GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,277
- 6,673
Nimeshuhudia baadhi ya waandishi wa habari wanaokuja wilaya ya Tandahimba wakilipwa Posho na Halmashauri ya Wilaya hiyo. Tena hupewa posho zaidi pale wanapotaka kubalance story ambazo zinawagusa watendaji wa Halmashauri. Tumeshuhudia ukandamizaji mkubwa kwa wakulima wa korosho ambao wameanzisha Umoja wao, katika kipindi hicho kulikuwa na utitiri wa waandishi ambao walikuwa wanazunguka huku na huko na kuchukua posho kila walikoenda. Walipoenda kwenye Umoja wa wakulima walipewa pesa na walipoenda Halmashauri pia walilipwa. Pia katika kumbukumbu zangu inaonyesha kuwa mwandishi mmoja anayeripoti katika vyombo vinavyomilikiwa na ndugu R. Mengi anaongoza kwa kupewa posho na Halmashauri. (kaanza siku nyingi)
Naomba ufafanuzi hapa, hii ni Takrima au kitu gani? Na mnaruhusiwa kufanya hivyo?
Kwanini Halmashauri itoe Posho kwa waandishi?
Naomba ufafanuzi hapa, hii ni Takrima au kitu gani? Na mnaruhusiwa kufanya hivyo?
Kwanini Halmashauri itoe Posho kwa waandishi?