Vyombo vya habari ni njia moja nzuri sana ya kuboresha lugha na njia mojawapo hatari sana ya kuharibu lugha tena kwa kasi sana..., Leo katika pitia pitia magazeti ya nyumbani katika mojawapo ya gazeti linalonivutia kwa habari zake 'mwananchi' wakati nasoma habari yenye kichwa cha habari "Polisi aliyepigwa na majambazi atolewa hospitali na risasi mwilini" ya tarehe 12/05/2009 tovuti "http://mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=11906" kusema kweli sikuridhika na uandishi ufuatao
"Katika mapambano hayo, majambazi wawili walipoteza maisha, na wengine wawili, akiwemo askari huyo na raia mmoja, walijeruhiwa."
Sijui kama ntakuwa nimekosea mimi au vipi ila kwa sentensi hiyo unaposema majambazi wawili ....., na wengine wawili ...., kwa ueleo wangu wa kiswahili nadhani hapo bado tunaongelea majambazi hivyo nadhani hapa neno wengine sio mahala pake kwa fikra zangu sentensi hii ilibidi iandikwe vingine ili kutofautisha vitu vitatu mosi waliofariki, pili waliojeruhiwa na tatu majambazi,raia na askari.Kwani ikibaki hivyo ilivyo inaonekana kana-kwamba huyo askari alikuwa ni mmojawapo wa majambazi hayo.
wakadau kama kuna mchango wowote toeni ili turekebishane lugha yetu bado inakuwa kurekebishana ni muhimu (maana labda mimi nimesoma vibaya).
"Katika mapambano hayo, majambazi wawili walipoteza maisha, na wengine wawili, akiwemo askari huyo na raia mmoja, walijeruhiwa."
Sijui kama ntakuwa nimekosea mimi au vipi ila kwa sentensi hiyo unaposema majambazi wawili ....., na wengine wawili ...., kwa ueleo wangu wa kiswahili nadhani hapo bado tunaongelea majambazi hivyo nadhani hapa neno wengine sio mahala pake kwa fikra zangu sentensi hii ilibidi iandikwe vingine ili kutofautisha vitu vitatu mosi waliofariki, pili waliojeruhiwa na tatu majambazi,raia na askari.Kwani ikibaki hivyo ilivyo inaonekana kana-kwamba huyo askari alikuwa ni mmojawapo wa majambazi hayo.
wakadau kama kuna mchango wowote toeni ili turekebishane lugha yetu bado inakuwa kurekebishana ni muhimu (maana labda mimi nimesoma vibaya).