X_INTELLIGENCE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2014
- 9,647
- 12,212
aiseeee ila kweli maana ata ukiangalia hotel muhimu za bongo ukivaa kama wazungu wanavyovaa wakiwa huku bongo aki ya Mungu hawakupokei...
bado tunatawaliwa aiseeeYaani watu kama wewe ndiyo mnakubali kuwa second citizens kwenye bara lenu wenyewe. Nilikwenda Malawi kwenye mkutano miaka michache iliyopita, asubuhi nilikwenda bank kabla mkutano haujaanza, kulikua na foleni, nikajiunga kwenye mstari, kwakua ilikua mapema bank haijafunguliwa nilikuwa mtu wa pili, nyumba yangu watatu mzungu. Huduma zilipoanza aliitwa yule mzungu watatu kwenye foleni akahudumiwa kwanza, niliumia lakini pale nilikauka nchi ya watu. Jioni niliuliza wenyeji inakuaje wakanijibu kuwa wazungu hawapangi foleni. Jamani miaka mingapi baada ya uhuru.