Waafrika tunaamini Mzungu ni ,,Super Human"!

Barbarosa

JF-Expert Member
Apr 16, 2015
22,584
27,782
Aidha kwa kukubali moja kwa moja au kwa siyo kwa moja kwa moja lkn mwisho wa siku Waafrika tunaamini kabisa kwamba Wazungu ni Super human yaani ni zaidi ya binadamu wa kawaida na chochote wakifanyacho ni sahihi!

Hili utaliona kila mahali, kosa hata liwe kubwa vipi likifanywa na Mzungu basi Waafrika tunaona ni sawa na kuliahalalisha ...

Kwa mfano yule dada ya Kikenya tuliyemdhalilishwa pale Mlimani City kwa kutuhumiwa uwizi nina uhakika 100% kama angekuwa ni Mzungu asingetendewa vile au hata tu kama angekuwa Mwarabu au Muhindi asingepigwa wala asingeguswa na si ajabu tungekwenda mbali zaidi na kumgeukia yule aliyesema Mzungu kaiba na kumpa yeye kibano!

Na kama unabisha au unakataa kama Waafrika hatuwaoni Wazungu ni Super Human fanya hii ,,thought experiment" uko br. unasafiri kwa gari, usiku mkubwa wenye giza nene kati kati ya pori kwenye gari lako kuna nafasi ya mtu mmoja tu, halafu watu wawili wanakuomba lifti mmoja Mzungu mwingine Mwafrika mweusi kama mimi utamchukuwa nani? Au fikiria Kitila Mkumbo, Zito Kabwe, Tundu Lisu Mbowe, Lowasa, Kikwete, mimi na wewe tutamchukuwa nani kati ya hao wawili?

Au kama hiyo haitoshi fikiria Zito Kabwe (hapa natolea tu mfano yeye kama Mwafrika ningeweza kutumia mfano wowote ule) ameoa juzi wewe ukaenda kwenye harusi yake bila ya mwaliko Je, utaingia? Sasa fikiria Mzungu bila ya mwaliko aende na atake kuingia kwenye harusi, Je Walinzi watamrudisha mlangoni kama walivyokurudisha wewe kwa kuwa hana kadi ya mwaliko au watamsikiliza na siajabu hata kumuibua Bwana harusi aje amsikilize?

Lakini hali ikoje kwa wenzetu? yaani Wazungu,Wahindi, Waarabu n.k wanatuonaje?
 
Aidha kwa kukubali moja kwa moja au kwa siyo kwa moja kwa moja lkn mwisho wa siku Waafrika tunaamini kabisa kwamba Wazungu ni Super human yaani ni zaidi ya binadamu wa kawada na chochote wakifanyacho ni sahihi!

Hili utaliona kila mahali, kosa hata liwe kubwa vipi likifanywa na Mzungu basi Waafrika tunaona ni sawa na kuliahalalisha ...
sema wewe ndio unaamini sio wote.

swissme
 
Kama wazungu wana uwezo wa kupeleka chombo pluto kilomita takribani billion 5,na chombo kilisafiri miaka tisa na data za sayari ya pluto tukazipata bila shida kwa nini tusiamini kuwa wazungu ni super human???


Lakini Wajapani wanaweza pia, hata Wachina na Wahindi pia wamefanya hivyo, kama hiyo ni sababu, na isitoshe, Mzungu wa Croatia au Romania anahusika vipi na kutuma chombo mwezini?
 
Ni Super Human kwa sababu wengi Wa Ewavumbuzi wa mambo mengi ya maendeleo ambayo binadamu tuna enjoy ni Wazungu. Invention ya mwafrika ni ipi? Angalia tu uundaji Wa kifaa ulichotumia kupost hapa if! Aliwezaje tu kubuni simu, computer, ndege, gari, meli, mashine, satellite, radar, space station? African kwa nini tusimuone mzungu ni Super? Ule ungo Wa kichawi tumeshindwa kuleta technology yake utumike kwa vitu vyenye faida oh mafuta yake damu ya binadamu!
 
Ni Super Human kwa sababu wengi Wa Ewavumbuzi wa mambo mengi ya maendeleo ambayo binadamu tuna enjoy ni Wazungu. Invention ya mwafrika ni ipi? Angalia tu uundaji Wa kifaa ulichotumia kupost hapa if! Aliwezaje tu kubuni simu, computer, ndege, gari, meli, mashine, satellite, radar, space station? African kwa nini tusimuone mzungu ni Super? Ule ungo Wa kichawi tumeshindwa kuleta technology yake utumike kwa vitu vyenye faida oh mafuta yake damu ya binadamu!


Kwa hiyo kulingana na maelezo yako niko sahihi hata wewe pia unaamni hivyo kwamba wazungu ni ,,Super human" na unaingia kwenye hiyo orodha, na kama ukiwa na nafasi moja kwenye gari yako kati ya Mzungu na Mwafrika mweusi kama mimi utamchukuwa Mzungu?!
 
Tunachojiaminisha ni kwamba mtu mweupe ana akili na hekima ila kumbukeni sio wote weupe wana akili ni sio kwamba weusi wengi hawana akili.
Tunajiaminisha hivyo wengi wetu hata mtu akienda hospitali akatibiwa na mzungu atahisi ugonjwa wake umepona bila kuelewa kwamba hawa wazungu wanatoka kwao kuja huku field kule kwao hakuna mtu wa kumfanyia field au research atakushtaki!!
waafrika lifestlye yetu iko tofauti na wenzetu ndo maana tumechelewa kujua mambo sisi hatupendi kujisumbua kutafuta maarifa pia ni watu wa kuridhika na moja hatuahitaji la pili.
Kingine hatupendani binafsi tena hatupendani ktk hali ya compentent ila incompetent ukiona mtu anafanikiwa unapata wivu kwann afanikiwe badala ya kutaka kujua siri zile ili na ww utoke inakuwa tofauti unakuwa unamuombea hata afe maana anafaidi
 
Simpi mzungu Super human kwa kumhudumia kuliko mweusi. Super human kwa matendo yake ya kumletea binadamu maendeleo hapa duniani. Lift uamuzi wangu nimpe nani. Nitampa mzungu ili aone kuwa hata Mimi mweusi najiweza. Pia ni njia ya kubadilishana mawazo na RAIA tofauti. Waaafrika wapo home, kazini daily nainteract nao. Kuombwa lift Na mzungu ni Golden Chance kwangu.
 
Ninachoamini wote tuna uwezo sawa wa kufikiri, tofauti inakuja kwenye social, psycho-economy factors. Wale waliosoma kile kitabu How Erope Undeveloped Africa watanielewa pia kwenye hili. Kama kule Mwakaleli, Bumbuli, Tandahimba, Namtumbo na kweingineko kukiwa na umeme, computer, vitabu na maktaba. Maktaba itoe mafunzo ya IT kwa kila raia wake alie eneo lile, wananchi wapewe saa moja kutumia computer kila baada ya siku tatu, watu wasome majarida ya utafiti, science, kilimo, na vinginevyo. Watoto wetu waanze kujengwa na imani ya kupenda kusoma, nanaamini tutapata wagunduzi wengi katika siku zijazo.
 
When the head is loaded with rotten pumpkins. ....
.
19f23bee45a685e8b2ab6c43ca86c839.jpg
 
Jiulize hivi kuna mzungu, hata kama analipwa buku 10 au zaidi, anayeweza kuja hapa JF na kufanya kazi unayoifanya wewe?
 
Ninachoamini wote tuna uwezo sawa wa kufikiri, tofauti inakuja kwenye social, psycho-economy factors. Wale waliosoma kile kitabu How Erope Undeveloped Africa watanielewa pia kwenye hili. Kama kule Mwakaleli, Bumbuli, Tandahimba, Namtumbo na kweingineko kukiwa na umeme, computer, vitabu na maktaba. Maktaba itoe mafunzo ya IT kwa kila raia wake alie eneo lile, wananchi wapewe saa moja kutumia computer kila baada ya siku tatu, watu wasome majarida ya utafiti, science, kilimo, na vinginevyo. Watoto wetu waanze kujengwa na imani ya kupenda kusoma, nanaamini tutapata wagunduzi wengi katika siku zijazo.
Dar zipo Huduma zote hizo, tumeVumbua nini? Mitaa michafu, foleni kila kona, Maji ya shida, bado tunapikia kuni, tunauza, kupika Na kununua kwenye sidewalks hapo bado tuko Undeveloped? Sisi ndugu tuna IQ tofauti Na Wazungu. Ethiopia not colonized wazungu waliwa undeveloped vipi? Africa hatujawahi kujikubali tuna tatizo tu.
 
Kuna project ya WHO tuliifanyia kazi Dar, head of project alikua Mswiss, alimleta mtoto wa rafiki yake kutoka kwao aje aprogramme IT packages tulizokuwa tunatumia na kutufundisha jinsi ya kutumia. Yule kijana alimaliza degree yake tena wala sio ya IT alisoma science. Any way kwake ilikua holiday, alipewa ticket, mahali pa ku lala na alikuwa na muda wa kujirusha viwanja. Nilimuuliza alijifunzia wapi skills zake, alinijibu kuwa akiwa na miaka 5 baba yake alimnunulia computuer kama birthday present, kutoka pale alijifunza kuifungua, kuifunga, kuprogramme, na vingine vingi na alivyoshindwa baba yake alimsaidia au walitafuta mwalimu. Kwahiyo jinsi unavyowekeza kwa mtoto ndivyo anavyokua mgunduzi.
 
Dar zipo Huduma zote hizo, tumeVumbua nini? Mitaa michafu, foleni kila kona, Maji ya shida, bado tunapikia kuni, tunauza, kupika Na kununua kwenye sidewalks hapo bado tuko Undeveloped? Sisi ndugu tuna IQ tofauti Na Wazungu. Ethiopia not colonized wazungu waliwa undeveloped vipi? Africa hatujawahi kujikubali tuna tatizo tu.
Socia Economy Factor ndiyo inakuja hapo, mtoto atajifunza maktaba wakati hajui jioni atakula nini?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom