Wanaharakati wapinga kauli za wabunge kuhusu JK
Rais Jakaya Kikwete
Rais Jakaya Kikwete
Wanaharakati wa Haki za Binadamu, Elimu na Mazingira (Thren), wamepinga baadhi ya kauli zilizotolewa na wabunge kwa kumtaka Rais Jakaya Kikwete ajiuzulu kwa kile walichoeleza kuwa ni kushindwa kwa Serikali kutekeleza maazimio ya Bunge.
Pingamizi hilo lilitolewa jana na wanamazingira 217 kutoka mikoa ya Dodoma, Arusha, Mwanza, Shinyanga, Mara, Kigoma, Kilimanjaro, Unguja, Mbeya, Rukwa, Morogoro, Ruvuma, Kagera, Pwani, Dar es Salaam, Lindi, Tanga, Mtwara na Tabora ambao wamesema kauli hizo zinalengo la kuvuruga amani ya nchi.
Wanaharakati hao wamewataja wabunge 46 na mawaziri 13 ambao walisema wamekuwa wakizunguka maeneo mbalimbali nchini kuwahamasisha wananchi waunge mkono ajenda yao ya kumtaka Rais ajiuzulu.
Mkurugenzi Mkuu wa taasisi ya kuhifadhi misitu na mazingira (Mreca), Mchungaji William Mwamalanga, alionya kuwa mpango huo ni matokeo ya uhasama, ufisadi, uzushi, udini, fitna na majungu yaliyojikita ndani ya chama tawala, ili kudhohofisha Serikali na vyombo vyake.
Mchungaji Mwamalanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa mtandao wa Thren, alisema kimsingi wanaotakiwa kujiuzulu ni wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambao wameshindwa kutumia vikao na miiko ya uongozi kuwafukuza mafisadi papa ndani ya chama chao ambao alisema wameanza kutoa vitisho kwa wazalendo wanaojaribu kuzuia kasi yao ya ufisadi.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Pingamizi hilo lilitolewa jana na wanamazingira 217 kutoka mikoa ya Dodoma, Arusha, Mwanza, Shinyanga, Mara, Kigoma, Kilimanjaro, Unguja, Mbeya, Rukwa, Morogoro, Ruvuma, Kagera, Pwani, Dar es Salaam, Lindi, Tanga, Mtwara na Tabora ambao wamesema kauli hizo zinalengo la kuvuruga amani ya nchi.
Wanaharakati hao wamewataja wabunge 46 na mawaziri 13 ambao walisema wamekuwa wakizunguka maeneo mbalimbali nchini kuwahamasisha wananchi waunge mkono ajenda yao ya kumtaka Rais ajiuzulu.
Mkurugenzi Mkuu wa taasisi ya kuhifadhi misitu na mazingira (Mreca), Mchungaji William Mwamalanga, alionya kuwa mpango huo ni matokeo ya uhasama, ufisadi, uzushi, udini, fitna na majungu yaliyojikita ndani ya chama tawala, ili kudhohofisha Serikali na vyombo vyake.
Mchungaji Mwamalanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa mtandao wa Thren, alisema kimsingi wanaotakiwa kujiuzulu ni wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambao wameshindwa kutumia vikao na miiko ya uongozi kuwafukuza mafisadi papa ndani ya chama chao ambao alisema wameanza kutoa vitisho kwa wazalendo wanaojaribu kuzuia kasi yao ya ufisadi.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI