Waajiri tendeni haki kwa wasichana kumbuka nawe ulizaliwa na mwanamke

mamabaraka

Member
Oct 18, 2011
92
14
kuna baadhi ya waajiri hasa ktk mashirika binafsi wanakwepa kuajiri wasichana, mi niliwah kusikia katika ofisi moja mkurugenzi akisema ukiajiri msichana graduate una hasara, akifanya kazi kidogo utasikia anataka kuolewa, akiolewa atapata mimba na kuanza kuumwa umwa kila mara anaomba ruhusa, akijifungua anadai matenity leave. Baada ya hapo mara mtoto anaumwa nampeleka hospitali mara clinic. Jamani waajiri na nyie mmezaliwa na wanawake tendeni haki kwa mabinti. Mnawanyanyasa kijinsia haipendezi kabisa.
 
Hata ofısı za Serıkalı ıkıtokea wanawake wengı wakıpata mımba kwa mfuatano mabosı wa kıume mara nyıngı hawafurahıı kwa sababu kazı zınalala sana hasa wakatı wa maternıty leave. Ingawa sıyo kosa lao kwanı hakuna anayekuwa akıjua kuwa kıpındı hıcho hıcho mwenzake pıa anapewa ujauzıto.
 
Hawapendi wangezaliwa Kama sio Hao wanawake? Wanajitoa fahamu mbona wakezao wakiwa na mimba wanafurahi japo mimba si zao...
 
Hawapendi wangezaliwa Kama sio Hao wanawake? Wanajitoa fahamu mbona wakezao wakiwa na mimba wanafurahi japo mimba si zao...

ahahahahahah umenchekesha! ni kweli kabisa me nshawah ona nafasi za kazi wamesema wanataka wanaume tu! sio haki jaman....kwa Mola mtaenda adhibiwa!
 
Upande mmoja inauma ila kwa upande mngine ukizingatia sio kosa lao, wenyewe wanatafuta productivity.
Naweza kusema ni kosa la paternalist system nzima, inayo toa value kwa kazi za watu wasio shinda nyumbani kusaidia basic needs za reproduction, feeding, shelter na mengine. wanaume au wanawake wanao taka kuonekana productive leo, lazima wacompete katika field za nje ya zile primary needs, huku ikiwa vigumu kwa mwanamke kuziacha moja kwa moja.
Kama system inge ipa thamani kazi watu wanayo ifanya hata manyumbani kwao kama kazi za ndani, za kulea watoto, kupika na kadhalika, kwa kweli hawange lazimika kutafuta hizo kazi za ofisini ikiwa bado wanataka kua na watoto kila miaka miwili au mitatu.
Ni swala ngumu sana kutatua.
 
kwa ukweli mabosi wengine hawako wazi kwa akina mama ni vema kuwajali manake nao wana wake zao na watoto nyumbani. tujue watoto ni taifa la kesho, sasa mama akienda matenity leave ndo majungu yanaanza! oooh jamaa hawafwati nyota ya kijani? tena ukute ndo umeunganisha kila mwaka mazee unalooooo!!!!:tongue:
 
Hili kwel hata mm huwa linanishangaza sana kuna shule moja ipo Dodoma mfanyakazi yeyote wa kike (walimu, secretary na wengine) akipata ujauzito anaanza kuhesabu siku za kufanya kaz. Akijifungua tu ndo mwisho wa kazi. Mbaya sana.
 
Hata ofısı za Serıkalı ıkıtokea wanawake wengı wakıpata mımba kwa mfuatano mabosı wa kıume mara nyıngı hawafurahıı kwa sababu kazı zınalala sana hasa wakatı wa maternıty leave. Ingawa sıyo kosa lao kwanı hakuna anayekuwa akıjua kuwa kıpındı hıcho hıcho mwenzake pıa anapewa ujauzıto.

Hivi nyie mkoje? Kama wewe ni bosi, unatoa ripoti ya kazi kwa mkubwa wako, unaweza kuweka hapo kipengele kuwa : Mapato yamepungua kwa kuwa uzalishaji mwaka huu umeshuka kwa vile wamama 17 walikuwa maternity leave?

Kazi ya bosi ni kuangalia ufanisi wa ofisi yake na wala sio kubalance jinsia kazini. Kwanza wanawake huwa wahako serious, kwa mfano saa hizi badala ya kufanya kazi, mko mnachat, baada ya miezi miwili, una mimba. Leo mtoto anaumwa, kesho kafa bibi yako, kesho kutwa unaenda ngomani, mara unasikia kichefu chefu. All in all, tutambue kuwa muajiri anawajibika kufanikisha kazi na sio kubalance jinsia.
 
Upande mmoja inauma ila kwa upande mngine ukizingatia sio kosa lao, wenyewe wanatafuta productivity.
Naweza kusema ni kosa la paternalist system nzima, inayo toa value kwa kazi za watu wasio shinda nyumbani kusaidia basic needs za reproduction, feeding, shelter na mengine. wanaume au wanawake wanao taka kuonekana productive leo, lazima wacompete katika field za nje ya zile primary needs, huku ikiwa vigumu kwa mwanamke kuziacha moja kwa moja.
Kama system inge ipa thamani kazi watu wanayo ifanya hata manyumbani kwao kama kazi za ndani, za kulea watoto, kupika na kadhalika, kwa kweli hawange lazimika kutafuta hizo kazi za ofisini ikiwa bado wanataka kua na watoto kila miaka miwili au mitatu.
Ni swala ngumu sana kutatua.

Wewe peke yako hapa ndio umeongea kitu cha maana. Watu hapa wanafikiri kuwa MAKAMPUNI YAPO ILI WAO WAAJIRIWE WALIPWE MISHAHARA wkt uhalisia ni kwamba makampuni yapo ILI YAZALISHE YAPATE FAIDA NA YAENDELEE KUWEPO. Tatizo letu watanzania ni kuwa hata wanaume, tunafikiri mtu akianzisha kampuni yake anaanzisha ili sisi tupate ajira. Hakuna anayejua kuwa inaanzishwa kwa lengo la kuzalisha na hii ndio maana mara nyingi watu hawajali wala kuona vibaya kulipwa hata kama wanapafom below standad.

Ukiangalia maneno yalioandikwa hapa, utaona dhana ya uwajibikaji haieleweki kabisa. Hona huyu anasema ujinga gani?
kwa ukweli mabosi wengine hawako wazi kwa akina mama ni vema kuwajali manake nao wana wake zao na watoto nyumbani. tujue watoto ni taifa la kesho, sasa mama akienda matenity leave ndo majungu yanaanza! oooh jamaa hawafwati nyota ya kijani? tena ukute ndo umeunganisha kila mwaka mazee unalooooo!!!!:tongue:

Yaani mtu unakuwa haupo serious kiasi unaamini mwajiri afurahi wewe kuwa mjamzito kila mwaka! Hivi kweli jamani kama tuna akili hata kidogo, nikuajiri uwe unauza dukani kwangu, halafu miezi 4 kati ya 11 unakuwa nyumbani unanyonyesha halafu mimi biashara yangu inakuwaje?
 
ofisi nyingne inaeleweka kuwa matenity leave inatolewa baada ya miaka mitatu, lakin kwa wanaume mnaochangia mada pia muangalie mkeo anafukuzwa kazi kisa mjamzito. Tena ofisi nyingne washenzi kweli ukigundulika una mimba unapewa barua ya kufuzwa kazi. Kama tatizo ni productivity itaftwe another alternative kuwasaidia kina mama. Kama anapata mimba kila mwaka apewe likizo bila malipo, lakin kama mtu anafata utaratibu inakuwaje kumwachisha kazi? Na saa nyingine mama wa watu ni mchapakazi kweli kweli? Its not fair.
 
ofisi nyingne inaeleweka kuwa matenity leave inatolewa baada ya miaka mitatu, lakin kwa wanaume mnaochangia mada pia muangalie mkeo anafukuzwa kazi kisa mjamzito. Tena ofisi nyingne washenzi kweli ukigundulika una mimba unapewa barua ya kufuzwa kazi. Kama tatizo ni productivity itaftwe another alternative kuwasaidia kina mama. Kama anapata mimba kila mwaka apewe likizo bila malipo, lakin kama mtu anafata utaratibu inakuwaje kumwachisha kazi? Na saa nyingine mama wa watu ni mchapakazi kweli kweli? Its not fair.

Tatizo sio mke wa nani, tatizo ni nini mwenye kampuni ametarget wakati anaanzisha kampuni yake. Wewe mwenyewe ni mfano wa mtu asiyejua mshahara unatoka wapi. Unaposema fulani apewe likizo bila malipo, kazi za huyo fulani anayepewa likizo bila malipo anazifanya nani? Lets be realistic, the business is about bargaining and not begging. Hakuna kitu kama kuwasaidia kina mama kwenye accounts.

Unashauri waajiri wawe flexible kwenye attendance bila kujali mishahara inatokana na uzalishaji. Your only alternative ni kumpa likizo bila malipo, kwa hiyo aajiriwe mwingine au? Wanawake wawe na shughuli za kufanya. Hata haukuwa mpango wa Mungu kumu- engage mwanamke kwenye direct production na ndio maana tuna complications za namna hii. Unaweza ukaniona mbaya kwa ninayoyasema lkn zingatia uhalisia huu.

Piga hesabu una genge lako la kuuza nyanya na vitunguu. Wakati una mimba, tayari una mtoto mwingine mdogo wa miaka miwili. Kwa wingi wa kazi za nyumbani unashindwa kwenda sokoni kuchukua bidhaa za gengeni, kwa hiyo biashara inaanza kusuasua na baadaye unaamua kuacha kabisa. The same inatokea kwenye makampuni tunayofanya kazi. Kinachotufanya tusione ni kwa sababu sisi hatuko responsible na hasara wala faida ya kampuni, mwisho wa mwezi unapokea mshahara kama umefanya kazi au hujafanya, hilo hujali. Na ndio maana si ajabu ukakuta wanawake wanapiga story huku teller desk za benki zimejaa foleni na hakuna anayejali. Siwalaumu lkn kubalianeni na maumbile na mipango ya Mungu.
 
ofisi nyingne inaeleweka kuwa matenity leave inatolewa baada ya miaka mitatu, lakin kwa wanaume mnaochangia mada pia muangalie mkeo anafukuzwa kazi kisa mjamzito. Tena ofisi nyingne washenzi kweli ukigundulika una mimba unapewa barua ya kufuzwa kazi. Kama tatizo ni productivity itaftwe another alternative kuwasaidia kina mama. Kama anapata mimba kila mwaka apewe likizo bila malipo, lakin kama mtu anafata utaratibu inakuwaje kumwachisha kazi? Na saa nyingine mama wa watu ni mchapakazi kweli kweli? Its not fair.

Kampuni ya mumeo ikifa kwa kuwa ameajiri wanawake na wako maternity utampigia makofi kwa kuwajali wanawake au utaanza kulia kuwa nyumba yenu mlioweka dhamana kupata mkopo wa kuanzishia hiyo kampuni itauzwa?

Business ni kitu serious, hakiongozwi na hisia.
 
jamani mmenikatisha tamaa mm nimeolewa nina mwaka ss na ndo nimepata ujauzito na nimeomba kazi kwenye kampuni fulani na wameshanifanyia interview na subiri majibu je kama wakinipa kazi na badae wakajua mm ni mjamzito watanifukuza?jamani naombeni maoni yenu am scared
 
jamani mmenikatisha tamaa mm nimeolewa nina mwaka ss na ndo nimepata ujauzito na nimeomba kazi kwenye kampuni fulani na wameshanifanyia interview na subiri majibu je kama wakinipa kazi na badae wakajua mm ni mjamzito watanifukuza?jamani naombeni maoni yenu am scared. pole sana dada prisca ni kweli hilo linaweza kutokea au lisitokee inategemea bosi wako atakuwaje, du it pains. Jamani kwa wakaka mnaochangia mada jaribu kufikiri wewe binafsi ungekuwa mwanamke umesomeshwa kwa tabu na mzazi mkulima unafanya kazi zako vzr then unafukuzwa kisa tu ni mchamzito. Fikiri ingekuwa wewe.
 
asante mamabaraka naimani Mungu atanihifadhi maana ndo bado changa si rahisi mtu ajue,lol kukaa tena miezi tisa bila kazi na mm nimezoea kufanya kazi sintaweza,ila maoni ni mazuri maana kila mtu ana upeo wake
 
Wakati unaona kwa upande huo, hebu fikiria mfano wa huyu anayeingia kazini na mimba tayari. Sio kwamba nina chuki na wanawake, lkn umeshaona shida atakayopata muajiri ikiwa huyu Priscilla ni secretary au typist? Unaingia kazini leo, baada ya miezi mi4 unaenda maternity ambako unakaa miezi kadhaa. Nani anafanya shughuli zako? UZAZI WA MPANGO UFANYIKE KWA KUZINGATIA MAJUKUMU PIA
 
Tatizo sio mke wa nani, tatizo ni nini mwenye kampuni ametarget wakati anaanzisha kampuni yake. Wewe mwenyewe ni mfano wa mtu asiyejua mshahara unatoka wapi. Unaposema fulani apewe likizo bila malipo, kazi za huyo fulani anayepewa likizo bila malipo anazifanya nani? Lets be realistic, the business is about bargaining and not begging. Hakuna kitu kama kuwasaidia kina mama kwenye accounts.

Unashauri waajiri wawe flexible kwenye attendance bila kujali mishahara inatokana na uzalishaji. Your only alternative ni kumpa likizo bila malipo, kwa hiyo aajiriwe mwingine au? Wanawake wawe na shughuli za kufanya. Hata haukuwa mpango wa Mungu kumu- engage mwanamke kwenye direct production na ndio maana tuna complications za namna hii. Unaweza ukaniona mbaya kwa ninayoyasema lkn zingatia uhalisia huu.

Piga hesabu una genge lako la kuuza nyanya na vitunguu. Wakati una mimba, tayari una mtoto mwingine mdogo wa miaka miwili. Kwa wingi wa kazi za nyumbani unashindwa kwenda sokoni kuchukua bidhaa za gengeni, kwa hiyo biashara inaanza kusuasua na baadaye unaamua kuacha kabisa. The same inatokea kwenye makampuni tunayofanya kazi. Kinachotufanya tusione ni kwa sababu sisi hatuko responsible na hasara wala faida ya kampuni, mwisho wa mwezi unapokea mshahara kama umefanya kazi au hujafanya, hilo hujali. Na ndio maana si ajabu ukakuta wanawake wanapiga story huku teller desk za benki zimejaa foleni na hakuna anayejali. Siwalaumu lkn kubalianeni na maumbile na mipango ya Mungu.

Kweli kazi ipo kwa akina mama.Mimi ninamfano hai wa dada mmoja tulimujiri katika idara ya IT kwa ajili ya kazi maalum lakini tumeishia kupoteza hiyo project.Alianza mara naumwa tumbo mara akapata mimba baada ya hapo akapewa bedrest ya miezi sita plus likizo ya uzazi siku 84 mwaka tayari.Yaani tumepata hasara kwa ajili ya mtu huyo.Sasa fikiria kama ungekuwa nao kama hao watano au kumi shirika kwisha kazi yake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom