Wabunge chadema makomandoo?

SILENT ACtOR

JF-Expert Member
Apr 9, 2011
627
181
Hawa jamaa kweli makamanda kwa maana halisi. Leo ktk mkutano wa CHADEMA tawi la UDOM mbunge Joseph Silinde alizungusha macho kama kinyonga ktk umati wa watu wakati akiendelea na hotuba akamgundua askari kanzu mmoja. Kisha akamuumbua kwa kusema, "mliotumwa kuchukua habari mkalipoti vema, maake namwona rafiki yangu mmoja aliyewahi kunikamata nikiwa UDSM yuko hapa, hebu njoo hapa mbele!" Lool! Yule jamaa jasho lilimtoka. Akamfanyia ishara ya mkono Silinde kama kuomba msamaha na mbunge kwa kujua yapi yangefuatia kutoka kwa umati akaamua kumhifadhi na kuendelea na hotuba. Haya tena mnaotumwa kwenye vikao vya wenzenu muwe makini, siku hizi kila mtu anazijua mbinu bana!.:israel:


--A country needs independence; a nation needs liberation; the people need revolution--
Tundu Lissu.
 
Hiyo Quatation Hayati Prof.Chachage aliwahi kusema Pia Waafrika tuliomba Ukombozi tukapewa Uhuru kwahiyo Ukombozi wa kweli haupatikani kwakupewa "Ukombozi" unatafutwa nakupiganiwa kwa nguvu zote.Shime Watanzania tuutafute huu Ukombozi coz kila mtu anaona Rasilimali zetu zinavyopokonywa kwa ukoloni Mambo leo wanaouita Uwekezaji saiv wanaelekea kuwapa na Ardhi yote bure kwa miaka kumi imepitishwa bungeni hii bila hata kuwalipisha kodi.Jamani Nchi inamalizwa hii tuamke.
 
Back
Top Bottom