Waandishi acheni ushabiki wa kisiasa

dos santos

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
256
128
Nilikuwa naangalia taarifa ya habari leo asubuhi kupitia kituo cha TBC,kuhusiana na mkutano wa waandishi wa habari na viongozi wa BAKWATA huko Igunga. Nilichoshuhudia ni sintofahamu baina ya waandishi wa habari na viongozi hao wa BAKWATA.Mvutano ulikuwa ni juu ya vazi la Hijabu.

Mshangao nilioupata ni pale baadhi ya waandishi walipokuwa wanang'ang'ania maelezo yao ndo sahihi kuliko yaliokuwa yanayotolewa na viongozi hao.Kiasi kwamba kukatokea malumbano baina yao kila upande ukishutumu mwingine anatumika kisiasa. Mshangao zaidi ni Mwandishi kabla hajaenda kuripoti hiyo habari ameshaonesha hisia na dhana ya kutoamini anachotakiwa kuripoti kwa wananchi,na badala yake anaanzisha mabishano. Wasiwasi je mwandishi huyu ataripoti alichonukuu au hisia na dhana zitajaa katika kuripoti habari hiyo?

Ukweli ni kuwa (hawapendi kuusikia) waandishi wengi wamekuwa wakitumika kisiasa,na wengine wakiripoti kishabiki katika habari mbalimbali.Jinsi walivyokuwa wakiuliza maswali kwa viongozi hao, kulikuwa na utashi zaidi wa kisiasa kuliko taaluma ya uandishi wa habari. Kama kuhoji ndo muongozo wa taaluma yao,angalia ripoti za tukio la Babu wa Loliondo.


Je waandishi walihoji kwa kina usahihi wa maelezo yaliyokuwa yanatolewa kuhusiana na dawa hiyo? Au wao ndo walikuwa ni vinara wa kuhamasisha wananchi kwamba dawa hiyo inaponya hata kabla ya ripoti za kitaalamu kutolewa. Waliongozwa zaidi na ushabiki kuliko usahihi wa jambo lenyewe. Hatimaye muda umetoa majibu sahihi,dawa hiyo inaponya au la.Bila shaka jibu unalo.


Tuwanasihi waandishi wasiripoti kishabiki au kutumiwa kisiasa ni hatari kwa jamii yetu.Na waandishi nao wakubali kukosolewa na pia wakubali walipokosea, kwani hakuna kundi linalojiona lipo sahihi zaidi, na lisilokosoleka kama wao. Wao si Malaika ni binaadamu wa kawaida wana udhaifu kama wengine. Kumbuka mwandishi ana haki ya kuwa shabiki wa chama chochote cha siasa ila anapokuwa katika taaluma yake anabanwa kuripoti kwa utashi wake.


Tuwapongeze kwa kazi nzuri wanayoifanya na tuwakosoe pale wanapokwenda kombo.Kwa kushirikiana tutafika
 
Lkn ktk inshu ya hao bakwata,wao wenyewe maelezo yao yalikuwa yana attract more questions and clarifications, mtu anapotoa maelezo tata sharti aulizwe tena na tena ili kupata jibu moja. Aidha nakubaliana nawe kuwa kiujumla hata ktk maswala mangine waandishi lazima waongozwe na miiko ya kazi na c ushabiki.
 
Wataacha kuwa mashabiki vp, na wakati kwenye payrol ya NAPE na wenyewe walijumuishwa..
 
Ndugu yangu hao siyo waandishi. Ni wachumia tumbo na wala hatushangai wanaporipoti utumbo.
 
Hawawezi wakaacha kushabikia siasa kwasababu ndiyo inayoendesha nchi.
 
Wana ushabiki kwa kuwa walikuwa wakiwabana wale mashekhe watoe maelezo kuhusu hijabu au?. Mböna sikuelewi. Ulitaka wakaripoti tu bila kupata clarification? Wao wenyewe(mashehe na wale kina mama waliovaa hijabu) walionyesha katika definition zao kuwa hjabu lazma ifunike mwili hata mikononi kasoro uso (kacheck kwenye youtube kwenye CTV)!..

Sasa hapo maswali yakajaa..kama alivaa hijabu na cyo mtandio mbona bi fatma mikono ilikuwa wazi..? Mbona kifua kilikuwa wazi?..! Waliposhndwa kujibu hapo sasa ndo wakaona waandish wanatumiwa kama wewe dos santos na wenzio mnavyosema. Ila wao, ah ah..wanatetea uislam na cyo chama..Bullshit!
 
Tz hakuna waandishi wa habari kuna makanjanja,samahani najua ukwel mchungu.We kaangalie vichwa vya habari vya MAJIRG na MTANZANIA vinafanana kabisa utajua waandishi wamefika pahala pa kupangiwa hata vichwa vya magazeti.

HIVI NYIE WAANDISHI MNAWAULIZA MASHEIKH KUWA IJABU IKOJE WANAWAPA MAELEZO MNAYAKATAA MMEKUA MAPILATO AU?.MNAKERA SANA .SERA HAMTUANDIKII MNAANDIKA MATUKIO TU. WATU WA AJABU, MNATUPELEKA WAPI WATZ, SIJUI KWA SABABU WENGI NI WAK..STO
 
Hata wewe habari uliyoiandika inaonyesha huna msimamo wako binafisi. Kwenye tukio lolote watu wanakuwa na mitazamo tofauti, kazi ya waandishi ni kuuliza maswali ambayo yanaleta majibu kwa mitazamo yote. Mwaandishi anaweza kuuliza swali kulingana na mtazamo wake binafsi au wa rafiki yake au wa mtu aliyemtuma, of course kila news media ina itikadi na mtizamo wake kuhusu masuala mbalimbali ya kijamii.

Wajibu upo kwa aliyeitisha mkutano na waandishi wa habari kuthibitisha uhalali wa msimamo wake, waandishi kazi yao ni kumpa changamoto ili ukweli upatikane. Mwitisha mkutano lazima awe amejiandaa, awe na majibu yanayoridhisha ili kufanikisha mkutano wake, vinginevyo itakuwa kituko kama ulichokiona igunga. Bakwata walioita mkutano walikuwa na wajibu wa kujibu swali lolote la waandishi wa habari hata kama ni la kijinga.

Waandishi walikuwa na haki ya kuwauliza Bakwata kama hawatumiki kisiasa na Bakwata walitakiwa watoe jibu na siyo kuwauliza waandishi swali hilo hilo. Kumbuka wajibu wa mwitisha mkutano ni kutoa majibu tu bila kuuliza maswali, na waaandishi wajibu wao ni kuuliza maswali tu na siyo kutoa majibu.
 
Back
Top Bottom