Wabara wachomewa makazi Zanzibar

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
IMESADIKIWA Watu wapatao 120 wenye asili ya Tanzania Bara wamekosa makazi kwa kuchomewa nyumba zao moto katika kijiji cha Pwani, Mchangani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Mbali na kuchomewa makazi pia watu hao wameweza kupoteza mali zao kwa kuteketeza maduka na mali mbalimbali wakati motohuo ukiendelea

Watu wanaodaiwa kutoka kijiji hicho ndio waliosababisha moto huo kwa kuanza kumwagia mafuta ya petrol maduka hayo huku wakiwa na vifaa vya mapigano yakiwemo mapanga na marungu walipovamia eneo hilo.

Imedaiwa kuwa wakati moto huo ulipoanza watu wenye mali hizo walipokuwa katika juhudi za kuokoa mali zao walizuiliwa kwa kushikiwa mapanga wasiokoe mali hizo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, Mselem Mtuliya alisema tukio hilo lilitokea Jumamosi majira ya saa 10 jioni.

Alisema tayari watu saba wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo huku jeshi la polisi likiendela na uchunguzi na taratibu za kuwafikisha mahakamani watu hao zinaendelea.

WAtu hao wengi wanaodaiwa kuwa wenyeji wa Kilimanjaro walikuwa wamewekeza kijijini hapo kwa kufanya biashara kama vinyago na nyingine nyingi kuwauzia watalii na wenyeji wa eneo hilo walikuwa wakiwabughudhi na kuwataka waondoke kijijini hapo

Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai, Zanzibar (DCI), Muhidini Juma Mshiri, aliwataka wananchi wawe watulivu wakati Jeshi la Polisi likiendelea na uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.

Nae Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Seif Ali Idd, aliwataka waathirika waorodheshe thamani ya mali walizopoteza ili serikali iangalie njia za kuwasaidia.

Pia ameagiza waathirika hao wapewe eneo jipya la kuishi na amekemea suala la ubaguzi, akisema kila raia wa Tanzania ana uhuru wa kuishi sehemu yoyote nchini Tanzania.
 
Back
Top Bottom