Bluray
JF-Expert Member
- Mar 25, 2008
- 3,449
- 127
Tunalaumu wasomi bila kutafakari mfumo uliozaa wasomi hao. Unatarajia wasomi wa aina gani wakati elimu yetu ya sasa ni kukariri, kusoma katika mazingira duni na kujali wingi wa wanafunzi bila kujali ubora wa elimu? Kama tusipobadili mfumo huu tutaendelea kuwa na waandishi na wasomi wanaoganga njaa kwani mfumo umedumaza akili na uwezo wetu wa kufikiri. Hata waliosomea nje, wakirudi wanamezwa na mfumo nao wanaanza kukimbizana na shilingi bila kuwa na ubunifu na mikakati yoyote ya kuiendeleza nchi.
In the land of the blind, the one eyed is king. Wasomi wetu ingawa unadai wamesomea katika mfumo wa "kukariri", lakini wengi wamepata bahati ya kusomea nje na kuona wenzetu wanavyofanya kazi. Huwezi kusema hawajui chochote kuhusu umuhimu wa biographies/ critical analysis za nchi inavyoendeshwa, huwezi kusema hawajui, sema labda hawaoni kama priority au wanaogopa.