Waandishi wa habari Dar walia na kampuni ya HQ kuwapa taulo zilizokwisha muda wa matumizi

Tuelimishanee

Member
May 23, 2018
20
18
Na Mwandishi wetu, Dar

Kampuni inayozalisha taulo za kike ya Human Cherish (HQ), Desemba 8, 2021 ilifanya Mkutano na waandishi wa habari kwa lengo la kutangaza uboreshaji wa huduma za kampuni hiyo,Sambamba na kugawa bidhaa hizo kwa waandishi waliokuepo katika Mkutano huo.

Katika hali ya kushangaza taulo hizo ziligundulikana kuwa zimeshakwisha muda wake wa matumizi(exp).

Baada ya kutokea kwa Sintofaham hiyo baadhi ya waandishi walifanya jitihada za kutafuta Uongozi wa Kampuni hiyo ili kuweza kuzungumza nao juu ya tukio hilo lakini hawakufanikiwa kuwapata.

Chanzo cha taarifa hizi kilielezea kuwa, walishangazwa na tukio hilo huku wakigubikwa na maswali mengi kichwani yaliokosa majibu .

"Ilinza kama masihara Mwandishi mmoja alituma picha kwenye group akielezea kuwa taulo alizopata yeye zimekwisha muda wa matumizi, na kututaka tukague na za kwetu Ili kuangalia usalama wa bidhaa hizo lakini majibu yalikuja sawa kuwa zote zimemaliza muda"kilielezea chanzo hicho.

Kiliendelea kusema kuwa, ni jambo la aibu mno kufanya tukio hilo kwa waandishi wa habari, huku akihoji ni box ngapi zimepelekwa mashuleni kwa ajili ya wanafunzi, na je zipo salama kweli....wangapi wametumia na nini kitatokea kwa watu ambao wameshatumia.

"Tunaziomba mamlaka husika kufatilia kampuni hii juu ya bidhaa zinazozalishwa kwani hatuna tena Imani nazo, sijui wamekusudia nini, au watasema walikua hawajui kua zimekwisha muda wa matumizi"kilihoji chanzo hizo.

PicsArt_12-10-10.15.08.jpg
 
Si mzitupe na mnunue nzuri kwa fedha zenu.Utashangaa na madume yanalia yamepewa Pedi zilizopita muda tena mengine hayajaoa
 
Na Mwandishi wetu, Dar

Kampuni inayozalisha taulo za kike ya Human Cherish (HQ), Desemba 8, 2021 ilifanya Mkutano na waandishi wa habari kwa lengo la kutangaza uboreshaji wa huduma za kampuni hiyo,Sambamba na kugawa bidhaa hizo kwa waandishi waliokuepo katika Mkutano huo.
Majumbani mwenu mnavitu vingapi vilivyoisha muda wa matumizi lakini bado mnavitumia.
 
Wamelia kwani wamelipia?

Umaskini ni kitu kibaya sana.

Yes wamekosea kuwapa pedi zilizoisha muda wake.

Ila tabia ya kupenda dezo ndio imewaponza...
Hii hoja yako haina mashiko,Hio kampuni ya ndio iliitisha mkutano wa waandishi kutangaza uboreshaji wa huduma sambamba na kugawa hizo taulo zao bure.

Sasa huoni kwamba walichofanya Kampuni ni uhuni mtupu,kwanza umeenda kutangaza kuboresha huduma halafu watu hao hao uliotegemea wakutangazie ubora wa bidhaa zako unawapa Pedi zilizokwisha muda wake unategemea wakae kimya?

Kampuni haikuombwa walifanya kwa matakwa yao,sasa huoni kwamba wanahatarisha afya za watu?

Kama wanaweza kufanya uhuni huu kwa watu kama waandishi ambao wana platform za kufikisha ujumbe kirahisi vipi huko mashuleni wanakoenda kujidai kutoa misaada? Isije ikawa shuleni ndio wanafanyia dumping site kwa bidhaa zao zilizoharibika kwa kigezo cha kutoa misaada.

Kwa hapa waandishi wapo sahihi sana tena walitakiwa wakawashtaki kabisa kwa huu upuuzi wao.
 
Wamelia kwani wamelipia?

Umaskini ni kitu kibaya sana.

Yes wamekosea kuwapa pedi zilizoisha muda wake.

Ila tabia ya kupenda dezo ndio imewaponza...
Utakuta hizo pedi walizopewa ghalama yake haifiki hata elfu kumi kwa kila mwandishi mmoja.
 
Hii hoja yako haina mashiko,Hio kampuni ya ndio iliitisha mkutano wa waandishi kutangaza uboreshaji wa huduma sambamba na kugawa hizo taulo zao bure.

Sasa huoni kwamba walichofanya Kampuni ni uhuni mtupu,kwanza umeenda kutangaza kuboresha huduma halafu watu hao hao uliotegemea wakutangazie ubora wa bidhaa zako unawapa Pedi zilizokwisha muda wake unategemea wakae kimya?

Kampuni haikuombwa walifanya kwa matakwa yao,sasa huoni kwamba wanahatarisha afya za watu?

Kama wanaweza kufanya uhuni huu kwa watu kama waandishi ambao wana platform za kufikisha ujumbe kirahisi vipi huko mashuleni wanakoenda kujidai kutoa misaada? Isije ikawa shuleni ndio wanafanyia dumping site kwa bidhaa zao zilizoharibika kwa kigezo cha kutoa misaada.

Kwa hapa waandishi wapo sahihi sana tena walitakiwa wakawashtaki kabisa kwa huu upuuzi wao.
Wenye uwezo wa kuelewa wameelewa!
Soma tena...
 
watu wenyewe wanamtumia pugi mwenye nuksi kila kona ya mwili wake wacha wachafuke
 
Hii hoja yako haina mashiko,Hio kampuni ya ndio iliitisha mkutano wa waandishi kutangaza uboreshaji wa huduma sambamba na kugawa hizo taulo zao bure.

Sasa huoni kwamba walichofanya Kampuni ni uhuni mtupu,kwanza umeenda kutangaza kuboresha huduma halafu watu hao hao uliotegemea wakutangazie ubora wa bidhaa zako unawapa Pedi zilizokwisha muda wake unategemea wakae kimya?

Kampuni haikuombwa walifanya kwa matakwa yao,sasa huoni kwamba wanahatarisha afya za watu?

Kama wanaweza kufanya uhuni huu kwa watu kama waandishi ambao wana platform za kufikisha ujumbe kirahisi vipi huko mashuleni wanakoenda kujidai kutoa misaada? Isije ikawa shuleni ndio wanafanyia dumping site kwa bidhaa zao zilizoharibika kwa kigezo cha kutoa misaada.

Kwa hapa waandishi wapo sahihi sana tena walitakiwa wakawashtaki kabisa kwa huu upuuzi wao.
Binafsi nawalaumu hao waandishi kwa uzembe. Unashindwa vip kukagua bidhaa muda huo huo? Tena mwandishi? Mwandishi akilalamika raia wa kawaida utakuwaje?
 
hamna wanachoweza kufanya hao waandishi.....hiyo kampuni sio ya kitoto....ina baraka zote kutoka kwa MAMA.....uliza ni makontena mangapi ya barakoa yalirudishwa yalikotoka.....HQ zilipita bila mbilinge......hii nchi ISHI KWA BUSARA ZA KUZALIWA, na sio za kukopi....
 
daa kweli hali ya Maisha ngumu, sijui walitaka wapewe mpya wakauze??
 
Back
Top Bottom