Wabunge 10 wa chadema walikataa kuingia bungeni ni akina nani?
"Wabunge hao kuwa ni Zitto Kabwe (Kigoma Kaskazini) ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Said Arfi (Mpanda Mjini) ambaye ni Naibu Mwenyekiti Taifa wa chama hicho, Mhonga Luhwanya (Viti Maalum), Jonh Shibuda (Maswa Magharibi), Maulida Komu (Viti Maalum).
Wengine ni Profesa Kulikoyele Kahingi,(Bukombe), Rachel Mashishanga(Viti Maalum), Raya Ibrahimu(Viti Maalum), Lucy Owenya (Viti Maalum) na Suzan Lyimo(Viti Maalum)...............
Mbona wote majina yanaonekana kulandana ? Au ndo walitaka wamsapoti jeykey mwenye asili yao? Mbona wana mambo ya ajabu! Zitto adai udini unasumbua ,ana akili timamu kweli? Ivi kugomea jk udini uko wapi? Zitto ondoka chadema haraka,naapa siingii chadema mpaka msaliti aondoke!
acha upumbavu tunazungumzia kutotii maazimio ya kikao halali cha wabunge wa chama.....lazima chadema iwe na kauli moja.....acha kueneza kansa....akili zako ziko sawa?jamani tuache majungu, hii habari ya zitto kutoonekana bungeni haina tija yoyote. Kama adhima ya chama ilifikiwa (kwa asilimia 90) na watanzania wengi wanakubaliana na msimamo wa chama, aya mengine sidhani kama ni tatizo. Kwenye mkusanyiko wowote lazima utegemee watu wengine kufikiria au kutenda tofauti na maadhimio ya wengi. Maadam zitto akubakia ndani ya bunge (hasingeweza kubakia kwa sababu hakuwepo), na kutokufika kwake bungeni inatosha kuonyesha kuwa anakubaliana na msimamo wa wabunge wenzake wa chama kwa kutokumsikiliza jk.
Pili, lazima tujenge utamaduni wa kuheshimu mawazo ya watu wengine na kuamini kwamba sio lazima wote tuwe na wazo moja. Mwenzetu anapowaza tofauti na sisi, tukubaliane nae na tumsikilize. Inawezakana akawa sahihi zaidi yetu, ndo demokrasia hii. Tukianza hii habari ya kukubali kila kitu na kufikiri kama mwenyekiti tutakuwa tunarudi nyuma na kuukaribisha umwinyi ulioko huko ccm, ambako kuhoji mawazo ya mwenyekiti ni uhaini.
acha upumbavu tunazungumzia kutotii maazimio ya kikao halali cha wabunge wa chama.....lazima chadema iwe na kauli moja.....acha kueneza kansa....akili zako ziko sawa?
na walioangalizia hotuba kwenye ukumbi mdogo wa wabunge watachukuliwa hatua gani? Upuuzi mtupu na unafiki. Unakataa kumuona live, kisha unaenda kumtazama kwenye kioo.
Inahitajika akili kujua...
Iko sababu, bora ambao hawakwenda maana hawakushiriki unafiki ule :embarrassed: