Mimi si mwandishi wa habari kwa taaluma lakini leo nataka niwashitue waandishiw wa Tz. sote tulimwona Jm akirusha habari zilizopelekea matrafiki kuonekana wakipokea rushwa, hatimaye Jm sasa hajui kama Mei mosi atakua uraiani au la. Ukifuatilia vizuri kuna maswali mengi ya kujiuliza. Kama vile zile pingu alinunua lini, bastola je? Nani alijua kuwa anazo? kwanini kumilikishwa kwake kuibue tafrani baada ya yeye kurusha kipindi mkakati hewani. Narudi kwenu waandishi, kuna historia kama za akina Jm duniani chungu mzima, tuna Asange pia, je, waandishi leo mnamkakati gani juu ya Jm? Kwani mwenzio akinyolewa... Wenzenu duniani hupiga kelele na kusaidiana kama tulivyoona wakati wa Asange. Je, ninyi wa Tz ndiyo mmekaa tu na kufurahia? yu wapi mwandishi wa Trailing the merchant of death? je si yeye aliye fanya uchunguzi wa kijasusi hata akaiibua kashifa ya minofu ya sangara dhidi ya silaha zilizokuwa zikiletwa east & central africa kupitia mwanza? Amkeni fanyeni juu chini ukweli wa JM uanikwe kwani kuwaachia askarihali twajua ni adui zake? HaleluYahu.