Waafrika hatuna uchungu na vifo vinavyotokea ktk nchi za Kiafrika

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,245
24,108
March 19, 2019
Beira, Mozambique

Maafa mkubwa yaliyotokea kusini mwa Afrika kutokana na kimbunga cha Idai kilichokuwa na mwendo kasi wa kilomita 177 kwa saa na mvua kubwa iliyoleta mafuriko makubwa. Hili la sisi wana-wa-Afrika kukosa uchungu na kuchukuliana linaonekana na habari ya maafa haya kukosa habari ndefu hapa JamiiForums na media za barani Afrika kwa ujumla. Tuna uharaka wa kujadili maafa yanayotokea Mashariki ya Kati, Ulaya na Ocenia lakini maafa ktk bara letu hayazungumziwi kwa hisia kali.

Shirika la Msalaba mwekundu Red Cross na serikali ya Msumbiji wanatuambia Zaidi ya mamia ya watu wamepoteza Maisha kutokana na kimbunga Idai. Rais wa Mozambique Mh. Filipe Jacinto Nyusi amesema inakadiriwa watu 1,000 wamepoteza maisha na maelfu ya watu kukosa makazi, chakula na maji safi ya kunywa.

Pamoja na vifo vingi vya watu pia Miundo mbinu kama bandari ya Beira , viwanja vya ndege, maghala ya vyakula, madaraja na barabara vimeharibiwa nchini Mozambique. Magonjwa ya mlipuko yanaweza kutokea kutokana na kukusekana maji salama.

 
Mzungu akifa ndio hasara kubwa duniani. Au hujui hata kwenye nyimbo zetu huwa tunaabudu wazungu ??
Utasikia 'baada ya Mungu, ni mzungu anafuata'

Mwafrika mpe bunduki tu, ataua waafrika wenzake.
Kiufupi this is the worsest generation we have in Africa
 
Hakika ndugu zetu wanaitaji misaada toka kwetu,Kutoa ni moyo usambe sio utajiri.Hongera serekali kwa kuwasaidia ndugu zetu wa Mozambique na Zimbabwe.
 
Raisi wetu alisema jirani yako akipata maafa hakikisha unapata faida kupitia majanga yake.

Nimesikia bandari ya Beira imeharibika vibaya na miundombinu haipitiki, ni muda muafaka kuwakaribisha wale wadau wa Beira wahamie bandari ya Dar.!

Sent using Jamii Forums mobile app
Kufa kufaana aise

Sent using my iPhone using jamiiforum app
 
Mzungu akifa ndio hasara kubwa duniani. Au hujui hata kwenye nyimbo zetu huwa tunaabudu wazungu ??
Utasikia 'baada ya Mungu, ni mzungu anafuata'

Mwafrika mpe bunduki tu, ataua waafrika wenzake.
Kiufupi this is the worsest generation we have in Africa

Hivyo waafrika tulaumu imani zilizokuja na majahazi toka kaskazini ndiyo zimetung'oa kifikra toka barani mwetu kiasi masikio, macho na uandishi wetu hauna tena uhusiano na Afrika. Bongo Bahati mbaya! Tunatamani tuwe nchi za kaskazini au mashariki ya mbali!

Over 1,000 Africans Feared Dead & Africans Are Quiet

Source : Wode Maya
 
March 25, 2019
Paris, France

Baada ya wiki moja kupita kufuatia kimbunga Idai kuikumba kusini mashariki ya Afrika, wahanga wa kimbunga na mafuriko ktk nchi za Mozambique, Zimbabwe na Malawi bado hawajapata misaada muhimu ya kutosha ya kibinadamu kama chakula na madawa.

Wakati huohuo huko nchini Ghana watu zaidi ya sitini (60) wamepoteza maisha ktk ajali ya basi kutokana na ukaidi wa dereva aliyekuwa mchovu kuendelea kushika usukani kuendesha chombo hicho cha moto.


Source : France 24
 
Hivi huko Msumbiji hakuna mabalozi wa nchi za Ulaya na Marekani? Mbona mataifa hayo ambayo hujinasibu kuwa "washirika wa maendeleo" yako kimya???? Hayazungumzii kabisa kinachoendelea Msumbiji, Zimbabwe na Malawi! Wanafiki wakubwa hawa!!!
 
Hivi huko Msumbiji hakuna mabalozi wa nchi za Ulaya na Marekani? Mbona mataifa hayo ambayo hujinasibu kuwa "washirika wa maendeleo" yako kimya???? Hayazungumzii kabisa kinachoendelea Msumbiji, Zimbabwe na Malawi! Wanafiki wakubwa hawa!!!

UINGEREZA JANA IMEPELEKA MSUMBIJI MSAADA WA MADAWA NA CHAKULA KWA KUTUMIA NDEGE ZAKE ZA KIJESHI. NADHANI NA WENGINE WANAENDELEA KUJIKUSANYA KUPELEKA MSAADA WA KIUTU.
 
Hivi huko Msumbiji hakuna mabalozi wa nchi za Ulaya na Marekani? Mbona mataifa hayo ambayo hujinasibu kuwa "washirika wa maendeleo" yako kimya???? Hayazungumzii kabisa kinachoendelea Msumbiji, Zimbabwe na Malawi! Wanafiki wakubwa hawa!!!
Waokoaji wakuu ni wazungu, kama hujaangalia habari kaangalie hata Youtube
 
Hivyo waafrika tulaumu imani zilizokuja na majahazi toka kaskazini ndiyo zimetung'oa kifikra toka barani mwetu kiasi masikio, macho na uandishi wetu hauna tena uhusiano na Afrika. Bongo Bahati mbaya! Tunatamani tuwe nchi za kaskazini au mashariki ya mbali!

Over 1,000 Africans Feared Dead & Africans Are Quiet

Source : Wode Maya

Kwani Dini ndio tatizo unadhani? Unakosea
Tatizo Waafrika bado tuna matatizo mengi mno nchini kwetu, so inakuwa ngumu kufuatilia yanayoendelea kwa jirani.
Pia media zetu hazina hata uwezo wa kwenda kurusha matangazo huko kwa kina..Tunategemea BBV warushe kisha tuchukue kipande turushe pia.
Janga kama hilo lingetokea nchi yoyote ya Ulaya ungekuta linafanyiwa coverage kubwa sana na tv zao za ukanda huo na za kimataifa
 
Hivi huko Msumbiji hakuna mabalozi wa nchi za Ulaya na Marekani? Mbona mataifa hayo ambayo hujinasibu kuwa "washirika wa maendeleo" yako kimya???? Hayazungumzii kabisa kinachoendelea Msumbiji, Zimbabwe na Malawi! Wanafiki wakubwa hawa!!!
Wapo na wanapeleka misaada kimya kimya tu kama sisi tulivyofanya mwaka 2014 pale Zimbabwe....misaada ya kiutu haipaswi kunangwa kisiasa na mbwembwe mingi kama ilivyofanyika kipind hiki!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna nchi zingine wanajitolea misaada kuliko ata nchi za wazungu. Mfano gulf countries wanasaidia sana african countries lakini hawajioneshi kama vile wazungu na ata cc waafrika 2napenda sana kujulikana 2metoa misaada.

Uislamu una2fundisha hivi.
Tutoe Sadaka kiasi kwamba mkono wa kulia unapotoa mkono wa kushoto usijuwe. Sasa wakina jiwe huku na maswaiba wao wazungu wanatoa dunia nzima ijuwe wametoa 😀😀
 
March 19, 2019
Beira, Mozambique

Maafa mkubwa yaliyotokea kusini mwa Afrika kutokana na kimbunga cha Idai kilichokuwa na mwendo kasi wa kilomita 177 kwa saa na mvua kubwa iliyoleta mafuriko makubwa. Hili la sisi wana-wa-Afrika kukosa uchungu na kuchukuliana linaonekana na habari ya maafa haya kukosa habari ndefu hapa JamiiForums na media za barani Afrika kwa ujumla. Tuna uharaka wa kujadili maafa yanayotokea Mashariki ya Kati, Ulaya na Ocenia lakini maafa ktk bara letu hayazungumziwi kwa hisia kali.

Shirika la Msalaba mwekundu Red Cross na serikali ya Msumbiji wanatuambia Zaidi ya mamia ya watu wamepoteza Maisha kutokana na kimbunga Idai. Rais wa Mozambique Mh. Filipe Jacinto Nyusi amesema inakadiriwa watu 1,000 wamepoteza maisha na maelfu ya watu kukosa makazi, chakula na maji safi ya kunywa.

Pamoja na vifo vingi vya watu pia Miundo mbinu kama bandari ya Beira , viwanja vya ndege, maghala ya vyakula, madaraja na barabara vimeharibiwa nchini Mozambique. Magonjwa ya mlipuko yanaweza kutokea kutokana na kukusekana maji salama.



Wana uchungu kwa mabeberu/wayahudi,ivyo saa ngapi watakuwa na uchungu kwa waafrika!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom