Waandishi Walioripoti mkutano wa Lissu wahojiwa na Vyombo vya Dola!

004520c70ff6281fb1b1722a50dd836c.jpg
Lissu jana amekamatwa mara ya nane (8) kuanzia June mwaka jana na hajawahi kupatikana na Hatia, Ubunifu ni Muhimu sana katika jambo lolote..

======

Dar es Salaam. Baadhi ya waandishi wa habari walioripoti mkutano wa Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu, uliofanyika Jumatatu ya wiki hii wamehojiwa na polisi.

Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, (TLS) alifanya mkutano huo Jumatatu wiki hii ambapo pamoja na mambo mengine alilaani kukamatwa kwa wanachama wa Chadema.

Leo, Ijumaa, Julai 21, Mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima, Ibrahim Yamola amehojiwa na watu waliojitambulisha kuwa ni polisi ambao walifika katika ofisi za gazeti hilo.

“Walitaka nifike Polisi Makao Makuu lakini tukakubaliana watakuja hapa ofisini kwetu asubuhi, wamekuja na wamenihoji kuhusu mkutano huo,” amesema.

Yamola amesema watu hao walimuhoji mazingira ya mkutano huo, maneno aliyoyatamka Lissu na namna walivyoichapisha habari hiyo siku ya pili.

Inaelezwa kuwa mwandishi mwingine wa gazeti la Mtanzania, Aziza Masoud naye anatarajia kuhojiwa baadaye leo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli !! Yaani kweeeli kabisa !!!,yaani elimu yenu yote,ya kipolisi,mashaada yote mliyo nayo,
Mnapoteza rasilimali za nchi kuhoji waandishi wa habari!! Seriously!! Kama kuna intelligencia inatafutwa,kuna mbinu nyingi sana za kisayansi,
Suala LA Tundu Lisu halikupaswa kufika hapa jamani,
Hili ni suala ambalo lingetatuliwa na Press ya ikulu,au hata mwandishi mmoja was TBC,angetoa makala inayotolea maelezo kile ambacho Tundu lisu kaongea,huyu alikuwa wa kupuuzwa tu,
Kwani serikali haina wanasheria,aina waandishi wa habari,vitengo vya propaganda,ndio kazi yao hii,
Ishu za kipolisi zipo Kibiti,jiji LA dar limejaa vibaka kila kona,hapo kawe,mbele ya shule ya feza,kuna njia,ikifika SAA 12:30,hupiti,sema kama unataka ukutane na Muumba,
Chonde chonde Polisi,msipoteze rasilimali za nchi bile kufatilia mambo ya kisiasa,
Hivi mnajua vibaka wa dar,wameamia Dodoma,kuna mitaa Dodoma,wanawake wanapolwa Mali zao mchana kweupe,na wezi wanavamia na kuiba mchana,pls we need security not fuckups
 
Sitaki kuamini kama tumefika hapa,ivi raisi wetu anayajua haya? Au watendaji wake ndio hujiamulia kufanya haya? Nakama raisi wetu anayajua haya nikweli hajui umuhimu wa democrasia na uhuru wakujieleza?? Sitaki kuamini kama magufuri anaogopa kukosolewa

Sent using Jamii Forums mobile app

Hivi upo duniani ndugu, achilia mbali kuwepo Tanzania.
 
Mkuu wa kaya aliwahi kusema kuwa vyombo vya habari haviko huru. Sasa usemi wake umeanza kujidhihirisha dhahiri.
 
Kosa lao kubwa ni kuvammia chumba cha mahakama kukiteka nyara na kukigeuza chumba cha press conference bila ridhaa ya mahakama
Duh! Biblia inasema usiabudu miungu mingine kumbe ilikuwa inamaanisha! Sikujua kama kuna miungu mingi kiasi hiki hapa duniani.
 


=========================================
Dar es Salaam. Baadhi ya waandishi wa habari walioripoti mkutano wa Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu, uliofanyika Jumatatu ya wiki hii wamehojiwa na polisi.

Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, (TLS) alifanya mkutano huo Jumatatu wiki hii ambapo pamoja na mambo mengine alilaani kukamatwa kwa wanachama wa Chadema.

Leo, Ijumaa, Julai 21, Mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima, Ibrahim Yamola amehojiwa na watu waliojitambulisha kuwa ni polisi ambao walifika katika ofisi za gazeti hilo.

“Walitaka nifike Polisi Makao Makuu lakini tukakubaliana watakuja hapa ofisini kwetu asubuhi, wamekuja na wamenihoji kuhusu mkutano huo,” amesema.

Yamola amesema watu hao walimuhoji mazingira ya mkutano huo, maneno aliyoyatamka Lissu na namna walivyoichapisha habari hiyo siku ya pili.

Inaelezwa kuwa mwandishi mwingine wa gazeti la Mtanzania, Aziza Masoud naye anatarajia kuhojiwa baadaye leo.

Kama ilivyisemwa,huo nao ni upuuzi mwingine. Unamhoji vipi Mwandishi ambaye alikuwa ktk kutekeleza majukumu yake!?
 
Uhuru wa kujieleza unaruhusiwa lkn sio Uhuru wa kutukana kukejeli na kutoa maneno ya kuudhi dhidi ya raia na serikali yake lkn kuchochea wananchi waichukie serikali yao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Katika mahojiano yale matusi na kejeli yanasomekaje?! Na nani huyo katukanwa?!

Dunia tuliyonayo leo viongozi siyo miunguwatu bali watumishi wa watu, kama Lumumba wanavyojaribu kutuaminisha

Cairo's
 
kuna sababu kwa wagombea uongozi wapimwe akili kwanza na kuchunguzwa juu ya mahusiano yao ndani ya familia zao..
kiongozi bora huanza kwenye familia yake..

Sent using Jamii Forums mobile app
Nakupa 100% kwa hili,kwa bahati maya ninafahamu maisha(hearsay za jirani) kabla hajawa mkulu wa kaya.Kwakuwa nilimuamini dada mleta story ambaye alikuwa 'shost' wa huyu mama namba moko wa sasa, hakuna ninachoshangaa.Ni kama tu mkulu anapigia mstari majibu yangu.Believe it or not,the worse is yet come.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kipengele cha kupimwa akili kabla kuchukua form kiwe no 1........pia kama kuna kipimo ch busara pia!!
 
Ninamkumbuka mzee kingunge alisema huyu alistahili kuwa mnyampala wa Barabara na si vinginevyo sasa yametimia
 
Mmebaki kupiga kelele mtandaoni. Mnampa kichwa huyo Lisu halafu akiswekwa selo hata uji tu hamumpelekei.
Jidanganye tu hizi hizi kelele ndo zinazidi kuwakosesha raha halafu mbaya zaidi wanazidi kuboronga hakuna watu wanaozaliwa na ujasiri tu wa kupinga utawala... dhuluma na uonevu wa wazi ukizidi hadi mbuzi wanaweza kuwa simba...

MWENYEZI MUNGU NI mkubwa sana...
Nimesoma sehemu kuna Mgombe urais wa Brazil TANCREDO NEVES aliwahi kudai akipata kura 500,000 hakuna anayeweza kumzuia kuwa Rais hata MWENYEZI MUNGU, alipata kweli hizo kura na akashinda uchaguzi lakini kabla ya kuapishwa akafa....

Sasa kuna wanosisitiza sana kuwa Atabaki tu mpaka 2025 au mara abaki milele... MWENYEZI MUNGU Anaweza kumtoa madarakani kabla hata ya uchaguzi utakaokuja (2020) tena bila hata ya kifo...
 
Back
Top Bottom