Eric Cartman
JF-Expert Member
- May 21, 2009
- 11,967
- 11,212
Alipoingia 2005 watu wote walikuwa nyuma yake wakijua tume zote alizoziunda na safari zake alizopita kwenye wizara zote,na warsha zote alizofanya kwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi,walijua alikuwa anasafisha njia ya kuifanya nchi itawarike
sasa hivi hata akilialia na mnagani Jakaya hana pa kukwepea ni dhaifu hawezi kuendesha nchi,kwa sababu yeye mwenyewe aliingia kwa kutumia mtandao,alikuwemo serikali iliyopita kwa hiyo maamuzi mengi ya baraza la mawaziri wakati wa mkapa aliyafahamu na alishiriki pia kupindisha baadhi ya sheria ili wao wanufaike kama viongozi
Hebu tujiulize kitu gani kinamfanya sasa hivi mambo ameyaacha holela hakuna utawala wa sheria ,hakuna anayemuogopa wala kumuheshimu kiongozi wa nchi anakataza hiki yue anafanya hiki ,mambo yanazidi kubomoka kuliko hata yalivyokuwa kwa Mkapa.
Miaka minne serikalini hajatafuta mbinu za kutukwamua kila siku vilio tuu kutoka kwa wananchi kutokana na jinsi mali zake zinavyoporwa na wahuni,wazungu,wahindi na waarabu,ametukatisha tamaa sana tulimwamini mno sasa anatuonyesha kwamba ni muhimu kuwe na mabadiliko makubwa kuanzia serikali za mitaa vinginevyo wanataka kutupeleka kusikofaa, kuzagaa kwa vijana bila kazi,njaa,hasira za watu maskini, ukosefu wa mapato sawia ni vitu vinavyoleta chuki,yeye ameshindwa hata kudhibiti mfumuko wa bei,watu wanateseka sana,maradhi,maisha tuu ni magumu mno kwao
Mimi naona apumzike tuu amwachie mwingine ampokee kijiti
kwanini tuandikie mate wakati wino upo mi naomba kuwe na ukweli wa namna moja katika hii post tuone hata dili nao vipi hao mawaziri wake? ni muoga ndio maana wanamchezea tu.