Wababa wanalalamika sana kutengwa na watoto wao kimawasliano hata kiuchumi. Je, shida ni nini? Wamama mnaliongeleaje hili? Watoto mnafanya haya kweli?

mama D

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
19,763
35,201
Kumekua na malalamiko mengi kwenye jamii za kitanzania na kiafrika kwa ujumla mara watoto wanapokua na kuanza kujitegemea na umri wa wazazi kusogea, wototo huwa wanakua karibu na mama zao zaidi ya baba zao.

Wababa wengi huumizwa na jambo hili na kujiona kutengwa na watoto wao baada ya watoto hao kupata mafanikio huku wakiamini kabiasa kwamba wake zao (wamama wa hao watoto) wanawafurahia hilo jambo na wana ushirika mkubwa na watoto wao katika kuwatenga

Wamama huwa tunakosea wapi hadi hawa wababa wafikie kulalamika kiasi hiki? Au umri ukienda mapenzi yanaisha na title ya mume inabadilika?

Nini kinawapelekea watoto kuwa na hii distance kubwa kwa baba zao? Je, wanajua kama na wao siku wakizeeka wakatengwa au kuhisi kutengwa itawaumiza?


Ikumbukwe hakuna mtoto wa mzazi mmoja, katika mazingira yoyote yale mtoto atabaki kuwa wa baba na mama unless huyo baba au mama amkatae mtoto

Kwenye imani zetu pia tumeamrishwa kuwaheshimu baba na mama. Hiyo ni amri bila maswali, kazi ni moja tuu kutekeleza. Yaani huwezi sema sababu mama yuko hivi au baba yuko vile sitamheshimu! Matakwa ya amri ni kutekeleza tuu

Familia ni upendo na familia ndio faraja na kimbilio la wakati raha na taabu. Tudumishe upendo

Cc Bushmamy mirisho pm Asprin Sky Eclat 50thebe wahenga wenzangu wote
 
Unaousema n ukwel mkuu

Ila wababa tuache kulea watoto kikauzu badala yake tubadirike hasa wakat huu ambao ulimwengu unaenda kasi unalea mtoto kwa mifumo ya miaka 1980 wakat dunia inehama huko

Mtoto anakupigia simu anataka kujua nyumban mnaendeleaje wewe unajibu kifupi na hauoneshi kufurah kuwa mtoto kakupigia

Ila ukimpigia mama anaonesha furaha anakueleza mambo muhimu kuhusu nyumban

Unategemea mtoto atampenda au atampigia Nani simu kila wakat pale anapohtaj kujua Jambo fulani

.....wazazi hasa wakiume tubadilike....

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mama yupo busy na watoto muda mwingi kuliko baba haijalishi wote ni waajiriwa au la, muda mwingi wanaoupata kuwa na mama unajenga ukaribu Kati ya mama na watoto tofauti na baba hali inayopelekea hata wanapokua wakubwa wanakua karibu Sana na mama na kumsahau baba

Kina baba wanatumia muda mwingi kutafuta pesa kwa ajili ya familia (hapa sizungumzii wale wanaokimbia majukumu ya kulea familia na kuwaachia kina mama pekee) kiasi muda mwingi anakua busy mno, anapata pesa anampa mama kwaajiki ya ada na matumizi mengine ya familia watoto wanajua mama ndio anayehangaika kwa kila kitu

Mazingira niliyaweka kwa watoto wangu ni kuwaweka karibu na baba yao Ili hata huko mbeleni waje kuona namna gani baba yao pia liua anahangaika kwa ajili yao .Ukaribu kwa maana kwamba endapo baba atatoa hela ya ada nawaambia watoto kwamba baba kanipa hela nikawalipie ada, kanipa hela ya kuwanunulia nguo nk hii itawajengea upendo Kati yao kwa kuona kwamba baba yao anawajali pia

Sent from my CPH2015 using JamiiForums mobile app
 
Si nyie ndo mnawalisha sumu! Yani wanawake hamjuagi mnachotaka adamu alikuwa anaishi vizuri tu mpaka akina mende Simba na wanyama wote!.. alipokuja Sasa mwanamke akafanya yake simba akaanza kumuona adamu Kama ugali tu..🤣

Hahaha nimecheka uwiiiiii nitarudi kucoment baadae🤣🤣🤣🤣🤣🤣😅
 
Kumekua na malalamiko mengi kwenye jamii za kitanzania na kiafrika kwa ujumla mara watoto wanapokua na kuanza kujitegemea na umri wa wazazi kusogea, wototo huwa wanakua karibu na mama zao zaidi ya baba zao.
Shida ni tawala za kishoga na kihuni duniani kushika hatamu na haki zinazoitwa za wanawake kuruhusiwa, yaani mifumo ya kifamilia imevurugika na kuvunjika. Wanawake wako huru kuzaa na yeyote na wanaume tofauti tofauti, na wanaume hawana tena mamlaka na watoto.

Baba akikataza mtoto wa kike kuvaa nusu uchi hadharani mama anaruhusu, mtoto wa kiume akivaa hereni na kusuka nywele baba akikataza mama anajibu niachie mwanangu! Ukiwapiga unashitakiwa ukatili wa kijinsia!!! Basi watoto wanaona baba mnoko hawapendi mama ndiyo anawapenda. Bila kurudi ktk maadili ya dini na ya tamaduni zetu wanaume tutazidi kutengwa tu.
 
Unaousema n ukwel mkuu

Ila wababa tuache kulea watoto kikauzu badala yake tubadirike hasa wakat huu ambao ulimwengu unaenda kasi unalea mtoto kwa mifumo ya miaka 1980 wakat dunia inehama huko

Mtoto anakupigia simu anataka kujua nyumban mnaendeleaje wewe unajibu kifupi na hauoneshi kufurah kuwa mtoto kakupigia

Ila ukimpigia mama anaonesha furaha anakueleza mambo muhimu kuhusu nyumban

Unategemea mtoto atampenda au atampigia Nani simu kila wakat pale anapohtaj kujua Jambo fulani

.....wazazi hasa wakiume tubadilike....

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

Asante mkuu Peramiho yetu
Kwakweli ifike mahala tuangalie tulipoangukia tukubali makosa kubadilika
 
Kumekua na malalamiko mengi kwenye jamii za kitanzania na kiafrika kwa ujumla mara watoto wanapokua na kuanza kujitegemea na umri wa wazazi kusogea, wototo huwa wanakua karibu na mama zao zaidi ya baba zao.
Wewe sindio unawaharibugi machalii unampondea mshua! Af sahizi unajidai hujui nini sababu 😅😅😅 unawachonganisha madogo na mzee kwa kujidai we unaonewaga sana
 
Mm ninae best yangu 68 yrs ni male anae watoto 6 wa mwisho ndio nalingana nae mm

But anaweza kaa hata 10months hakuna mtoto wake anaempigia simu wala kumuuliza chochote na yy tupo nae hapa kijijini wala hawazi

Anaishia tu kulalamika kuwa watoto hawamjali wala nn wakimtumia pesa mingi sana ni 15k na hata wakija home anaambulia kupewa chupa ya konyag kubwa tu

Watoto wa kuiume jua mnayowafanyia baba zenu sasa hiv,ndio mtakayofanyiwa na nyie mtakapozeeka

What goes around comes around
 
Wakati mwingine wazee wanasababisha wao.
Mm ninae best yangu 68 yrs ni male anae watoto 6 wa mwisho ndio nalingana nae mm

But anaweza kaa hata 10months hakuna mtoto wake anaempigia simu wala kumuuliza chochote na yy tupo nae hapa kijijini wala hawazi

Anaishia tu kulalamika kuwa watoto hawamjali wala nn wakimtumia pesa mingi sana ni 15k na hata wakija home anaambulia kupewa chupa ya konyag kubwa tu

Watoto wa kuiume jua mnayowafanyia baba zenu sasa hiv,ndio mtakayofanyiwa na nyie mtakapozeeka

What goes around comes around
 
Shida ni tawala za kishoga na kihuni duniani kushika hatamu na haki zinazoitwa za wanawake kuruhusiwa, yaani mifumo ya kifamilia imevurugika na kuvunjika. Wanawake wako huru kuzaa na yeyote na wanaume tofauti tofauti, na wanaume hawana tena mamlaka na watoto. Baba akikataza mtoto wa kike kuvaa nusu uchi hadharani mama anaruhusu, mtoto wa kiume akivaa hereni na kusuka nywele baba akikataza mama anajibu niachie mwanangu! Ukiwapiga unashitakiwa ukatili wa kijinsia!!! Basi watoto wanaona baba mnoko hawapendi mama ndiyo anawapenda. Bila kurudi ktk maadili ya dini na ya tamaduni zetu wanaume tutazidi kutengwa tu.

Sasa hapa wa kulaumiwa ni nani? Aliyepewa mamlaka ya kuwa kichwa au msaidizi wake?

Nadhani hili swala ni pana sana, tukiliangalia kwa kulaumiana na kunyoosheana vidole tutakuja kujikuta tuko na generation ya ajabu ajabu isiyokua na miiko wala maadili.

Tusimame kwenye nafasi zetu na tufanye majukumu yetu, turekebishane kwenye makosa huku tukiheshimu nafasi za wenzetu tutafika
 
Unaousema n ukwel mkuu

Ila wababa tuache kulea watoto kikauzu badala yake tubadirike hasa wakat huu ambao ulimwengu unaenda kasi unalea mtoto kwa mifumo ya miaka 1980 wakat dunia inehama huko

Mtoto anakupigia simu anataka kujua nyumban mnaendeleaje wewe unajibu kifupi na hauoneshi kufurah kuwa mtoto kakupigia

Ila ukimpigia mama anaonesha furaha anakueleza mambo muhimu kuhusu nyumban

Unategemea mtoto atampenda au atampigia Nani simu kila wakat pale anapohtaj kujua Jambo fulani

.....wazazi hasa wakiume tubadilike....

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

Wanawake wana akili sana! Laiti wangekuwa hawana hila tungefika mbali!

Usikubali kutegemea mwanamke Sio kifedha tu, hata kujihudumia, jikaze mwanaume!

Haya mambo mpaka unanawishwa mikono huwezi inuka kwenda kwenywe sink wakati wa kula huleta utegemezi hatari kwenye umri mkubwa!
 
Haya Mambo mlianza zamani sana

Mimi niwaombe wababa wabebe nafasi zao kwenye kutusimamia sisi wanafamilia, tena wawe wakali kidogo hapa kama mama wa taifa alivyokua mkali kwa chalamila alipoona anaharibu familia ya mwanza

Mkisema mtuachie wamama tufanye tutakavyo tutaharibu tuu...... hata Mungu anajua ndio maana aliwapa nyie mamlaka ya kuwa kichwa ili mtoe malekezo ya wapi tunaelekea kwetu
 
Wanawake wana akili sana! Laiti wangekuwa hawana hila tungefika mbali!

Usikubali kutegemea mwanamke Sio kifedha tu, hata kujihudumia, jikaze mwanaume!

Haya mambo mpaka unanawishwa mikono huwezi inuka kwenda kwenywe sink wakati wa kula huleta utegemezi hatari kwenye umri mkubwa!

Asante uttoh2002 Kwa kweli umeandika kitu kikubwa sana hapa lakini kwa ufupi mnooo natamani kama ungedadavua zaidi kwa faida yetu sote

Asante
 
Back
Top Bottom