Wabunge CCM kuunda chama?

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
headline_bullet.jpg
Wako mbioni kujiengua chama hicho
headline_bullet.jpg
Baadhi wakiri uwezekano ni mkubwa
headline_bullet.jpg
Chiligati: ``Sina taarifa hizo na mimi sio mmoja wa wabunge hao."

Na Restuta James 10th January 2010

Baadhi ya wabunge ndani ya CCM wamedaiwa kujipanga kwa lengo la kuunda chama chao katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.

Habari za uhakika ambazo Nipashe Jumapili imezipata, zinaeleza kuwa wabunge hao wako mbioni kujiengua kwenye chama hicho, licha ya juhudi za Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC) kuunda Kamati ya kuchunguza mahusiano ya wabunge na serikali ili kunusuru mpasuko ndani ya chama .

Kamati hiyo ambayo inaongozwa na Rais mstaafu, alhaj Ali Hassan Mwinyi, ilipewa jukumu na NEC kutafuta dawa ya mpasuko uliopo miongoni mwa wabunge hao jambo ambalo linahatarisha mshikamano miongoni mwa wanachama wa chama hicho tawala.

Taarifa hizo zinaeleza kuwa bunge na wanachama hao wameazimia kuunda chama hicho kabla ya uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu, iwapo CCM haitawawajibisha mafisadi wanaoitafuna nchi.

Chanzo cha uhakika kimeliambia gazeti la Nipashe Jumapili kuwa maamuzi mazito ambayo chama kinapaswa kuyachukua ni pamoja na kuwawajibisha viongozi na wanachama waliohusika kwenye ufisadi wa Richmond, Kiwira, Benki Kuu ya Tanzania na katika ufisadi mwingine ulioliingizia taifa hasara.

Chanzo hicho kimeeleza kuwa sababu kubwa iliyopelekea wanachama wameguke na kuunda chama kipya ni kutokana na CCM kutosimamia kikamilifu Katiba yake jambo linalopelekea kumomonyoka kwa maadili ndani ya chama na Serikali.

"Kwa sasa kutokana na hali ilivyo ndani ya CCM uwezekano wa kumeguka ni mkubwa lakini itategemea sana hatua zitakazochukuliwa na viongozi kutokana na taarifa ya kamati ya Mwinyi na hatua zitakazochukuliwa dhidi ya ufisadi unaokithiri nchini," alisema mbunge mmoja wa CCM.

Mbunge mwingine wa CCM alisema, "kupasuka kwa CCM na kuundwa chama kingine kutawezesha kuwepo upinzani utakaoleta faida kwa wananchi kwa kuwawezesha kuchagua Serikali mbadala kuliko hali ilivyo sasa."

Alisema ili kuepuka kuundwa kwa chama hicho kipya, uongozi wa juu wa CCM unapaswa kufanya vikao na kuchukua maamuzi magumu.

"Mfano, wale waliotuhumiwa kwa ufisadi na kuchukuliwa hatua kwenye Serikali ya CCM kama Waziri Mkuu aliyejiuzulu kutokana na kashfa ya Richmond, Edward Lowassa, Rostam Aziz, Andrew Chenge na Nazir Karamagi, inabidi wawajibishwe," kilisema chanzo hicho.

Chanzo hicho kilinukuu Katiba ya CCM toleo la 2007 sehemu ya kwanza kifungo 3, 4, 7 na 14 inayokemea ufisadi nchini.

Alipohojiwa na gazeti hili kuhusu suala hilo, Mbunge wa Kishapu (CCM), Fred Mpendazoe alikiri kuwepo kwa mpasuko ndani ya chama hicho na kutabiri uwezekano wa suala hilo kutokea.

Alisema hali ya chama si shwari kuanzia ngazi ya juu hadi shina kutokana na kushamiri kwa rushwa katika chaguzi nyingi, jambo alilosema linazidi kukibomoa chama.

"Na hali hii itaendelea kuleta mpasuko ndani ya chama hasa baada ya kura za maoni, na hivyo upo uwezekano chama kikadhoofika...lakini viongozi wanapokuwa na msuguano maana yake chama hicho hakiwezi kutoa uongozi uliotarajiwa," alisema Mpendazoe.

Alisema mpasuko uliopo ndani ya CCM unatokana na namna chama kinavyoendeshwa na kwamba wapo viongozi wanaotaka chama hicho kiendeshwe kwa mujibu wa Katiba ya chama na wengine wanataka kiendeshwe kwa matakwa ya wachache.

"Upo uwezekano kwamba kuwaondoa wanaotuhumiwa na ufisadi ndani ya chama itashindikana, basi wale wanachama wanaopendelea hatua zichukuliwe watafakari kwa makini sana pendekezo la mwasisi wa CCM Hayati Mwalimu Julius Nyerere kwamba upinzani wa kweli wa CCM utatoka ndani ya CCM, hatua hii itakuwa yenye tija kwa taifa," alisema na kuongeza kuwa "Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa 'watu wengine wakiamua kutoka ndani ya CCM tutafanya makosa tukiwaona ni wasaliti, kwa sasa CCM iking’ang’aninia umoja wa bandia itaununua umoja huo kwa kupoteza itikadi yake na wananchi kupoteza imani kwa CCM”.

Mpendazoe aliwataka wananchi kuepuka tabiri na kauli zinazotolewa na watu mbalimbali na kuwasihi wamtegemee Mungu ili aweze kuwapatia viongozi watakaojali maslahi ya nchi.

Alipohojiwa na gazeti hili kuhusu taarifa hizo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NEC, John Chiligati, alijibu kwa ufupi "sina taarifa hizo na mimi sio mmoja wa wabunge hao."

Chiligati ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, aliahidi kufuatilia taarifa hizo ndipo chama kiyatolee tamko.

CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
 
possible,wamekosa mlezi wa kumpelekea matatizo yao......
 
This is the moment anxiously awaited by any rational Tanzanian!

"Upinzani wa kweli utatoka ndani ya sisiemu"!

Na juzijuzi wametoa kali kwa kumtumia sheikh wao kwamba atakayejaribu kugombea kwa kumpinga JK atakufa!

Kwahiyo sasa ni muda muafaka kusambaratika ili kuqualify kupingana na JK KWA YULE ATAKAYETAKA!
 
Hakuna hata suala la 'kumekucha' hapo. Angalau wangetaja jina moja. Zaidi ya hivyo ni Bla bla za magazeti kuuza magazeti yao.
 
Alipohojiwa na gazeti hili kuhusu taarifa hizo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa NEC, John Chiligati, alijibu kwa ufupi "sina taarifa hizo na mimi sio mmoja wa wabunge hao."

Chiligati ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, aliahidi kufuatilia taarifa hizo ndipo chama kiyatolee tamko.

Kwa mtu mwenye akili ukitafakari kauli ya Chiligati 'ila mimi simo' jua kuna jambo. Chiligati ninayemjua mimi kwa jambo kama hili angesema hayo ni mambo ya kipuuzi lakini sasa anaonekana kuwa mpole zaidi.

Anyway ikitokea ni ahueni kwa wa Tanzania naona Names of shame na mafisadi slogan inazidi kupasua miamba sera ya ufisadi ya Chadema ndiyo itakayowamaliza CCM wapende wasipende big up Chadema.
 
Sasa si wajitokeze hadharani, tunarudi pale pale hawatambui kwamba hiyo ni haki yao kikatiba. Na wanahisi kufanya hivyo ni uhaini
 
It is afalse alarm,very very very far fron reality!

Nami msafi katika Wabunge wa CCM kama kampeni yenyewe iliendeshwa na kina Maranda na Rostam? Kilicho cha wazi ni kuwa hawa watu wamesaliti Chama chao na wanajuwa kuwa adhabu inakuja dhidi yao. Wanajaribu kuitisha CCM lakini hali halisi ni kuwa mawekamatwa kooni.

Kujiunga na Chama chengine kuna maana kupoteza ubunge na kwa uroho wao nani yuko tayari kupoteza lile burungutu la mwishi wa kipindi August 2010?


Hawa si wengine bali ni wale waliokwishajuwa kuwa hawana nafasi tena CCM na hivyo kupandikiza propaganda dhidi ya CCM.

Kwangu mimi sioni ground hata moja ya kuwezekana kwa hili.
 
EEH MUNGU bariki jio wa chama kipya, bariki vurugu ndani ya CCM, WAFANYE WASIELEWANE KUELEKEA uchaguzi mkuu, naomba CCM iwafukuze uanachama wapigaji wote, iwafukuze Uanacham,a kina Mengi, Malecela ,Idd Simba, Warioba, quares, na wengine, eeh Mungu baba mfanye Kikwete apatane na Lowassa tena...ili CCM wengine wamkatae kwa sauti moja, nikiomba hayo nikataraji shehe Yahya aaibike yeye nA mapepo yake.....AAMEN.
 
I pray for that to happen, lets hope for the best , inawezekana ila ngumu sana kuamini.
 
It is afalse alarm,very very very far fron reality!

Nami msafi katika Wabunge wa CCM kama kampeni yenyewe iliendeshwa na kina Maranda na Rostam? Kilicho cha wazi ni kuwa hawa watu wamesaliti Chama chao na wanajuwa kuwa adhabu inakuja dhidi yao. Wanajaribu kuitisha CCM lakini hali halisi ni kuwa mawekamatwa kooni.
Kujiunga na Chama chengine kuna maana kupoteza ubunge na kwa uroho wao nani yuko tayari kupoteza lile burungutu la mwishi wa kipindi August 2010?
Hawa si wengine bali ni wale waliokwishajuwa kuwa hawana nafasi tena CCM na hivyo kupandikiza propaganda dhidi ya CCM.
Kwangu mimi sioni ground hata moja ya kuwezekana kwa hili.

wabunge gani hawana nafasi ndani ya CCM, na lini wataenguliwa ili tujue CCM wasafi

Mkuu unatumiwa nini hapa?? JK huyuhuyu unasema kuna wana CCM wamekamatwa kooni, wakati kuanzia JK waliingia madarakani kwa rushwa?? wadanganye haohao!
 
Siku CCM itakapo sambaratika ndio siku ya ukombozi wetu zidi ya zuluma,wizi uonevu,utapeli,zihaki,unyanyasaji,ujinga,umasikini na mengine mengi.

Mimi nitatangaza kama siku ya UHURU na kuitaja Tanzania mpya,nitapiga parapanda siku iyo CCM itakapo vunjika wana JF tuweke kwenye maombi ya kila siku,ipo siku tutashinda na tutaona Tanzania mpya
.
 
Naomba siku hiyo ifike haraka iwe hata leo, itakuwa ni ukombozi kwetu kama mtoa hoja hapo juu kasema kwake itakuwa kama siku ya Uhuru. Mimi mchango wangu nitaanzisha thread tupendekeze jina gani la hicho chama kiitwe, let say;
CCM B? CCM Asili? au ....... you name it.
 
Naomba siku hiyo ifike haraka iwe hata leo, itakuwa ni ukombozi kwetu kama mtoa hoja hapo juu kasema kwake itakuwa kama siku ya Uhuru. Mimi mchango wangu nitaanzisha thread tupendekeze jina gani la hicho chama kiitwe, let say;
CCM B? CCM Asili? au ....... you name it.

CCMM-chama cha mapinduzi mapya!
 
Strategically this is a false start. Some of us know that this thing is contemplated and the quoted guy is the secretary of the group. Him being quoted in the article is like telling the enemy 'we are here'. Coming out from Nipashe tells it all. You get my point?

You heard Kulikoni being suspended? For a story of November? A military story? Proving that Mengi is not a patriot and ensuring that the Army and Intelligence detest him. You know you have to have the army by your side to take political power?

Two things

  1. Mengi anajipendekeza kwa kutoa habari ile ili CCM wamhurumie
  2. Mengi na kundi lake sasa wameamua kweli kutoka CCM. Kwa kuwa hawana mikakati na kuanza hovyo kama hivi, watasagwa na kwisha kabla hawajaanza. Ndembwela Ngunangwa once wrote .... Bingwa wa mikakati iliyoshindwa kabla ya kuanza......
 
Mimi sidhani kama hilo ninawezekana maana naona kama ni politics agenda zao katika kipindi hiki kidogo cha uchaguzi kuna vyama kibao basi waingine huko kwanza hakuna jipya juu ya mambo haya
 
- Hapa ndipo CCM inapopiga bao kwenye uchaguzi na hizi propaganda zao za kampeni sounds like Ruhinda, sasa tayari ameshashika tena ile kazi yake ya kampeni na Mtandao!

Respect.


FMEs!
 
Lini watajitoa? lini wataandikisha chama cha Siasa? Lini watatangaza Mgombea wao wa Urais! Watu huwa wanapima vitu kwa kuangalia dimension tatu tu Urefu ( length), Upana (width) na Kimo ( height) wanasahau parameter moja ya dimension ambayo ni muda! Wasijejikuta wakati wanatangaza kuunda chama chao muda wa kuchukua fomu umeisha
 
This is the moment anxiously awaited by any rational Tanzanian!

"Upinzani wa kweli utatoka ndani ya sisiemu"!

Na juzijuzi wametoa kali kwa kumtumia sheikh wao kwamba atakayejaribu kugombea kwa kumpinga JK atakufa!

Kwahiyo sasa ni muda muafaka kusambaratika ili kuqualify kupingana na JK KWA YULE ATAKAYETAKA!


Unachosema ni kweli kabisa PJ, lakini hawa Wabunge wana nia ya kweli kuanzisha chama kipya cha siasa au wanatingisha kibiriti tu? Kama wana nia ya kweli basi hizo ni habari nzuri sana kwa Mtanzania yeyote ambaye anapenda maendeleo ya nchi yetu maana upinzani uliopo sasa hivi kwa maoni yangu umeshindwa kukabiliana na CCM pamoja na kuwa imegubikwa na tuhuma chungu nzima na mifarakano mikubwa ndani ya chama hicho.

Ikiwa imebaki miezi 10 kabla ya uchaguzi, CHADEMA wana misukusuko mikubwa ndani ya chama hicho nadhani hili linasababishwa zaidi na ubinafsi. Mrema wa TPL amekuwa ni kitengo cha CCM kumpigia debe Kikwete ili achaguliwe tena 2010. CUF ndiyo hao bado wanapigia debe muafaka ili kuwe na Serikali ya mseto 2010 kule Zenj, sijui kama wana mikakati yoyote ya Bara. NCCR hawa hata sijui kama chama chao kina uhai. Tusubiri tuone kama Wabunge hao wataunda kweli chama chao au ni kelele tu.
 
Back
Top Bottom