Wabunge wa CCM hawana nia njema na wananchi

MLO

Senior Member
Apr 2, 2012
197
84
Ukiangalia Bunge linaloendelea Dodoma utadhani kuna jipya kwa chama tawala.Wanatumia hira hiyo ya kuongea na kushutumiana ili kupoza joto la Arumeru linaloongezeka kila kukicha.Nawakumbusha walikana na kuita uchochezi baada yakuibuliwa kashfa ya EPA walipobanwa kisawasa walijiunga na kukubali kuwepo kwa ufisadi huo.Tuliwaona kina Ole sendeka,Kilango na wengine wakijiita wapapanaji.Baada ya dhoruba hilo kupoa hakuna fisadi wala msafi wote bega kwa bega kusafishana.
Naomba wote wenye nia njema na Tanzania warudishe kadi za chama chao au waungane na kupeleka hoja ya kutokuwa na imani na serikali ya chama cha Mapinduzi.
Vinginevyo tunawaona Chui ndani ya vazi la Mwanakondoo Tuna akili timamu waache ulaghai.
Mfano kwa sasa Kilango na Ole sendeka hawezi kusimama tena na kuyasema waliyoyasema 2008 kwenye kashifa ya EPA.
 
Back
Top Bottom