Cantalisia
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 5,222
- 2,925
Habari zenu wapendwa,hiki kisa kimemtokea clacment wangu wa kike jana, yeye ana boyfriend wake wa siku nyingi tu tangu chuon, ila ana katabia kakumchanganya na vimeo vyake(kazi za nje), bf wake alisafiri kikazi tangu jtatu na alimwambia anarudi kesho jmoc, bishost kama kawa jana akapata kazi ya nje mida ya lunchtime wakakubaliana watatoka jion coz anajua jamaa hayupo, basi jion wakawa wametoka wako mahali wanapata vinywaji kumbe bf wake karudi bila taarifa na jion ile kamfata kwao na akakaa bar ya jiran na kumtumia msg amfate pale,shost alipopa ile msg akachanganyikiwa na akawa amechenji gafla mshikaji akamuuliza vp akamwambia anatakiwa nyumban haraka akamwambia poa twende nikupeleke wakiwa njian bf wake akapiga simu baada ya kuona mda unaenda,akawa anaikata coz hawezi kupokea mbele ya mshikaji na alimwambia yuko single, jamaa kuona vile akaichukua ile cm ya shost na kupekua akukuta zile msg za bf wake jamaa akaanza kuchati na mume mwenzie akamwelekeza alipo wakenda na shost mpaka pale alipokaa wakakaa shost hapo anasema alikuwa hoi hajui hata atawaambia nn, baada ya salamu yule jamaa akamwambia shost atoe utambulisho hapo ndio kazi ilianza akamtambulisha bf kuwa ni x wake na yule mshikaji ndio wasasa huku machozi yamejaa uso mzima,so yule mshikaji akanyanyuka na kurudi kwenye gari na kumwacha shost na bf wake na kumwambia anamsubiri kwenye gari,shost anasema hawakuongea kitu na bf wake kila mtu akanyanyuka na kuondoka na yeye hakuenda kwenye gari akazima cm na kuingia uchochoron na kurudi hm, sasa hajui cha kufanya kaharibu kote, anashindwa kuwasha cm kapagawa hajui cha kufanya,anahitaji ushauri afanyeje!