wababa mliomo JF acheni kubania vitu katika familia,vingine ni vitu vya kawaida tu

Money Stunna

JF-Expert Member
Aug 9, 2011
13,054
6,281
900030_318403_287516004599104_260597767_n_jpg49a07cdf010c6c4041537b443c188cc3.jpeg 900030_318403_287516004599104_260597767_n_jpg49a07cdf010c6c4041537b443c188cc3.jpeg 900030_318403_287516004599104_260597767_n_jpg49a07cdf010c6c4041537b443c188cc3.jpeg

kuna wababa wengine kuangalia tv adi yeye aamue,anaacha amefungia tv,vitu vingine ni vya kawaida,wababa/wamama wapunguze ubabiloni
 
Daah haya maisha nayakumbuka enzi za 1995 tv zilikua adimu sana majumbani kwetu
 
Hii niliiona kwa jirani yangu mmoja, sikusita kuhoji na nikaambiwa mtoto wake mmoja amekuwa teja na haoni shida kuiba vitu hivyo na kuuza ili apate kete angalau moja.
Kazi kweli kweli.
 
enzi zetu.....TV inakaa chumbani kwa baba mpaka arudi ndo muombe itolewe,tena mnaangalia kipindi cha katuni kimoja alafu basi inarudishwa na stendi yake ya matairi,glassi zingine marufuku kugusa mpaka mgeni aje,album za picha kedekede kwenye kabati,ila bonge la ufunguo,watoto wanazionaga tu,ila ni marufuku kugusa....vitambaa vya sebuleni sasa wakati wa kuangalia Tiivii,ole wako upangarue,utakiona cha moto,kuondoa ugomvi bora tu ukae chini,kula kwenye kochi ni marufuku,ila baba anaruhusiwa.....baada ya kuangalia VIDEO mnaifunika VIDEO vizuuurrii,isiingie vumbi na vile vitambaa vya kufuma....na baba ndo anakaa na remote control,imefunikwa na ma-nylon kibao ili isizeeke.....akija mgeni nyumbani anafundishwa jinsi ya kuwasha na kuzima Tivii na namna ya kuweka mkanda asije akaugeuza.......kipindi hicho kuwa fundi TV ni bonge la ishu,unakuta fundi ana magari,,,,ni enzi hizzooo,katika utoto wangu,nilishuhudia hayo
 
enzi zetu.....TV inakaa chumbani kwa baba mpaka arudi ndo muombe itolewe,tena mnaangalia kipindi cha katuni kimoja alafu basi inarudishwa na stendi yake ya matairi,glassi zingine marufuku kugusa mpaka mgeni aje,album za picha kedekede kwenye kabati,ila bonge la ufunguo,watoto wanazionaga tu,ila ni marufuku kugusa....vitambaa vya sebuleni sasa wakati wa kuangalia Tiivii,ole wako upangarue,utakiona cha moto,kuondoa ugomvi bora tu ukae chini,kula kwenye kochi ni marufuku,ila baba anaruhusiwa.....baada ya kuangalia VIDEO mnaifunika VIDEO vizuuurrii,isiingie vumbi na vile vitambaa vya kufuma....na baba ndo anakaa na remote control,imefunikwa na ma-nylon kibao ili isizeeke.....akija mgeni nyumbani anafundishwa jinsi ya kuwasha na kuzima Tivii na namna ya kuweka mkanda asije akaugeuza.......kipindi hicho kuwa fundi TV ni bonge la ishu,unakuta fundi ana magari,,,,ni enzi hizzooo,katika utoto wangu,nilishuhudia hayo
mkuu we mdogo kiasi,.cartoon za ctn na itv mi nishamaliza la saba(niko form one),kwa hiyo nilivyokuwa mdogo hakukuwa na tv
 
Kuna jamaa alinunua friji lamtumba kariakoo (sio zamani), sasa akawa hataki mkewe na watoto walitumie wakati yeye hayupo. Na kwa kuwa friji lile la mtumba halikuwa na lock basi akamwita fundi amtengenezee lock ili awe analifunga na kulifungua kwa matakwa yake. Aisee wakati jamaa anatoboa si akatoboa paipu ya gesi. Nilipotaka kujua kuna nini hasa kinatunzwa humo nikakutana na sijui nyanya 2, na maji ya kuchemsha kwenye chupa za uhai. Sasa huu sijui tuuite ukomunisti au mawazo ya kimaskini!
 
Lakini wakuu tukubali kuwa yapo mazingira mtu unaweza kulazimika kufanya kitu kinachofanana na hiki (say kwa kuweka password etc).

TV zinaweza kukuharibia watoto (kutwa ni kutizama katuni au movies/programmes zisizofaa kwa watoto) na hata wadada wa nyumbani (baadhi) wanaweza kushindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo na badala yake kutwa wapo kwa TV/movies. Wengine ni waaribifu - deck, remote etc! Yamenitokea haya na kwa kweli yanakera mno. I have stopped paying for DSTv, nikiona haijawa effective nitaondoa TV sebuleni kwangu na kuifungia chumbani kabisa!
 
mkuu we mdogo kiasi,.cartoon za ctn na itv mi nishamaliza la saba(niko form one),kwa hiyo nilivyokuwa mdogo hakukuwa na tv

kila mtu ana zamani yake mwenyewe......zamani ya nzi ni jana,,,,zamani ya kobe ni miaka 100,zamani yangu na yako labda tofauti.....
 
Lakini wakuu tukubali kuwa yapo mazingira mtu unaweza kulazimika kufanya kitu kinachofanana na hiki (say kwa kuweka password etc).

TV zinaweza kukuharibia watoto (kutwa ni kutizama katuni au movies/programmes zisizofaa kwa watoto) na hata wadada wa nyumbani (baadhi) wanaweza kushindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo na badala yake kutwa wapo kwa TV/movies. Wengine ni waaribifu - deck, remote etc! Yamenitokea haya na kwa kweli yanakera mno. I have stopped paying for DSTv, nikiona haijawa effective nitaondoa TV sebuleni kwangu na kuifungia chumbani kabisa!

mkuu hiyo siyo solution kwa dunia ya sasa,akikosa apo nyumban ataangalia kwa jirani,waache watoto waenjoy mambo ya kawaida sana ayo
 
  • Thanks
Reactions: SMU
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom