Wabongo angalieni hii kitu....!

SAD!!

Halafu ndiyo tunasikia Spika wa Bunge letu hataki hoja zisikilizwe mpaka awepo yeye!! Kama hili si tusi kwa Mama Makinda ni nini?!!

Pole pole, viongozi wetu wanachochea kujengeka kwa chuki kama hizi za Kenya. Tuombe Mungu yasitokee, maana kwa nchi kama Tanzania, hakutakuwa na suluhisho!! Na njia kabambe ya kuzuia mambo kama yanavyofanyika kwa majirani zetu hivi sasa ni kwa kero zilizopo kusikilizwa ipasavyo na maovu yote kuanikwa nje na wahusika kuadhibiwa wakati sheria zetu na majengo ya mahakama bado yanakinga.... tusisubiri kuomba Mungu yasitokee ya Kenya tuu bali tutende yaliyoya haki hivi sasa kama kinga ya adhabu zisizo haki kuanza kutendeka au sheria na majengo ya mahakama kuanza kuchomwa moto!!

SteveD.
 
Ooh my God inatisha Kibaki and Raila are accountable on deaths of innocent Kenyans ...should both be taken to the international court of justice...The Hague
 
http://www.washingtonpost.com/wp-dyn/content/gallery/2007/12/31/GA2007123102000.html

Naomba muangalie hizi picha nd'o muone hali halisi iliopo hapo nchi jirani.Some of the pics are really brutal I should say.


Usihofu Watanzania sio mazuzu. Hatuwezi kupigana wenyewe kwa wenyewe. Ati CUF na CCM au Mchaga na Mgogo. Tupigane kwa sababu ya uchaguzi? Hawa wana lao. Na atakayeanza kutuvuruga sisi tutampiga yeye. Tumeshapokea wakimbizi wengi sana. Tunajua madhara ya vita. Aidha tuna uwezo wa kusema na njaa zetu. Fikiria M'Bongo analipwa mshahara sh. 70,000/= kwa mwezi ana watoto saba wanasoma, ana wake wawili na nyumba ndogo. Anaishi bila taabu. Kamlete Mmarekani Bongo, mlipe mshahara wa dola mia 200 tu bila mke wala mtoto uone atakavyohaha kama siyp kufa kabisa. Wabongo sisi ngangari bwana
 
Kwa bahati mbaya, sikubaliani na nukta zako, takriban zote:
Usihofu Watanzania sio mazuzu.
Hata hao wapiganao nao si mazuzu. Wana sababu zao; ama zitokanazo na udhaifu wao, au zitokanazo na kunyimwa haki zao. Nasi tuna udhaifu wetu, na kuna unyimwaji wa haki ktk nyanja mbalimbali. Kumbuka, mafisadi kuachwa bila kupewa adhabu wanazostahili, wakati wakosaji wadogo wadogo wanaadhibiwa, ni unyimwaji wa haki za raia. Je, jambo km hili haliwezi kuwa sababu ya machafuko. Si lazima sababu za wakenya ziwe sawa na za kwetu.

Hatuwezi kupigana wenyewe kwa wenyewe. Ati CUF na CCM au Mchaga na Mgogo. Tupigane kwa sababu ya uchaguzi? Hawa wana lao. Na atakayeanza kutuvuruga sisi tutampiga yeye.
Alilolifanya binadamu, binamu mwingine yeyote analiweza. Sijui "wenyewe kwa wenyewe" ni akina nani, na "yeye" ni nani! Wote hao wanaweza kuwa watanzania.

Tumeshapokea wakimbizi wengi sana. Tunajua madhara ya vita. Aidha tuna uwezo wa kusema na njaa zetu. Fikiria M'Bongo analipwa mshahara sh. 70,000/= kwa mwezi ana watoto saba wanasoma, ana wake wawili na nyumba ndogo. Anaishi bila taabu. Kamlete Mmarekani Bongo, mlipe mshahara wa dola mia 200 tu bila mke wala mtoto uone atakavyohaha kama siyp kufa kabisa. Wabongo sisi ngangari bwana

Ktk dunia ya leo, ya utandawazi, hakuna asiyejua madhara ya vita.
Ukimya wa watanzania wengi si k/sbb ya kuridhika na hali halisi, bali unatokana na uwoga wa kisiasa, kutojua haki, na kutokuwa na imani na serikali na vyombo vya dola. Wala tusijidanganye kuwa nchi yetu ni "kisiwa cha amani", bali nchi yetu ni tulivu kutokana na yale niliyokwishayataja. Hakuna amani ya kweli ktk nchi km wananchi wake hawana amani ktk mioyo yao.

KWA KIFUPI, TUSIJIDANGANYE, TUKAENDELEA KUWA WADANGANYIKA.
 
Nyerere alimsihi Kenyatta Tgka isubiri uhuru ili pamoja na Uganda kuanzisha shirikisho- na Mzee Kenyatta kuwa Raisi wa Kwanza- yeye Kenyatta kwa ubinafsi wake akakataa!

Sisi wakati Nyerere anaimarisha umoja wa kitaifa, JKT, Azimio Kenya alitucheka- sasa kwenda kwao mbele kiuchumi ndo haya tunayaona leo!
 
tatizo la kenya sio la kikabila. mimi siamini kwamba viajana wa kizazi hiki cha dotcom na katika ulimwengu huu unaokimbia kwa kasiya tsunami, kuna watu wanaendekeza vitendo vya ukabila.

nionavyo mimi ni vijana wanataka mabadiliko! wamechoshwa na mambmo ya wapigania uhuru kuzidi kujigawia nchi yao kama wanavyotaka kama mkulima shambani mwake. ni wakati wa kubadilika na kuwa na njia mpya za ufanyaji mambo.

tanzania tutaelekea huko muda si mrefu hata kama mafisadi hawataki. spika sitta ni kati ya mazoba tulionao bungeni ambaye anaedesha bunge kiholela!

nashangaa wale jamaa wanaojiita ma-mediator wanaenda kenya kufanya nini. sijaona hata mmoja wao akimwambia kibaki live kwama yeye ni kibaka mdokoa democrasia ya kenya. wote wanamtaka odinga akubali yaishe. this is very dangerous to kenyan

odinga akitaka ujinga basi akubali yaishe uone soo litakavyokuwa kubwa sana! vijana wa kenya hawamtaki Odinga, bali wanataka mabadiliko na njia mpya za utawala.

ma-mediators waache kupoteza resources kwenda kenya kupiga porojo, bora watume ujumbe wao kwenye vyombo vya habari au wawatumie emails.

tatizo ni kwamba mediators wakifika nairobi wanakuwa wanategemea ulinzi wa jeshi lililoko chini ya kibaki na hivyo wanakuwa hawana nguvu za kumpinga live lakini kumbuka pia wanalinda maslahi ya nchi zinazo watuma!
 
.....na wanaoumia, kuteseka na kufa ni walalahoi, walalahai wako mjini Nairobi na maisha yanaendelea kama hakuna misukosuko nchini mwao.
 
hivi odinga angekubali kunyongwa na kujitahidi kuweka mikakati ya kuwa na uchaguzi ufuatao kuwa huru zaidi na makosa yalioooooopo yasijutokeze tena angehasirika nnnn?

au haki itendeke lazma yeye awe rais ?
 
Fikiria M'Bongo analipwa mshahara sh. 70,000/= kwa mwezi ana watoto saba wanasoma, ana wake wawili na nyumba ndogo.

Lakini swali linakuja kwanini unaamua kuwa na watoto wengi wakati unajua huna uwezo wa kuwatunza, ina maana watoto hao unawapata kwa bahati mbaya au unalazimishwa kuwa nao. Umasikini na tabu nyingine tunajitakia
 
hivi odinga angekubali kunyongwa na kujitahidi kuweka mikakati ya kuwa na uchaguzi ufuatao kuwa huru zaidi na makosa yalioooooopo yasijutokeze tena angehasirika nnnn?

au haki itendeke lazma yeye awe rais ?
The problem is that you can't trust Kibaki for nothing. Kumbuka kua 2002 alipewa mamlaka na wakenya ili kuleta haya mabadiliko watu wanayopigania leo. Je alifanya nini...si aliwasahau wananchi na kujizunguka na jamaa zake. Wakenya wanalilia kitu kimoja muhimu ambacho kitatatua shida zao zote...nacho ni katiba mpya.Kibaki promised to do that in the first 100 days in office.Kisha ikawaje...jamaa alikataa licha ya kwamba referendum ilionyesha watu wanataka ile Bomas of Kenya draft.Sababu ni kwamba the powers of the presidency would be reduced. Hapa nd'o walalahoi wakaanza kuona ubinafsi wa huyu bwana na ukabila wake. Wewe unadhani Kibaki will call a meeting to overhaul the ECK...utasubiri m'da mrefu sana.Yote wanayofanya ni kumuandalia Uhuru Kenyetta kiti cha urais hapo 2012 na wakenya washaona hii kitu na wamekataa.. We do not need leaders like Kibaki or M7 hapa Easti maana wanatuchelewesha mambo kibao.
 
Fikiria M'Bongo analipwa mshahara sh. 70,000/= kwa mwezi ana watoto saba wanasoma, ana wake wawili na nyumba ndogo. Anaishi bila taabu.
Hii nayo ni sifa ya sisi kujivunia? Mhhh, hapana haijakaa sawa! Halafu tunategemea kushinda mapambano dhidi ya ufisadi... kwa mwendo huu kaazi kwelikweli...
 
hivi odinga angekubali kunyongwa na kujitahidi kuweka mikakati ya kuwa na uchaguzi ufuatao kuwa huru zaidi na makosa yalioooooopo yasijutokeze tena angehasirika nnnn?

au haki itendeke lazma yeye awe rais ?

your right. kama Odinga inaipenda sana Kenya na wakenye, basi awenao kwenya maandamano na akifa si watagombea wengine? kwani lazima yeye ndo awe rais?
u hav got a point sir. mbona kuna watu walifia uhuru, dini nk, sasa kwanini Odinga asiwe tayari kuifia kenya na wakenya if he real love them?
 
your right. kama Odinga inaipenda sana Kenya na wakenye, basi awenao kwenya maandamano na akifa si watagombea wengine? kwani lazima yeye ndo awe rais?
u hav got a point sir. mbona kuna watu walifia uhuru, dini nk, sasa kwanini Odinga asiwe tayari kuifia kenya na wakenya if he real love them?

Tangu lini uliona "Amirijeshi mkuu" anakwenda mstari wa mbele? Kila mapambano yana strategy zake unafikiri Odinga akijipeleka kwenye kifo ndiyo Kibaki ataachia Kiti? Of course Odinga anawapenda Wakenya na wao wanampenda otherwise wasingekubali kujitoa kafara. Ila ambacho sikubaliani nacho ni uuaji wa raia wasio na hatia unaofanywa na pande zote mbili yaani Serikali na Wapinzani.
 
Lakini swali linakuja kwanini unaamua kuwa na watoto wengi wakati unajua huna uwezo wa kuwatunza, ina maana watoto hao unawapata kwa bahati mbaya au unalazimishwa kuwa nao. Umasikini na tabu nyingine tunajitakia

Haya mambo si ya kujitakia Bongolander, wewe fikiria, huyu baba kwake ndio hakuna umeme, ikifika jioni giza linaingia hamna activity wala starehe yeyote anayoweza kujikita nayo (hawezi kuangalia game kwenye TV, kwanza hana, hawezi kujisomea, taa hamna n.k) kula uroda na mamaa ndio starehe iliyopo na haitolei pesa, sasa mtu huyu ataacha kuzaa watoto wote hao? ...
 
hivi odinga angekubali kunyongwa na kujitahidi kuweka mikakati ya kuwa na uchaguzi ufuatao kuwa huru zaidi na makosa yalioooooopo yasijutokeze tena angehasirika nnnn?

au haki itendeke lazma yeye awe rais ?

Risk ya kuleta mabadiliko ni lazima ichukuliwe. Na wale wanaokataa risk siku zote ni masikini na wasiondelea. Bila Vasco Da Gama kuchukua risk ya kwenda India wazungu wangetawala dunia.

Bila Columbus kuchukua risk ya kwenda India asingevumbua Marekani.

Bila kuchukua risk ya kurusha vyombo angani, tusingekuwa na mawasiliano ya anga.

Na risk zote hizo zilileta maafa ya vifo.

Nakuomba Odinga usirudishe majeshi yako nyuma na kusikiliza matapeli wa kitanzania wanaotaka maendeleo ya kuletewa kwenye kisaani kama mamwinyi wanaokula sambusa.
 
Haya mambo si ya kujitakia Bongolander, wewe fikiria, huyu baba kwake ndio hakuna umeme, ikifika jioni giza linaingia hamna activity wala starehe yeyote anayoweza kujikita nayo (hawezi kuangalia game kwenye TV, kwanza hana, hawezi kujisomea, taa hamna n.k) kula uroda na mamaa ndio starehe iliyopo na haitolei pesa, sasa mtu huyu ataacha kuzaa watoto wote hao? ...

This is very funny Kisura...nakumbuka mwalimu alikuwa anatuambia hii kitu darsani chini ya mada 'The vicious cycle of Poverty'... wewe usiekua na kitu n'do mwanzo anasa ya uroda umeipa kipa umbele maana hauna TV wala redio...afu pia mwili umechoka kwa kukoroga zege kwa Mulji...Fanaleki.We cant win for ishhh!!!
 
Mugo"The Great";135136 said:
Tangu lini uliona "Amirijeshi mkuu" anakwenda mstari wa mbele? Kila mapambano yana strategy zake unafikiri Odinga akijipeleka kwenye kifo ndiyo Kibaki ataachia Kiti? Of course Odinga anawapenda Wakenya na wao wanampenda otherwise wasingekubali kujitoa kafara. Ila ambacho sikubaliani nacho ni uuaji wa raia wasio na hatia unaofanywa na pande zote mbili yaani Serikali na Wapinzani.

Mugo "The Great" heshima yako upewe kaka.
Hapo umemjibu huyu bwana swafi sana nami nataka niongeze senti zangu hamsini.Raila ashafanya kila kitu kuonesha kwamba hajali maisha yake ila ya wakenya wote.Katika kumbukumbu za historia ya Kenya huyu bwana alifungwa miaka kama tisa hivi na serikali ya Moi.Aliswekwa lupango bila trial wala nini, akasota miaka yote hio Kibaki akiwa serikalini kama V-P.Mkewe pia aliteseka na kibarua kuoteshwa majani simply because mume wake alikua controversial.Kisha during the fight for multipartysim yeye na marehemu babake walikua mstari wa mbele wakikwepa risasi na mabomu ya kutoa machozi in the streets of Nairobi while Kibaki was fence sitting.Baada ya section 2A kuwa repealed nd'o hawa kina Kibaki wakaingia upinzani.Kwa hivyo Raila has done a lot in making sure the growth of democracy is upheld in Kenya na kama mtu hajui basi ni aelimishwe!
Wenyewe wamnamuita "Agwambo the Enigma'.Viongozi kama hawa nd'o wanahitajika hapa Easti ili kuhakikisha kua demokrasia inakuzwa ipasavyo.Naomba kuwasilisha.
 
Back
Top Bottom