Waandishi wa Habari Tanzania wamekosa Uzalendo

Barubaru

JF-Expert Member
Apr 6, 2009
7,161
2,323
Kwa takriban siku mbili nipo Tanzania na napata fursa kubwa kusoma magazeti ya nchi hii na pia kusikiliza radio na kuona TV mbalimbali za Tanzania hususan Bara naona kweli Maadili ya Uandishi wa Habari sio tu wa magazeti lakin pia hata Radio na TV umekosa uzalendo.

Waandishi wengi sana wamejikita katika USHABIKI na kupenda kufanya BIASHARA ya habari zao na kusahau kabisa miiko na Sharia na kaanun za Uandishi wa habari. Tukumbuke mwiko mkubwa kwa mwandishi yoyote wa habari ni USHABIKI. Mwandishi anatakiwa kutoa ripoti ya kile anachokiona bila kuongeza jambo lake lolote na kama anataka kuripoti tukio ni lazima ahakikishe anatenda haki kwa kila upande kwa kupata maoni na rai zao. Kwani siku zote habari inakuwa na sehemu mbili (mlalamika na mlalamikiwa).

Inatakiwa ifahamike kuwa kazi ya Mwandishi wa habari ni KUELIMISHA JAMII, KUBURUDISHA JAMII na Kuijuza au KUIPASHA HABARI JAMII. Kwa mantiki hii utaona Kalamu ya mwandishi ni sumu au bomu baya sana kuliko lile la nyuklia. Mwandishi siku zote anatakiwa kutumia busara sana katika kazi zake ikiwemo na kuweka uzalendo wa nchi yake mbele kwa kutoa habari zilizo sahihi zisizo na hata chembe ya ushabiki kwa jamii kwani jamii inataraji kupata habari zilizo sahihi na zisizo na upendeleo wa upande wowote.

Ukipitia Sharia za Tanzania inaozungumzia Uhuru wa maoni sharia namba 15 ibara ya 6 ya mwaka 1984, kifungu cha 18

.-(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru
kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta,
chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wamawasiliano yake kutoingiliwa kati.(2) Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusumatukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimukwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala
muhimu kwa jamii.
Kwa hicho nilichobainisha Juu utaona karibu kila chombo cha habari tanzania kimekosa uzalendo. Chukulia habari ndogo tu jinsi wanavyoripoti mambo kutoka Bungeni. Waandishi hawa hawana umakini na hawajui kuwa kuna sharia maalum za uandishi wa habari za Bunge na Mahakama. Wao wanajaza ushabiki miongoni mwa jamii za Kitanzania na kuigombanisha Serikali na raia wake kwa manufaa yao ya kibiashara na kisiasa na kusahau Amani ya nchi hiyo.

Jana nilikuwa napitia habari za Kiongozi wa madaktari Dr Mkopi kufikishwa mahakama ya kisutu. Utaona kila gazeti limeripoti linavyofahamu na kwa mtu makini kama atasoma unaona kabisa waandishi hawa wana nia kubwa ya kuigombanisha Serikali na Madaktari bila kufahamu kuwa watakao umia ni wananchi. Wameshindwa kabisa kujua kuwa Dr Mkopi ameshitakiwa na mahakama kwa kudharau amri halali ya mahakama na sio Serikali.

Ukisoma kwa kina wanashindwa kabisa kuofautisha Mahakama, Serikali na Bunge. Kwao wao kila kitu ni sawa. Nasikitika sana kuona Baraza la Habari Tz limekaa kimya na hata wizara ya habari Tz zimekaa kimya bila kukemea haya. Kwa tunaamini kuwa msipoziba Ufa basi kifo kitawaumbua.

nawasihi muwe wazalendo kwa nchi yenu na ondoeni kabisa ushabiki wa Siasa au kidini kwani mnaiangamiza nchi yenu.


Haya ni maoni yangu kwenu
Dr Hamza Yousuf Al naamaniy (Barubaru)

Mwanza Tarabu (Muta) na Nkurukumbi

Omwana nikalikwela,ina shani ommano,
Lutiluti nanda maiza, omoyo tigindi munda.
Owenfundo nyamilinga, lugayo olwo nakubone,
ijamawe kinyalyana, lugayo ongalule moyo

Nkurukumbi 2

hay
 
Rais nae akamatwe na kufikishwa mahakamani kwa kuzungumzia jambo ambalo lipo mahakamani.Mahakama ilikuwa wapi muda wote kumkamata dk.Mkopi?
 
Barubaru


Uongozi bora ni Ulikuwa huu hapa CHINI; Walikuwa hawagombanii MALI; Walikuwa hawagombanii MADARAKA na

kutafuta NJIA bora za kupeleka fedha za Nchi Nje; Hawakuuza Maliasili ya Nchi kwa Hasara ya Nchi bali kwa faida

Yao Wenyewe; Hawa Viongozi wetu wa Sasa hawajali Maendeleo ya Nchi wanajali Maendeleo yao Wenyewe

Tangu lini Umeiona Nchi ina Matatizo ya UMEME wakati ina kila kitu cha kuweza kujikwamua na tatizo hilo?

Serikali iliondoa Umiliki wa Mishahara baada ya AZIMIO la ZANZIBAR; nchi sio ya KIJAMAA tena kwahiyo ni fursa

Kama Wafanyakazi hawaridhiki kugoma; Serikali inapaswa ku-float SALARIES za wafanyakazi wake na sio ku-control

as a CAPITALIST NATION; CCM na Serikali yake SIO A SOCIALIST GVT any longer after AZIMIO LA ZANZIBAR

imekumbatia MATAJIRI; ndio wanokiendesha hicho chama... ni TOFAUTI NA HII PICHA...




534463_389871837741865_208906763_n.jpg

BARAZA LA KWANZA LA MAWAZIRI LA TANGANYIKA 1961.. Ndugu Job lusinde (serikali za mitaa), ndugu Mfaume Kawawa (waziri asiye na wizara maalumu), ndugu Nsilo Swai (biashara na viwanda), ndg Oscar Kambona (elimu), ndg Tewa S. Tewa (ardh na upimaji), ndg Dereck Bryceson (Afya na kazi), ndg Paul Bomani (kilimo), ndg Chief Abdallah Fundikira (sheria), ndg sir Ernest Vassey (Fedha), ndg Amiri Jamal (mawasiliano) na ndg Clement G. Kahama (mambo ya ndani). Watanzania daima tutawakumbuka na kuwaenzi kwa misingi imara mulioijengea taifa letu
 
Last edited by a moderator:
Mkuu nakurekebisha sio sharia Tanzania inaongozwa na SHERIA hivyo ni vitu viwili tofauti.

Pili mkuu serikali imeshindwa kudhibiti mgomo imeishia kupanga mauaji ya Dr Ulimboka huo ni udhaifu mkubwa sana upande wa serikali.

Vyombo vya habari vinafanya kazi zao vizuri tu kuripoti kama Mwanahalisi, Mwananchi, Channel 10. Kuna vyombo vya propaganda vinavyoshabikia serikali na mauaji yake kama Clouds FM, Clouds TV.
 
Mkuu Barubaru, waandishi hawa wangeandika kuwa serikali ya Tanzania inaendeshwa kwa mfumo kristo na kuwaonea, kuwatenga na kuwanyanyasa waislam, waandishi hao wangekuwa wamekosa uzalendo kwa taifa lao?
 
Hawawezi kutofautisha Bunge, Mahakama na Serikali km ulivyoeleza kwa sababu ya mambo yanavyoendeshwa sasa hivi.

Mfano; jaribu kurejea mijadala bungeni ambapo wabunge hasa wa CCM wanapogeuka kuwa wasemaji wa serikali na hukumu tata za Mahakama mfano kesi ya mgombea binafsi maamuzi ambayo yanaonekana kulalia upande wa serikali. Kwa misingi hiyo mtu hawezi kuona tofauti ya mihimili hii mitatu kiuntendaji.
 
Mkuu Barubaru, waandishi hawa wangeandika kuwa serikali ya Tanzania inaendeshwa kwa mfumo kristo na kuwaonea, kuwatenga na kuwanyanyasa waislam, waandishi hao wangekuwa wamekosa uzalendo kwa taifa lao?

Gwalienzi.

Ahali yangu suala hili nimeliandika kitaaluma zaidi na nimejikita zaidi katika MAADILI YA UANDISHI na sipo kwenye ushabiki wa siasa wala Imaan.

Naomba unisome kwa uzuri sana between line kisha leta hoja yako. Kumbuka kuwa Uandishi wa habari ni taaluma kama taaluma nyingine na inaongozwa na maadili na kanuni zake.

 
Bwanamdogo

Hairuhusiwi kabisa Mwandishi kuandika habari ya kitu asichokijua. Kila mwandishi anatakiwa kujua kile anachokiandika na anamwandikia nani. kama nilivyodokeza huko juu kuwa Kila mwandishi anatakiwa aweze kutofautisha Shughuli za Bunge, Serikali na Mahakama .

Inampasa ajue kazi za Bunge ni kutunga sharia, Kazi za mahakama ni kutafsiri sharia zilizotungwa na Bunge na Kazi za Serikali ni kusimamia na kutekeleza sharia zilizotungwa na Bunge.

na kwa mwandishi anatakiwa kujua namna ya kuandika habari za mihimili hii mikuu mitatu. ndio maana utana kuna waandishi maalum waliosomea kuandika habari za shughuli za Bunge, Na wengina habari za shughuli za mahakama na za Serikali.

Kumbuka kuwa Uandishi ni taaluma makini sana kwani kwenda kinyume na maadili ni kuihadaa jamii na kuleta mtafaruku mkubwa katika jamii.

 
Last edited by a moderator:
Gwalienzi.

Ahali yangu suala hili nimeliandika kitaaluma zaidi na nimejikita zaidi katika MAADILI YA UANDISHI na sipo kwenye ushabiki wa siasa wala Imaan.

Naomba unisome kwa uzuri sana between line kisha leta hoja yako. Kumbuka kuwa Uandishi wa habari ni taaluma kama taaluma nyingine na inaongozwa na maadili na kanuni zake.

Mkuu wangu Barubaru, kwahiyo unatangaza wazi bila kuumauma maneno kuwa madai yako ya muda mrefu kuwa Tanzania inaongozwa na mfumo kristo unaowaonea na kuwakandamiza waislam ni USHABIKI WA KIIMANI NA KISIASA!
 
Mkuu wangu Barubaru, kwahiyo unatangaza wazi bila kuumauma maneno kuwa madai yako ya muda mrefu kuwa Tanzania inaongozwa na mfumo kristo unaowaonea na kuwakandamiza waislam ni USHABIKI WA KIIMANI NA KISIASA!
Umemuuliza swali gumu sana.
Inabidi arudi chuo kusoma ndipo aweze kulijibu.
I give u a like!
 
..wale wa gazeti la an-nuur na redio imaan ndiyo wamesheheni maadili,uzalendo, na weledi wa taaluma ya uandishi??je, hawachonganishi serikali na wananchi wake? je, hawachonganishi imani moja dhidi ya nyingine??
 
..wale wa gazeti la an-nuur na redio imaan ndiyo wamesheheni maadili,uzalendo, na weledi wa taaluma ya uandishi??je, hawachonganishi serikali na wananchi wake? je, hawachonganishi imani moja dhidi ya nyingine??
Maswali kama haya huwa magumu sana kwa Barubaru. Hawezi kuja kujibu. Ni magumu sanaaaaaa
 
Jana nilikuwa napitia habari za Kiongozi wa madaktari Dr Mkopi kufikishwa mahakama ya kisutu. Utaona kila gazeti limeripoti linavyofahamu na kwa mtu makini kama atasoma unaona kabisa waandishi hawa wana nia kubwa ya kuigombanisha Serikali na Madaktari bila kufahamu kuwa watakao umia ni wananchi. Wameshindwa kabisa kujua kuwa Dr Mkopi ameshitakiwa na mahakama kwa kudharau amri halali ya mahakama na sio Serikali.

Nikukumbushe tu, hapo penye blue, mahakama huwa haishtaki, bali husikiliza na kuamua mashauri mbali mbali. Katika sheria (au sharia kama unavyoita) mashtaka huletwa na Director of Public Prosecution ambayo ni sehemu ya serikali (the executive) ambayo serikali hiyo ni mhimili mmoja wapo wa dola (the state), mihimili mingine ni mahakama (judiciary) na bunge.

Hiyo ni elementary civic knowledge bwana Barubaru. next time usiandike makala ukiwa na passion otherwise wewe utaonekana kituko. Na pia tafsiri kwamba habari imeandikwa kishabiki inatokana na mtazamo wako pia, ingawa inaweza kuwa kweli kwamba waandish wanakosea.
 
BwanaMdogo.

Hairuhusiwi kabisa Mwandishi kuandika habari ya kitu asichokijua. Kila mwandishi anatakiwa kujua kile anachokiandika na anamwandikia nani. kama nilivyodokeza huko juu kuwa Kila mwandishi anatakiwa aweze kutofautisha Shughuli za Bunge, Serikali na Mahakama .

Inampasa ajue kazi za Bunge ni kutunga sharia, Kazi za mahakama ni kutafsiri sharia zilizotungwa na Bunge na Kazi za Serikali ni kusimamia na kutekeleza sharia zilizotungwa na Bunge.

na kwa mwandishi anatakiwa kujua namna ya kuandika habari za mihimili hii mikuu mitatu. ndio maana utana kuna waandishi maalum waliosomea kuandika habari za shughuli za Bunge, Na wengina habari za shughuli za mahakama na za Serikali.

Kumbuka kuwa Uandishi ni taaluma makini sana kwani kwenda kinyume na maadili ni kuihadaa jamii na kuleta mtafaruku mkubwa katika jamii.


Wewe mwenyewe mwongo, kwani tayari katika bandiko lako ushatudanganya kuwa Dr. Mkopi kashtakiwa na mahakama ilhali mahakama huwa inasikiliza tu na kutoa maamuzi! Hata Paschal Mayalla msomi wa sheria na mwandishi wa habari ameshindwa kuona kosa lako katika bandiko lako!
 
habari inajichanganya,unaonekana unaifahamu kijujuu sana dhana nzima ya separation of power,kwa taarifa yako tu kazi ya kuwafikisha watu kwenye mikono ya sheria si la mahakama na zaidi ya yote hiyo dhana kwa hapa tanzania haipo.

Kwa mfano kitu kidogo tu,mbuge anapolazimishwa kwenye cocus ya chama aikubali hoja iliyoletwa na serikali utasema tuna seperation of power hapo?.

Hivyo basi ili waandishi wawe na maadili inabidi kwanza wayaone maadili katika wale waliopewa dhamana ya kusimamia maadili ya uandishi.

Wasalimie Oman
 
Ibambasi

Inakubidi upitie sharia zenu katika katiba yenu imeweka mambo wazi kabisa kuwa mwenye haki ya Kushitaki ni JMTz kupitia vyombo vyake DPP. Hivyo hata ukikataa kutii amri ya mahakama basi chombo cha Serikali chenye mamlaka hayo.

Kumbuka hata Mbowe alipokiuka amri za mahakama kule Arusha alikamatwa na Serikali kupitia vyombo vyake na kupelekwa mahakamani.

Kumbukeni kazi ya Serikali iliyobainisha ni Kulinda na kutetea sharia zilizotungwa na Bunge. Na unatakiwa ukumbuke kuwa Mahakama na Bunge wana kaanun zao zinavyoviongoza na ukienda kinyume navyo basi lazima utaingia matatani.

nafikiri nimekujibu suala lako.

 
Last edited by a moderator:
Hivyo basi ili waandishi wawe na maadili inabidi kwanza wayaone maadili katika wale waliopewa dhamana ya kusimamia maadili ya uandishi.
Hapa unanikumbusha kuwa kwa sababu mwenzangu kaiba lakin hajakamatwa na kufikishwa mahakamani basi na wewe unaiba. sasa ukifikishwa mahakamani na kufungwa unalalama.

Kumbuka kuwa kutojua sharia sio sababu ya kuachiwa. Sharia ni msumeno na lazima ufuate pasi na shuruti kwani zimetungwa na Bunge lanu lenye wawakilishi wenu kwa pesa nyingi. Na kumbuka Tanzania inaongozwa kwa Rules of law.

Nashukuru sana kwa sasa nipo hapa kamachumu nimekuja kwenye harusi ya Mtoto wetu na nitakuwepo Tz mpaka taarih 25 July 2012.

Tunainjoy na Nsenene na tunacheza Nkurukumbu usiku huu na tunatumbuizwa na Mukrim hapa kamachumu Inn
 
Mkuu wangu Barubaru, kwahiyo unatangaza wazi bila kuumauma maneno kuwa madai yako ya muda mrefu kuwa Tanzania inaongozwa na mfumo kristo unaowaonea na kuwakandamiza waislam ni USHABIKI WA KIIMANI NA KISIASA!
Gwalienzi.

Ni wapi mimi nimesema au kuandika kuwa Tz inaongozwa kama ulivyonena. naomba unibainishie wazi na kama utapata quote nitafurahi sana.

Lakin vile vile kama mwandishi na anaedai hayo kama ataleta ushahidi kamili na vielelezo vyake na kisha kuweka katika makala yake basi ni sahihi. Lakin vile vile mtu mwingine ana haki kamili ya kujibu tuhuma hizo kupitia chombo hicho hicho na kuweka mambo sawia.

waandishi makini siku zote wanatoa nafasi kwa pande zote mbili ya mwandishi wa kudai tuhuma hizo na yule anayepinga wote wanakuwa na haki sawa katika kutoa habari.

Kumbuka sharia zenu zinaweka mambo sawa kuwa wananchi wanahaki kamili ya kupata habari kamili na sahihi.

nakuomba ondoa ushabiki katika TAALUMA YA HABARI.

 
Wewe mwenyewe mwongo, kwani tayari katika bandiko lako ushatudanganya kuwa Dr. Mkopi kashtakiwa na mahakama ilhali mahakama huwa inasikiliza tu na kutoa maamuzi! Hata Paschal Mayalla msomi wa sheria na mwandishi wa habari ameshindwa kuona kosa lako katika bandiko lako!

Ibambasi,

Kosa lake ni kukiuka amri ya mahakama na ndilo lililomfikisha mahakamani. Kumbuka kuwa mahakama ni kama Bunge zote zinaendeshwa na taratibu na kaanun zake.

lakin kumbuka kwa mujibu wa Katiba yenu mwenye haki ya kumfikisha mtu mahakamani ni Serikali kupitia taasisi zake kama DPP. Kazi ya Serikali kwa mujibu wa Rules of law imebainishwa wazi kuwa kazi ya Serikali ni kulinda sharia na kutetea sharia.

kama una ziada basi bismillah
 
Back
Top Bottom