mbwe
JF-Expert Member
- Feb 23, 2018
- 1,173
- 2,873
Natunaini wote ni wazima humu na mnaendelea na majukumu ya kila siku. Nijielekeze moja kwa moja kwenye hoja yangu tajwa hapo juu,serikali imekuwa na tabia ya kuwaonea walimu kila siku kila mwana siasa anajipima ubavu kwa hawa ndugu zetu walimu .Jiulize Leo unamtoa mwalimu kumpeleka primary bila hata senti moja kwa madai eti ni ndani ya kata ,swali je kama huyu mwalimu alikuwa anaishi kwenye nyumba ya shule na ukampanga shule amabyo haina hata nyumba Moja ya walimu atajimudu vipi kuanza maisha mapya?yani mnawatumia Wakati Wa uchaguzi Leo hii mnawanyanyasa kwa staili hii ,kisheria huyu mwalimu alitakiwa apewe posho ya usumbufu na kujikimu Siku kumi na NNE.ngoja niishie hapa ila unyanyasaji huu kwa walimu Ipo siku utaisha tu maana uvumilivu ukipotea kifutacho ............