Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
1 )"Kwa hiyo tumesema inatosha, hapo tulipofikia tusiendelee mbele. Wanaoropoka hovyo ni walevi ....! - Chiligati
Chiligati ni kimbelembele na anajiona yeye ni mwenye kupendeza ndani ya serikali hii kumbe hajui kama amekalia kuti kavu,Cheo alichonacho kinamfanya ajione yeye ndio mwenye kauli ya mwisho ,mambo ya kuwaita watu walevi yalitokea kwa kuitwa viongozi kuwa ni walevi wa gongo sasa yeye anendeleza kuwaita wabunge watetezi wanaoihoji na kuijadili pamoja na kufikisha ujumbe kwa wananchi kuwa ni walevi ,hili wabunge wapo na watamueleza vilivyo ili ijulikane nani mlevi
2) Njia sahihi, alisema, ni malalamiko kushughulikiwa kulingana na taratibu za chama na siyo kuyasema majukwaani ili kuufurahisha umma - Dk Mahanga, ambaye ni Naibu Waziri wa Kazi.
Naibu huyu hajui analolisema maana mafisadi hawazungumziwi katika ngazi ya Chama bali wanazungumzwa katika ngazi ya Taifa hivyo anashindwa kutofautisha Chama na Bunge,anasema zitumike taratibu za chama katika mambo ya kiTaifa, pia amezidi kujidharaulisha pale aliposema wanafurahishwa umma ,yaani wananchi kufahamu na kuelezwa mambo ya ufisadi haihusu na wananchi hao hawana uwezo wa kufanya lolote lile,amesahau kuwa wananchi ndio wanaowachagua wabunge ,ila hapa ifahamike tu wabunge wengi wa CCM hupitishwa kwa njia za panya kama alivyopitishwa yeye Mahanga.
Mahanga anashindwa kufahamu kuwa mambo ya ufisadi sio ya kuzungumzwa katika vikao na kamati za siri bali ni mambo ambayo yanahitaji kila mwananchi ayajue na inapotokea mtu kufukuzwa wananchi wasione ameonewa, mficha uchi hazai ndivyo wahenga wanavyosema kwa maana hiyo kama tukiendelea kuficha na kuzungumza ndani ya vikao ya siri hakuna maendeleo yatakayopatikana..
3) Kuna haja ya wabunge kudhibitiwa kwa sababu wengine wamefikia hatua hata ya kuwakejeli viongozi wa serikali badala ya kutumia hoja katika kujenga hoja.- Shelukindo
Mwengine huyu anasema kuwajadili viongozi kwenye bunge ni kuwakejeli sasa atueleze ni wapi viongozi wajadiliwe ikiwa mienendo yao inaenda kinyume na utaratibu wa uongozi kwa maana Mkapa alienda kinyume na taratibu za kiutawala na sheria za nchi,wapi akajadiliwe ?
Majibu waliyoyapata CCM baada ya kikao chao cha siri au NEC.
Spika Samuel Sitta ambaye alikuwa kwenye wakati mgumu wakati wajumbe wapatao 22, walipopendekeza atimuliwe kwenye chama, bado ana msimamo wa kuendeleza vita ya ufisadi.
Wabunge ambao majina yao kapuni.
"Kama kuna watu serikalini au wabunge wanaofurahia msimamo huo wa Nec, wajue wanajidanganya kwa sababu hauna nguvu yoyote ya kudhibiti uhuru wa bunge,"Bunge lina nguvu ya kujadili mambo ambayo si spika wala Nec wanaoweza kuizuia."
"Kama suala ni uhuru ambao umefanya wabunge kuvuka mipaka na kila mmoja kuamua kufanya lolote bungeni, basi Nec isingesema na kuacha tu hewani. Ingeorodhesha kanuni zilizovunjwa na wananchi wakaelewa,"
Tunawataka wananchi kuondoa shaka kuhusu uamuzi huo wa Nec akisema kuwa wao kama wabunge wako imara na wataendelea kutetea maslahi ya wananchi bila kuogopa. - Christopher Ole Sendeka mbunge CCM.
"Sidhani kama kuna mtu amefungwa mdomo na Nec.
Mdomo upo palepale na watu wataendelea kuongea. Nec haiwezi kumfunga mdomo spika wala wabunge
"Tumeisikia Nec, lakini wavumilie tu kwani lazima mabadiliko yatokee. Wananchi ndio wenye chama na ndio wanaotaka wabunge wao wapambane na uovu na ufisadi,"Ni lazima watuhumiwa wa rushwa wafikishwe mahakaman.-Mbunge wa Vunjo (CCM), Aloyce Kimaro
Kazi kwenu CCM mnavuna mlichopanda watu hawarudi nyuma tena kuogopa makeke na vishindo vyenu.
Chiligati ni kimbelembele na anajiona yeye ni mwenye kupendeza ndani ya serikali hii kumbe hajui kama amekalia kuti kavu,Cheo alichonacho kinamfanya ajione yeye ndio mwenye kauli ya mwisho ,mambo ya kuwaita watu walevi yalitokea kwa kuitwa viongozi kuwa ni walevi wa gongo sasa yeye anendeleza kuwaita wabunge watetezi wanaoihoji na kuijadili pamoja na kufikisha ujumbe kwa wananchi kuwa ni walevi ,hili wabunge wapo na watamueleza vilivyo ili ijulikane nani mlevi
2) Njia sahihi, alisema, ni malalamiko kushughulikiwa kulingana na taratibu za chama na siyo kuyasema majukwaani ili kuufurahisha umma - Dk Mahanga, ambaye ni Naibu Waziri wa Kazi.
Naibu huyu hajui analolisema maana mafisadi hawazungumziwi katika ngazi ya Chama bali wanazungumzwa katika ngazi ya Taifa hivyo anashindwa kutofautisha Chama na Bunge,anasema zitumike taratibu za chama katika mambo ya kiTaifa, pia amezidi kujidharaulisha pale aliposema wanafurahishwa umma ,yaani wananchi kufahamu na kuelezwa mambo ya ufisadi haihusu na wananchi hao hawana uwezo wa kufanya lolote lile,amesahau kuwa wananchi ndio wanaowachagua wabunge ,ila hapa ifahamike tu wabunge wengi wa CCM hupitishwa kwa njia za panya kama alivyopitishwa yeye Mahanga.
Mahanga anashindwa kufahamu kuwa mambo ya ufisadi sio ya kuzungumzwa katika vikao na kamati za siri bali ni mambo ambayo yanahitaji kila mwananchi ayajue na inapotokea mtu kufukuzwa wananchi wasione ameonewa, mficha uchi hazai ndivyo wahenga wanavyosema kwa maana hiyo kama tukiendelea kuficha na kuzungumza ndani ya vikao ya siri hakuna maendeleo yatakayopatikana..
3) Kuna haja ya wabunge kudhibitiwa kwa sababu wengine wamefikia hatua hata ya kuwakejeli viongozi wa serikali badala ya kutumia hoja katika kujenga hoja.- Shelukindo
Mwengine huyu anasema kuwajadili viongozi kwenye bunge ni kuwakejeli sasa atueleze ni wapi viongozi wajadiliwe ikiwa mienendo yao inaenda kinyume na utaratibu wa uongozi kwa maana Mkapa alienda kinyume na taratibu za kiutawala na sheria za nchi,wapi akajadiliwe ?
Majibu waliyoyapata CCM baada ya kikao chao cha siri au NEC.
Spika Samuel Sitta ambaye alikuwa kwenye wakati mgumu wakati wajumbe wapatao 22, walipopendekeza atimuliwe kwenye chama, bado ana msimamo wa kuendeleza vita ya ufisadi.
Wabunge ambao majina yao kapuni.
"Kama kuna watu serikalini au wabunge wanaofurahia msimamo huo wa Nec, wajue wanajidanganya kwa sababu hauna nguvu yoyote ya kudhibiti uhuru wa bunge,"Bunge lina nguvu ya kujadili mambo ambayo si spika wala Nec wanaoweza kuizuia."
"Kama suala ni uhuru ambao umefanya wabunge kuvuka mipaka na kila mmoja kuamua kufanya lolote bungeni, basi Nec isingesema na kuacha tu hewani. Ingeorodhesha kanuni zilizovunjwa na wananchi wakaelewa,"
Tunawataka wananchi kuondoa shaka kuhusu uamuzi huo wa Nec akisema kuwa wao kama wabunge wako imara na wataendelea kutetea maslahi ya wananchi bila kuogopa. - Christopher Ole Sendeka mbunge CCM.
"Sidhani kama kuna mtu amefungwa mdomo na Nec.
Mdomo upo palepale na watu wataendelea kuongea. Nec haiwezi kumfunga mdomo spika wala wabunge
"Tumeisikia Nec, lakini wavumilie tu kwani lazima mabadiliko yatokee. Wananchi ndio wenye chama na ndio wanaotaka wabunge wao wapambane na uovu na ufisadi,"Ni lazima watuhumiwa wa rushwa wafikishwe mahakaman.-Mbunge wa Vunjo (CCM), Aloyce Kimaro
Kazi kwenu CCM mnavuna mlichopanda watu hawarudi nyuma tena kuogopa makeke na vishindo vyenu.