nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
JUMANNE, JULAI 31, 2012 06:25 NA MAREGESI PAUL, DODOMA
*Yadaiwa mafisadi wanajipanga kukata umeme
*Washtukia walinzi wa makampuni binafsi
WABUNGE wamechachamaa. Kuanzia sasa wanataka mitambo ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na vyanzo vyote vya umeme, vilindwe na askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) pamoja na askari polisi.
Mapendekezo hayo, yalitolewa bungeni jana na Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugora (CCM) na Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia (NCCR-Mageuzi), baada ya kuwapo taarifa kwamba, kuna watu wanajipanga kuifanyia hujuma mitambo hiyo ili umeme usipatikane.
Lugora na Mbatia, walitoa mapendekezo hayo walipoomba mwongozo wa Spika, kwa nyakati tofauti kuhusu usalama wa shirika hilo la umeme.
Aliyekuwa wa kwanza kuomba mwongozo wa Spika ni Lugora, ambaye alisema kuna taarifa za mafisadi kuandaa mikakati ya kuihujumu TANESCO kama njia ya kukwamisha jitihada za Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na manaibu wake, Slyvester Masele na George Simbachawene.
"Mheshimiwa Naibu Spika, nasimama hapa kwa kutumia Kanuni ya 68 (7) ambayo inaruhusu mbunge kusimama wakati wowote wakati ambao hakuna mbunge mwingine anayezungumza.
"Mheshimiwa Naibu Spika, juzi Jumamosi wakati Waziri wa Nishati na Madini akihitimisha mjadala wa hotuba ya bajeti yake, alilihakikishia Bunge na Watanzania wote, kwamba mgawo wa umeme ambao tumekuwa tukikumbana nao ulikuwa ni wa kuumba.
"Waziri alituhakikishia kuwa, kulingana na hatua alizochukua, kuanzia sasa mgao wa umeme utakuwa ni wa historia.
"Lakini kwa kuwa suala la mgawo wa umeme ni zito na kwa kuwa uamuzi wa Spika wa kuvunja Kamati ya Nishati na Madini siyo suluhisho na kwa kuwa kuwasimamisha watendaji wa TANESCO pia siyo suluhisho na pia uamuzi aliosema Waziri atavunja bodi ya TANESCO siyo suluhisho.
"Sasa ninazo taarifa kwamba, baada ya waziri na manaibu wake kuvunja mirija ya ulaji TANESCO, sasa mafisadi wanajipanga kufanya hujuma nje ya Bunge kwenye gridi ya taifa na mitambo yote ya TANESCO ili umeme wa uhakika usipatikane kama waziri na manaibu wake walivyoahidi.
"Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mitambo ya TANESCO inalindwa na walinzi wa makampuni ya kawaida wenye filimbi na virungu na kwa kuwa nchi nyingine duniani wanajeshi na polisi ndio wanaolinda mitambo kama hiyo, kwa nini sasa na sisi tusiimarishe ulinzi kwa kuwatumia askari wa majeshi hayo?
"Mheshimiwa Naibu Spika, naomba mwongozo wako katika jambo hili kwa sababu baadhi ya vyanzo vingine vya umeme viko porini," alisema Lugora.
Mbunge huyo, alipomaliza zamu yake, ilikuja zamu ya Mbatia ambaye aliunga mkono hoja ya mbunge mwenzake huyo, akitaka Bunge, liiagize Serikali ipeleke askari hao katika mitambo yote ya TANESCO.
"Mheshimiwa Naibu Spika na mimi natumia Kanuni ya 68 (7) aliyotumia Mheshimiwa Mbunge wa Mwibara.
"Mheshimiwa Naibu Spika, siku zote kinga ni bora kuliko tiba na tishio hili linafanya hali iwe tete kwa sababu ufisadi ni mfumo na kuufumua kwa kauli siyo suala jepesi.
"Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa JWTZ wapo na moja ya kazi yao ni kuwalinda wananchi, tusichelewe kuiagiza Serikali ianze kuwatumia wanajeshi na JKT.
"Uamuzi huu, tuutoe sasa tusichelewe tena na pia Waziri wa Nishati na manaibu wake nao wapewe ulinzi, Mheshimiwa Spika naomba mwongozo wako tusingoje kesho," alisema Mbatia.
Akizungumzia miongozo hiyo, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, alisema ataitolea ufafanuzi jioni (jana), baada ya kupata ushauri zaidi.
*Yadaiwa mafisadi wanajipanga kukata umeme
*Washtukia walinzi wa makampuni binafsi
WABUNGE wamechachamaa. Kuanzia sasa wanataka mitambo ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na vyanzo vyote vya umeme, vilindwe na askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) pamoja na askari polisi.
Mapendekezo hayo, yalitolewa bungeni jana na Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugora (CCM) na Mbunge wa Kuteuliwa, James Mbatia (NCCR-Mageuzi), baada ya kuwapo taarifa kwamba, kuna watu wanajipanga kuifanyia hujuma mitambo hiyo ili umeme usipatikane.
Lugora na Mbatia, walitoa mapendekezo hayo walipoomba mwongozo wa Spika, kwa nyakati tofauti kuhusu usalama wa shirika hilo la umeme.
Aliyekuwa wa kwanza kuomba mwongozo wa Spika ni Lugora, ambaye alisema kuna taarifa za mafisadi kuandaa mikakati ya kuihujumu TANESCO kama njia ya kukwamisha jitihada za Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na manaibu wake, Slyvester Masele na George Simbachawene.
"Mheshimiwa Naibu Spika, nasimama hapa kwa kutumia Kanuni ya 68 (7) ambayo inaruhusu mbunge kusimama wakati wowote wakati ambao hakuna mbunge mwingine anayezungumza.
"Mheshimiwa Naibu Spika, juzi Jumamosi wakati Waziri wa Nishati na Madini akihitimisha mjadala wa hotuba ya bajeti yake, alilihakikishia Bunge na Watanzania wote, kwamba mgawo wa umeme ambao tumekuwa tukikumbana nao ulikuwa ni wa kuumba.
"Waziri alituhakikishia kuwa, kulingana na hatua alizochukua, kuanzia sasa mgao wa umeme utakuwa ni wa historia.
"Lakini kwa kuwa suala la mgawo wa umeme ni zito na kwa kuwa uamuzi wa Spika wa kuvunja Kamati ya Nishati na Madini siyo suluhisho na kwa kuwa kuwasimamisha watendaji wa TANESCO pia siyo suluhisho na pia uamuzi aliosema Waziri atavunja bodi ya TANESCO siyo suluhisho.
"Sasa ninazo taarifa kwamba, baada ya waziri na manaibu wake kuvunja mirija ya ulaji TANESCO, sasa mafisadi wanajipanga kufanya hujuma nje ya Bunge kwenye gridi ya taifa na mitambo yote ya TANESCO ili umeme wa uhakika usipatikane kama waziri na manaibu wake walivyoahidi.
"Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mitambo ya TANESCO inalindwa na walinzi wa makampuni ya kawaida wenye filimbi na virungu na kwa kuwa nchi nyingine duniani wanajeshi na polisi ndio wanaolinda mitambo kama hiyo, kwa nini sasa na sisi tusiimarishe ulinzi kwa kuwatumia askari wa majeshi hayo?
"Mheshimiwa Naibu Spika, naomba mwongozo wako katika jambo hili kwa sababu baadhi ya vyanzo vingine vya umeme viko porini," alisema Lugora.
Mbunge huyo, alipomaliza zamu yake, ilikuja zamu ya Mbatia ambaye aliunga mkono hoja ya mbunge mwenzake huyo, akitaka Bunge, liiagize Serikali ipeleke askari hao katika mitambo yote ya TANESCO.
"Mheshimiwa Naibu Spika na mimi natumia Kanuni ya 68 (7) aliyotumia Mheshimiwa Mbunge wa Mwibara.
"Mheshimiwa Naibu Spika, siku zote kinga ni bora kuliko tiba na tishio hili linafanya hali iwe tete kwa sababu ufisadi ni mfumo na kuufumua kwa kauli siyo suala jepesi.
"Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa JWTZ wapo na moja ya kazi yao ni kuwalinda wananchi, tusichelewe kuiagiza Serikali ianze kuwatumia wanajeshi na JKT.
"Uamuzi huu, tuutoe sasa tusichelewe tena na pia Waziri wa Nishati na manaibu wake nao wapewe ulinzi, Mheshimiwa Spika naomba mwongozo wako tusingoje kesho," alisema Mbatia.
Akizungumzia miongozo hiyo, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, alisema ataitolea ufafanuzi jioni (jana), baada ya kupata ushauri zaidi.