Waafrika tunajivunia tulivyoumbwa mfano nguvu za mwili au vitu tulivyovikuta kama mito, milima na madini, kwanini hatujisifii vitu tulivyotengeneza ?

Waafrika tunajivunia tulivyoumbwa mfano nguvu za mwili au vitu tulivyovikuta kama mito, milima na madini, kwanini hatujisifii vitu tulivyotengeneza ?

mkata uzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2025
Posts
2,534
Reaction score
7,586
1779040509543.png


Unajua, sehemu kubwa ya fahari ya jamii yoyote duniani hutokana na vitu walivyovibuni au kuviumba wao wenyewe. Waarabu walitoa mchango mkubwa kwenye mfumo wa namba, wazungu wameunda teknolojia na uvumbuzi usiohesabika, Wachina na Wahindi nao wameacha alama kubwa kupitia kazi na ubunifu wao.

Lakini ukimwangalia Mwafrika mara nyingi hutumia nguvu kubwa kujieleza kupitia mambo ambayo hakuyatengeneza mwenyewe. Atajivunia nguvu alizopewa kwa kuzaliwa, sura au maumbile yake.

Zaidi ya hapo, Mwafrika atajisifia kabila ambalo hakuliumba yeye, atajivunia milima na mandhari ambayo ni sehemu ya mazingira ya asili, au madini yaliyopo ardhini ambayo hakuyatengeneza yeye mwenyewe.

Changamoto kubwa si kuwa hatuna vya kujivunia, bali ni kwamba bado hatujawekeza vya kutosha kwenye ubunifu, utafiti na vitu vitakavyobeba alama yetu duniani kama Waafrika.
 
tuzidi kufikiria,
Tufikirie jana nilikua naangalia sehemu wabunge wanapitisha zaidi ya 25 billion kwenye utalii kwa ajili ya safari kwenda kutangaza utalii nje hao ni bodi tu ya utalii harafu uniambie Waafrika wana akili aisee labda uwizi na ubinafsi..
 
Si hivyo tu bali hata hivyo tunavyojivunia navyo hatufaidiki navyo, waarabu kwa mafuta tu nchi nyingi zimekuwa tajiri ila sisi tumebaki kujivunia mambo mengi tuliyokuwa nayo.
 
Back
Top Bottom