Waandishi wa habari 12 wauawa kwenye vita nchini Ukraine

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,480
9,239
Waandishi wa habari 12 wamekufa nchini Ukraine tangu kuzuka kwa vita nchini humo mwezi mmoja uliopita taarifa hii ikiwa ni kulingana na mwanasheria mkuu Iryna Venediktova.

Ameandika kupitia ukurasa wa Facebook kwamba pamoja nao waandishi wengine 10 wamejeruhiwa wakati wa mapigano hayo.

Kulingana na Venediktova waandishi hao waliuawa na wanajeshi wa Urusi na kuongeza kuwa taarifa hizo zinaweza kuthibitishwa na vyombo huru.

Kulingana na uchunguzi uliofanyika hadi sasa karibu wawakilishi wa vyombo vya habari 56 wameshambuliwa ikiwa ni pamoja na vyombo 15 vya kigeni.

Venediktova amesema waandishi wa kigeni ni wa mashirika ya Uingereza, Jamhuri ya watu wa Czech, Denmark, Uswisi, Umoja wa Falme za Kiarabu na Marekani.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom