Wa Kufanana naye - chumbani

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,947
22,101
na:
lazaro mbilinyi

Wa Kufanana naye - chumbani

Tofauti ya kiumbo kati ya mke na mume ni asilimia ndogo sana ya tofauti kati ya mwanamke na mwanaume kwa ujumla.
Bila kufahamu tofauti zilizopo tunaweza kujikuta katika shida na matatizo au confusion ya uhakiuka chumbani.

Ukiacha tofauti zingine zote zilizopo kati ya mke na mume linapokuja suala la sex mwanaume sex ni hitaji la kimwili kwanza (physical) na baadae emotions wakati mwanamke ni hitaji la emotions kwanza then kimwili.
Hii ina maana kwa mwanamke sex ni upendo kwanza, kujisikia vizuri kwanza, kupata caring kwanza kwa mwanamume ni kuwasha tu na bus linaondoka.

Linapokuja suala la kila anakiona mwanaume anavutiwa kwa nguvu ya ajabu (hasa anapomuona mwanamke, wakati huohuo mwanamke naye anauwezo na nguvu ya ajabu ya hamu ya upendo, ukaribu, mapenzi na kusikilizwa na mwanaume.

Mwanaume huwaza ni mara ngapi anahitaji sex wakati mwanamke anawaza ni namna gani sex itakuwa
 
lazaro mbilinyi

Wa kufanana naye - Migogoro!

Kukiwa na mgogoro kati ya mume na mke, kawaida mke hujitahidi kufanya bonding na mumewe kwa kuongea (talk, relate) na kuhakikisha emotions zinakuwa wazi kwa kuwa hajui tofauti ya mwanaume huamini na mume wake naye atakuwa mwepesi kuongelea kama yeye na matokeo yake mwanamke huishia kuwa na hasira na frustrated.

Jambo la msingi ni kwamba mume anatakiwa kufahamu kwamba kunapotokea mgogoro au kupishana lugha ni jambo la maana sana kumsikiliza mke au kuhakikisha mnaongea na unampa mke muda na wakati wa kutosha kuongea yote aliyonayo (kutoa emotions zake hata kama atalia machozi ila hakikisha analia akiwa mwilini mwako) na kwa njia hiyo anajiona unamjali kuliko kumwambia tusiongee sasa au tutaongea baadae au kukwepa au ku-ignore maana hapo ataumia zaidi na kuona humjali, hapendwi na upo harsh.
Pia mke naye asikasirike pale anaona mume anakwepa kuongelea tatizo au mgogoro uliopo kwani wanaume ndivyo walivyo (tofauti zilizopo kwani wanaume huamini kwa kuacha kuongelea ndiyo njia nzuri ya kumaliza mgogoro) hivyo wewe mke mpe muda na akitulia (akitoka kwenye cave) mnaweza kuongea zaidi.

When men and women agree, it is only in their conclusions; their reasons are always different.
- George Santayana
 
Uwezo wa kuwasiliana kati ya mke na mume ni moja ya precious commodities muhimu sana katika ndoa au mahusiano yoyote.

Wanandoa wenye uwezo mzuri wa kusiliana huwa na ndoa/mahusiano bora na zaidi huweza kuwa na watoto ambao nao huwa wazuri katika kuwasiliana na hatimaye kuwa candidates wazuri wa ndoa baadae.
Pia kuwa na mawasiliano mazuri husaidia mtu kuwasiliana na watu wengine na kuwa na mvuto zaidi.

Kuna usemi wa kingereza usemao
"Great communicators are people who change their approach based upon the person they are talking to"

Hii ina maana kwamba kama wewe ni mwanaume huwezi ongea the same style kwa mwanaume mwenzako na mwanamke.
Kuongea na mwanamke au mke ni tofauti na mwanaume au mume.
Hivyo kujua au kufahamu jinsi ya kuongea au kuwasiliana na mke wako au mume wako ni jambo la msingi sana ili kuwa na mahusiano mazuri.


Kumbuka mwanaume na mwanamke wapo tofauti sana kwani;
Huwaza na kufikiri tofauti,
Huongea tofauti,
Huamua tofauti na zaidi
linapokuja suala la hisia kuna tofauti kubwa sana.


Inawezekana wewe ukiwa na mume wako au mke wako huwa mnajikuta ni bubu, au ni kubishana tu au kila mmoja hamwelewi mwenzake au mwenzako akiongea unahisi haeleweki kwani anazunguka wakati anatakiwa kuwa direct to the point.


Unataka kujua kwa nini?
 
Back
Top Bottom