Ulimbo
JF-Expert Member
- Aug 14, 2009
- 3,767
- 4,034
Ndio tatizo hilo la kutoijua jamii yako, matokeo yake ni kutojitambua na kukosa mwelekeo- kama upo Dar tembelea barabara ya Ally Bin Said utaona Mbuyu wa Tambiko la Wabantu. Nchi hii haiwezi kujinusuru bila kuondoa kasumba za kikoloni - kasome mada ya Toba ya Mkapa kuhusu matokeo hasi ya Ubinafsishaji na Ugenisishaji!
Naomba tuwekee hiyo mada ya Toba ili tuisome. Nadhani sijakuelewa vizuri unaposema tukatambike, naomba nieleweshe kidogo. Lakini kama tabiko ni huko kutoa sadaka kwa mizimu - Unachinja myama, unaweka nyama sehemu fulani ati Babu/Bibi ale, na unapoondoka Mbwa/paka/kunguru au kitu kingine chochote kinapita na kula zile nyama unasema babu/Bibi amekula, mambo hayo yamepitwa na wakati.
Tutafute tatizo na shuluisho la matatizo na si vingineyo.