Waandamanaji wavamia Ubalozi wa Afrika Kusini kudai kuachiwa kwa ndege ya Tanzania. Watatu wakamatwa wakidaiwa kuwa viongozi

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Umati wa watu umejitokeza leo nje ya Ubalozi wa Afrika Kusini jijini Dar es Salaam ukishinikiza kuachiwa kwa ndege ya Air Tanzania iliyoshikiliwa nhini Afrika kusini kufuatia kesi ya fidia inayomhusu Bwana Hermanus Steyn wa nchio hiyo na Serikali ya Tanzania.
******

Kundi la Watanzania limejitokeza leo nje ya Ubalozi wa Afrika Kusini uliopo jijini Dar likishinikiza kuachiwa kwa ndege ya Air Tanzania inayoshikiliwa Afrika Kusini

Ndege hiyo inashikiliwa kwa siku tano zilizopita kutokana na kesi ya kudai fidia inayomhusu Hermanus Steyn, raia wa Afrika Kusini dhidi ya Serikali ya Tanzania

Watu hao waliokusanyika nje ya Ubalozi huo wameonekana wamebeba mabango mbalimbali huku wakiimba “Tunataka ndege yetu”

UPDATES
Watu watatu wanaodaiwa kuwa viongozi wa maandamano ya kushinikiza kuachiwa kwa ndege ya Air Tanzania yaliyofanyika nje ya Ubalozi wa Afrika Kusini wanashikiliwa na Polisi

Kamanda wa Polisi, Lazaro Mambosasa amesema wao kama Jeshi la Polisi hawaruhusu maandamano wala mtu kufanya anavyofikiria yeye

Amesema “Baada ya kupata taarifa niliamuru Kikosi cha kutuliza ghasi (Field Force Unit - FFU) na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ilala kwa ajili ya kuchukua hatua, kwanza kuzuia maandamano na kuwakamata walioratibu maandamano

Aidha, ameongeza kuwa chochote watu hao wanachotaka kupeleka kwa umma wanaweza wakaandika au wanaweza wakatuma wawakilishi


 
Ningependa kupata elimu ya kujitoa ufahamu japo ilitakiwa waende kule SA ''RSA'' mimi binafsi nadhani maandamano hayana tija Serikali iko makini na ndiyo maana mawakili wameenda Afrika kusini tujifunze kuwa wavumilivu kama wanauchungu basi wachangie deni ama wallilipe lote ''mahakama huwa haingiliwi''
 
Umati wa watu umejitokeza leo nje ya Ubalozi wa Afrika Kusini jijini Dar es Salaam ukishinikiza kuachiwa kwa ndege ya Air Tanzania iliyoshikiliwa nhini Afrika kusini kufuatia kesi ya fidia inayomhusu Bwana Hermanus Steyn wa nchio hiyo na Serikali ya Tanzania.
kwani ubalozi ndio umeishikilia? Si wakaandamane mahakama ya Gauteng?
 
Umati wa watu umejitokeza leo nje ya Ubalozi wa Afrika Kusini jijini Dar es Salaam ukishinikiza kuachiwa kwa ndege ya Air Tanzania iliyoshikiliwa nhini Afrika kusini kufuatia kesi ya fidia inayomhusu Bwana Hermanus Steyn wa nchio hiyo na Serikali ya Tanzania.

Intelejensia ya policcm kujeni huku kuna fununu ambazo hamjazipata bado.
 
#BreakingNews:

Umati wa watu umejitokeza leo nje ya Ubalozi wa Afrika Kusini jijini Dar es Salaam ukishinikiza kuachiwa kwa ndege ya Air Tanzania iliyoshikiliwa nhini Afrika kusini kufuatia kesi ya fidia inayomhusu Bwana Hermanus Steyn wa nchi hiyo na Serikali ya Tanzania.

#AzamTVUpdates #BreakingNews, #AzamTVApp #AzamTV #AzamTWO #AzamTVHabari #Habari #UTV #UFM

Angalia Video Kamili Hapa
 

Attachments

  • 1566980207840.png
    1566980207840.png
    239.6 KB · Views: 59
#BreakingNews:

Umati wa watu umejitokeza leo nje ya Ubalozi wa Afrika Kusini jijini Dar es Salaam ukishinikiza kuachiwa kwa ndege ya Air Tanzania iliyoshikiliwa nhini Afrika kusini kufuatia kesi ya fidia inayomhusu Bwana Hermanus Steyn wa nchio hiyo na Serikali ya Tanzania.

#AzamTVUpdates #BreakingNews, #AzamTVApp #AzamTV #AzamTWO #AzamTVHabari #Habari #UTV #UFM
Hebu funguka kidogo, maandamano hayo yanahusisha watu gani??

Je ni watanzania wa "praise and worship for Magufuli" ??

Kifupi tu kwenye nchi inayoendesha mambo yake kwa kuheshimu mhimili wa mahakama, hata kama mtaandamana kwa mamilioni, mtakuwa mnapoteza muda wenu bure tuuuu

Dawa ya Deni ni kuilpa. Full Stop
 
Back
Top Bottom