Wabongo ni wa ajabu sana

Frey Cosseny

JF-Expert Member
Feb 4, 2015
1,984
1,405
Tanzania tuna watu wa ajabu sana! Watu waliokuwa wanabeza Serekali zilizopita kuwa ni Dhaifu hazikusanyi kodi Leo ndiyo hao Leo wanalalama Serekali ya Awamu ya Tano inavyoziba Mianya ya ukwepaji Kodi Bandarini,Utalii,na kwingineko! Lazima Msome alama za nyakati ya Serekali ya Mh Magufuli hairudi nyuma katika suala la Ukusanyaji kodi! Kama hamuwezi kulipa kodi za Watu Bandarini ziko nyingi nendeni huko Mombasa,Beira na Weles, na Mbuga ziko nyingi kakwepeni kulipa kodi huko! Tumechoka na kelele zenu ,Wacheni Viongozi Wazalendo Wafanye kazi! "Shamba la Bibi limeuzwa" Poleni!
 
Mkuu watu sio kuwa walikuwa wanalalamika kuhusu kukwepa kulipa kodi issue hapa ni vyanzo vipya na ubunifu katika kukuza biashara ili ukusanye kodi zaidi na zaidi, leo umepandisha ushuru wa viingilio mbugani, wafanyabiashara wanalalamika kuwa wanalipa kodi nyingi sana, kodi inayolipwa haiwafikii wananchi hata sukari tu hawana, mkuu hicho ndio kilio na wala sio kitu kingine.
 
Endelea kukamua ng'ombe huyo huyo mmoja tuone kama maziwa yataongezeka
 
Hii nchi inarasilimali kibao haiwezekani tukusanye kodi kwa namna Rwanda wanavyokusanya kodi..tuna vyanzo vingi vya mapato,watu wanacho lalamikia ni kwanini hivi vyanzo vyingne havimpi unafuu mwananchi zaidi mzingo wote anabebeshwa yeye?mfano mzuri ni kwenye mataifa ya kiarabu zaidi wanategemea mafuta na bandari tu na tunaweza kuona tofauti..uku kwetu tuna bandari,gesi,mbunga madini ya kila aina,misitu,ardhi,nk kwann serikali inalazimisha kumkandamiza mwananchi!?
Alikija juzi waziri mkuu wa India raisi wetu aliomba msaada wa bajaj na pikipiki teh teh
 
Tanzania tuna watu wa ajabu sana! Watu waliokuwa wanabeza Serekali zilizopita kuwa ni Dhaifu hazikusanyi kodi Leo ndiyo hao Leo wanalalama Serekali ya Awamu ya Tano inavyoziba Mianya ya ukwepaji Kodi Bandarini,Utalii,na kwingineko! Lazima Msome alama za nyakati ya Serekali ya Mh Magufuli hairudi nyuma katika suala la Ukusanyaji kodi! Kama hamuwezi kulipa kodi za Watu Bandarini ziko nyingi nendeni huko Mombasa,Beira na Weles, na Mbuga ziko nyingi kakwepeni kulipa kodi huko! Tumechoka na kelele zenu ,Wacheni Viongozi Wazalendo Wafanye kazi! "Shamba la Bibi limeuzwa" Poleni!

Nonsense, haKuna anayesema mianya ya rushwa isizibwe and the like, we do not want that at the expense of democracy
 
Tanzania tuna watu wa ajabu sana! Watu waliokuwa wanabeza Serekali zilizopita kuwa ni Dhaifu hazikusanyi kodi Leo ndiyo hao Leo wanalalama Serekali ya Awamu ya Tano inavyoziba Mianya ya ukwepaji Kodi Bandarini,Utalii,na kwingineko! Lazima Msome alama za nyakati ya Serekali ya Mh Magufuli hairudi nyuma katika suala la Ukusanyaji kodi! Kama hamuwezi kulipa kodi za Watu Bandarini ziko nyingi nendeni huko Mombasa,Beira na Weles, na Mbuga ziko nyingi kakwepeni kulipa kodi huko! Tumechoka na kelele zenu ,Wacheni Viongozi Wazalendo Wafanye kazi! "Shamba la Bibi limeuzwa" Poleni!
Ni Serekali? serikali au siri-kali?
Frey unanunua ze utamu (sukari) sh. ngapi kwa kilo moja?

Pili kwa nini kodi ya kuku, mbuzi na baiskeli haijaanzishwa bado ili tuisome namba na alama za nyakati?

Tatu. Unaelewa madhara ya watu(wafanyabiashara) kuacha kutumia bandari zetu na kutumia Mombasa, Beira au Afrika Kusini kwa uchumi wa Tanzania?

Je maisha yako na ya watu wa mtaani kwenu yamekuwa "maisha bora kwa mwendokasi" au unaishi/mnaishi kama malaika baada ya serekali inayokusanya kodi kuwa madarakani kwa miezi 6+?

Hakuna anayepinga Kaizari kuchukua vilivyo vyake, achukue tu, tena kwa mwendokasi.
La msingi kwa usalama wako, funga mkanda na kaza mkanda, uchumi unataka kupaa angani.
 
Back
Top Bottom