Wababe wa Simba kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho wachezea kichapo cha 4-0 kwa AS Vita ya DR CONGO

Mawembasa1979

JF-Expert Member
Feb 26, 2015
2,152
2,500
Wababe wa Simba kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho leo tarehe 24/10/2018 wamechapwa magoli manne bila majibu. Hadi mapumziko wenyeji AS Vita walikuwa wanaongoza kwa mabao 2-0, mabao yaliyofungwa na E. Ngoyi dakika 6 na 39. Kipindi cha pili Al Masry walijitahidi kuweza kusawazisha mabao hayo. Hata hivyo walijikuta wakifungwa bao la tatu na mshambuliaji hatari aitwaye J. Makusu. Kuingia kwa bao hilo kulisababisha Al Masry kutaka kugomea mchezo kwa kuweka mpira kwapani kama ambavyo Simba wamewahi kugomea mechi na Yanga baada ya mapumziko. Wachezaji wa Al Masry walidai mfungaji alikuwa ameotea kabla ya kufunga bao hilo.
Hata hivyo, Al Masry walikubali kuendelea na mchezo na kufungwa bao la nne dakika za nyongeza na mfungaji akiwa ni M. Batezadio.
Katika mchezo huo Al Masry walionesha kiwango kibovu cha uchezaji. Kiasi kwamba haieleweki kwa nini waliweza kuwatoa Simba kwenye michuano hiyo.
 
Hilo ndio swali la msingi,
Kwanza sio kweli kuwa Al Masry wamefika fainali bali wametolewa kwenye nusu fainali baada ya kutoka sare kule kwao Misri na kufungwa leo mabao 4-0. Kuhusu hiyo timu ya Botswana si ajabu kutolewa Kwa kuwa walikuwa wanacheza kwenye champions league ambako kuna Timu bora ukilinganisha na Conferadation (Shirikisho) ambako timu zilizoshindwa kupita kwenye mchujo wa Champions League zinaangukia huko. Nadhani umenielewa Mtani wangu.
 
Umejibu kishabiki. Kwani Township Rollers walikuwa wangapi kwenye kundi lao ?Kuthibitisha kwamba ni vibonde na pamoja na ukibonde wao waliwatoa Yebo Yebo?
Mbona huyatujulisha kuhusu wababe wenu Rayon ya Rwanda waliomaliza wa pili kwenye kundi ambalo mlishindwa hata kuwepo na wao Rayon wakiwa wa pili. Walipokutana na Enyimba wakapigwa goli 5 kwa moja? Rayon wababe wenu walifungwa 5 mbona hukutuhabarisha?Hivi mwaka huu Novemba mtakutana na nani?
 
Ningekuwa shabiki wa timu iliyofungwa na Town Rollers ya Botswana tena nyumbani goli 2-1 ningefunga mdomo na singekumbusha hiyo aibu kubwa. Tatizo kuna mashabiki wa Yebo Yebo wana uso wa mbuzi na kumbukumbu fupi.
 
Wazi zuri matokeo dhidi ya Mbao misimu 2 iliyopita mpaka msimu huu.Au vipi?Tena ili izidi kunoga matokeo ya Kirumba na Taifa.
 
Umejibu kishabiki. Kwani Township Rollers walikuwa wangapi kwenye kundi lao ?Kuthibitisha kwamba ni vibonde na pamoja na ukibonde wao waliwatoa Yebo Yebo?
Mbona huyatujulisha kuhusu wababe wenu Rayon ya Rwanda waliomaliza wa pili kwenye kundi ambalo mlishindwa hata kuwepo na wao Rayon wakiwa wa pili. Walipokutana na Enyimba wakapigwa goli 5 kwa moja? Rayon wababe wenu walifungwa 5 mbona hukutuhabarisha?Hivi mwaka huu Novemba mtakutana na nani?
Tunakutana tena na Mbao Mkuu!!!
 
Wenye kuwakilisha Tanzania wanajulikana na wanaotembeza bakuli ili kulipa mishahara ya wachezaji wanajulikana.
 
Wababe wa Simba kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho leo tarehe 24/10/2018 wamechapwa magoli manne bila majibu. Hadi mapumziko wenyeji AS Vita walikuwa wanaongoza kwa mabao 2-0, mabao yaliyofungwa na E. Ngoyi dakika 6 na 39. Kipindi cha pili Al Masry walijitahidi kuweza kusawazisha mabao hayo. Hata hivyo walijikuta wakifungwa bao la tatu na mshambuliaji hatari aitwaye J. Makusu. Kuingia kwa bao hilo kulisababisha Al Masry kutaka kugomea mchezo kwa kuweka mpira kwapani kama ambavyo Simba wamewahi kugomea mechi na Yanga baada ya mapumziko. Wachezaji wa Al Masry walidai mfungaji alikuwa ameotea kabla ya kufunga bao hilo.
Hata hivyo, Al Masry walikubali kuendelea na mchezo na kufungwa bao la nne dakika za nyongeza na mfungaji akiwa ni M. Batezadio.
Katika mchezo huo Al Masry walionesha kiwango kibovu cha uchezaji. Kiasi kwamba haieleweki kwa nini waliweza kuwatoa Simba kwenye michuano hiyo.
Hawa Hawakuwahi kuifunga Simba uwanjani kwenye open gameplay. Tuweke kumbukumbu sawa
 
Back
Top Bottom