo ya Waziri Mkuu. Au hata Rais kubadilisha decision aliyofanya Waziri Mkuu [e.g. Nyerere kubadili uamuzi wa Waziri Mkuu Kawawa kufunga maduka yote vijijini katika miaka ya sabini].
Tatizo la Pinda ni alikwenda public na mapendekezo yake kwa Rais ya kutaka Jairo afukuzwe kazi bila kujua ni nini yalikuwa mawazo ya Rais. Hapo naamini kabisa Pinda alikosea kusema recommendation yake kwenye Bunge kuwa Jairo afukuzwe kabla hata hajapewa nafasi ya kujieleza. Hii ilikuwa nikurudi kwenye zile enzi za civil servants wakifukuzwa kazi kwenye redio bila kupewa nafasi ya kujiteteta wakati mwingine on the basis of majungu.
 
Hii ni miongoni mwa sinema nyingi tunazoendelea kuoneshwa na serikali hii ya JK. Natarajia kuona nyingi zaidi siku za usoni. Ni wajibu wa wananchi kuamua kuifukuza kazi serikali ya ccm ili tupunguze mizaha na kuwa na serikali makini inayojali maslahi ya Taifa.

Sijui vipaumbele vya serikali hii ni vipi, lakini kwa watu kuamua kuchangisha 500million ili kuitumia 'kupitisha' bajeti ni wendawazimu. Nchi ina matatizo lukuki, lkn hayafanyiwi kazi kwa kisingizio cha ufinyu wa bajeti.

Watanzania, KAZI NI KWETU!
 
Mwanakijiji umeonesha Umbumbu mkubwa kwa kutofahamu kazi za Mbunge! Katiba ya JM wa Tanzania haijaonesha kazi ya Mbunge wa Upinzani ni ipi na ya Chama kinachotawala ni ipi!? Kazi ya Bunge na Mbunge ni kuibana serikali!
 
Kwa maoni yangu, ni wazi kuwa Pinda alikurupuka, na sasa baada ya uchunguzi na kusafishwa kwa Jairo hahitaji kujiuzulu. Kwa nini ajiuzulu? Kwani amekosea nini? Serikali imefuata 'natural justice' na kuamua kumsafisha Jairo. Kama Jairo angefukuzwa kwa kauli ya Pinda, si angekuwa na madai mahakamani? Kuna uwezekano mkubwa Pinda alikurupuka 'in the heat of the moment' na kusema lake. Nadhani hilo ni somo tosha.
 
Nitakuwa wa kwanza kushangaa kama Pinda hata jiuzulu kutetea na kulinda hadhi yake
<br />
<br />
pinda bendera kaka. Yeye ni kama sikirini afu mtu mwengne ana remote. HAKUNA ATAKAE JIUZURU WALA KUWAJIBIKA NA JAIRO MZIGONI KAMA KAWA, hii ndo tz
 
Back
Top Bottom