Indume Yene
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 2,950
- 711
Huyu mwandishi inaelekea hata hamjui Robert Maxwell. Kuanguka kwa huyu fisadi wala haikuwa kwasababu ya kuchanganya biashara na siasa.
Ina fact kwa UK ni kawaida kwa wafanyabiashara wanaohusika na vyombo vya habari kuchanganya siasa na biashara.
Ukiangalia UK na USA, Rupert Murdoch na vyombo vyake (SKY NEWS, FOX NEWS, SUN etc) wanafikia hata kuamua nani awe rais au PM. Hivyo hivyo Italy kwa Berlusconi na vyombo vyake anaendelea na biashara pamoja na siasa.
Kuanguka kwa Maxwell ilikuwa sio kwasababu ya kujihusisha na siasa, ilikuwa kwasababu ya ufisadi. Muda wote alikuwa anatumia njia za mkato kujitajirisha kwa cost ya wafanyakazi wake na wanyonge wengine.
Mwandishi hajafanya homework ya kutosha labda kwasababu yuko biased na lengo lake lilikuwa kumshambulia mengi. Ukiandika makala ukiwa na chuki na mtu sio rahisi kuja na arguments ambazo ni balanced.
Nakuunga mguu kwa asilimia 700. Naamini mwandishi ana chuki fulani dhidi ya Mengi. Penye ukweli daima uongo hujitenga. Na gazeti hilo ni moja ya magazeti ambayo yalianzishwa yakiwa na ajenda rasmi nazo ni kupinga ukweli, kusafisha mafisadi kwa kutumia kalamu za waandishi na migongo ya wananchi.
Lakini nawapa pole maana WATANZANIA wameelimika na busara zaidi kutambua pumba na mchele.