UZUSHI Waandishi wa Habari Kilimanjaro Wafanya utapeli wa pesa kwa kisingizio cha gharama za kurusha habari

Baada ya tathmini, tumebaini kuwa taarifa hii ni ya uzushi
Kumezuka tabia ya waandishi wa habari mkoani Kilimanjaro kujihusisha na utapeli kwa kuchukua fedha za watu (wadau) wakidai ni gharama za kutuma habari lakini kinachotokea ni wizi mtupu.

IMG_7117.jpeg


Juzi mama mmoja wa Uru Mjini wilaya ya Moshi Vijijini ametoa Tsh. laki 4 kwa waandishi wa habari wanne ili waripoti tukio la mtoto wake mwenye Utindio wa ubongo kubakwa na kupewa ujauzito, mpaka sasa waandhi hao watatu wa TV na mmoja wa gazeti wameshindwa kutoa habari yake.

Huu ni utapeli wa aina yake, ni jukumu la viongozi wa Press Club kilimanjaro kuchukua hatua dhidi ya waandishi hawa ambao ni wanachama wenu na hata kama si wanachama wenu wanachafua tasnia ya habari.

Ni hayo tu kwa leo, wasiporudisha tunawaanika chap ili vyombo vya vichukue hatua, ushahidi upo na mhanga yupo.
 
Tunachokijua
Baada ya kutokea kwa dokezo hili JamiiForums imefuatilia tukio hili Kwa kupiga simu kwa wahusika ili kubaini ukweli wake.

Kwanza, Waandishi wa habari, Mama wa mtoto na mtoto wamekiri kutokea tukio la kubakwa kwa mtoto aliyekuwa anasoma ambaye kapata ujauzito. Inaelezwa taarifa hizo hazijatolewa kwenye vyombo vya habari hadi sasa kwasababu anayetakiwa alizungumzie na kuweka mizania wa hiyo taarifa ni RPC wa Kilimanjaro ambaye bado anasubiriwa RPC lizungumzie kwa sababu kesi ipo bado polisi na Waandishi wanatakiwa "wabance Story".

Jamiiforums imemhoji mama wa mtoto huyo (Jina tumelihifadhi) ili kujua kama alitoa kiasi cha laki nne ili Waandishi waripoti tukio la kubakwa kwa mwanaye amekana na kusema hana uwezo wa kutoa hiyo fedha sababu anafanya biashara ndogo ndogo. Mama huyo anaeleza kuwa yeye ni mfanyabiashara ya matunda na kipato chake ni kidogo sana hawezi kumudu kulipia laki nne kama taarifa zinavyoeleza.

Naye, mtoto wa Kiume wa Mama huyu ambaye ni kaka wa huyo anayeelezwa kubakwa amekanusha suala la mama yake kutoa laki nne kwa Waandishi wa habari. Huyu Kaka wa Mtoto aliyebakwa ndiye alitoa taarifa kwa wanahabari ili wafuatilie kesi ya kubakwa kwa mdogo wake sababu haipelekwi Mahakamani.

Aidha, Kiongozi wa Club ya waaandishi wa habari wa mkoa huo amekana na kusikitishwa na habari zinazodai kuwa waandishi hao wa Mkoa huo wamelipwa pesa ili watoe hizo habari kitu ambacho si kweli.
Kumezuka tabia ya waandishi wa habari mkoani Kilimanjaro kujihusisha na utaperi kwa kuchukua fedha za watu(wadau) wakidai ni gharma za kutuma habari lakini kinachotokea ni wizi mtupu.
Weka jina la huyo mwanahabari na chombo anachofanyia kazi sio kuchafua watu wote,

USSR
 
Baada ya jana kufichua kitendo cha waandishi wa habari wanne mkoani Kilimanjaro kudaiwa kumtaperi fedha mama mmoja ambaye mwanaye mwenye mtindio wa Ubongo amebakwa na kupata ujauzito,mjadala mkali unaendelea kwenye group la wanahabri Kilimanjaro wengi wakitaka waliofanya kitendo hicho watajwe na hatua zichukuliwe.
Wengi wanasema mama huyo ambaye ni muuza maparachichi kwenye viunga vya jengo la Bodi ya kahawa,n mwanamke asiyekuwa na uwezo kifedha kiasi cha kugharamia habari ya mwanaye kubakwa na ilistahili wanahari hao kulichukulia kama trukio la kijamii .

"mliochukua hela nisaidieni kujua huyu mama anakaa wapi,wapo ambao tumejitolea kwenda kufnbaykazi bure kabisa",amechangia mwandishi mmoja jina kapuni na kungwa mkono na wenzake huku wanaodaiwsak ushiriki dhambi hiyo wakifura kama wamedungwa sindano za ganzi.

Mwanafuzni huiyo aliyekuiwa akisoma shule ya mazoezi Pantandi wilaya ya Arumeru mkoani Arusha,alikatisdha masomo kwa kufukuzwa shule basa ya kubvainika kuwa na ujauzito unaotokana na kubakwa na kijana mmoja katika kijiji cha Uru Mnini wilaya ya Moshi Vijijijni .

Hadi sasa mtuhumiwa huyo hajafikishwa kweney mkono wa sheria huku mama mzazi wa mtoto huyo akilalamikia askari wakituo cha polisi majengo kutomfikisha mahakamani mtuhumiwa.

Waandishi wengi wanaoendnelea kuchangia kuhusu tuhuma hizo wanataka viongozi wa klabu ya waandishi wa habari mkoani Kilimanjaro kuchukua hatua za haraka kwani tukio hilo linawachafua wanahabari wote na si hao waliofanya dhambi hiyo pekee.
"Hivi baadhi yetu waandishi ni tumekosa utu au,kweli unachukua laki nne ya mama mjasirimali muuza parachichi,kweli...waliofanya dhambi hii hhaitawacha salama",amechangia mwandishi mwingine.

Je nini kinaedelea juu ya sakata hilo,kaa mkao wa kula mambo mazuri yanakuja
 
wewe kaa kimya usilolijua ni sawa na usiku wa giza,tuna miiko ya kimaadili katika kila tasnia siyo kama wewe unvyotaka iwe
 
Kumezuka tabia ya waandishi wa habari mkoani Kilimanjaro kujihusisha na utapeli kwa kuchukua fedha za watu (wadau) wakidai ni gharama za kutuma habari lakini kinachotokea ni wizi mtupu.

View attachment 2616519

Juzi mama mmoja wa Uru Mjini wilaya ya Moshi Vijijini ametoa Tsh. laki 4 kwa waandishi wa habari wanne ili waripoti tukio la mtoto wake mwenye Utindio wa ubongo kubakwa na kupewa ujauzito, mpaka sasa waandhi hao watatu wa TV na mmoja wa gazeti wameshindwa kutoa habari yake.

Huu ni utapeli wa aina yake, ni jukumu la viongozi wa Press Club kilimanjaro kuchukua hatua dhidi ya waandishi hawa ambao ni wanachama wenu na hata kama si wanachama wenu wanachafua tasnia ya habari.

Ni hayo tu kwa leo, wasiporudisha tunawaanika chap ili vyombo vya vichukue hatua, ushahidi upo na mhanga yupo.
Kumbe uzushi.
 
Bado elimu inahitajika kwenye jamii wajanja ni wachache ila wajinga ni wengii
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom