Wa Kijijini usiende mjini kwa nduguyo bila sababu yenye faida, mnatesa watu

MC Chere

JF-Expert Member
Jun 29, 2015
586
400
"Ebwana hapa nilipo nina ndugu kibao wamejazana hapa, na siwezi kuwafukuza, yaani walipiga simu eti anko tunakuja kukusalimia, hata kuwazuia siwezi, sasa ninajaribu kuwaelekeza namna maisha ya mjini yanavyotaka kujichanganya changanya ili mkono uende kinywani, lakini inaonekana somo lipo mbali na sasa maisha yanakaba mpaka naona kero kwa uwepo wao. Na tena bwana nitaomba kama ukiipata hiyo mashine naomba uwaajiri hawa vijana, nitawashawishi hata wawili waje na kuwapa elimu zaidi ya kufanya kazi".

Hayo ni maongezi niliyoyanasa kutoka kwa bwana mmoja aliyepo Dar akimwelekeza rafiki yake wa Iringa kwa simu wakati huo tupo internate cafe.

Jamani, Watanzania wenzangu mliopo vijijini, msidhani kuwa waliopo mjini mambo yao ni poa, ni ujanjaujanja tu jamani, sasa unapofunga safari kwenda kwa mtu just kumsalimia tu, kwanza amekuomba umsalimie!? Pili unasalimia hadi miezi mitatu?

UJINGA HUZAA UMASKINI, TUBADILIKE JAMANI.

Tujali kutumia muda kujiingizia pesa.

By MC Chere kipenzi cha Lara 1.
 
Mhh,acha waje we mwenyewe umempata Lara 1 ukiwa mjini.

Nyie si ndio wale mkienda Kijijini masifa teleeeee

Sasa wao wamekuja ku practice,wakimaliza watarudi.Field yao ni miaka minne tu wala si mingi.Vumilia mkuu

Nina experience ya kotekote,bush na town,eti wapo field ya miaka minne hahahahahaha! mbavu zangu kwisha,ngoja tumsubiri Lara 1.
 
Wakifika kijjn watasema uliwatesa. Binadamu hasa ndugu jamani wengine sio wema.
 
Mhh,acha waje we mwenyewe umempata Lara 1 ukiwa mjini.

Nyie si ndio wale mkienda Kijijini masifa teleeeee

Sasa wao wamekuja ku practice,wakimaliza watarudi.Field yao ni miaka minne tu wala si mingi.Vumilia mkuu

Teh!teh!,teh!,mkuu umenikumbusha nikiwa mdogo nilikuwa ninajua kuwa kila anayesema anaishi mjini ana maisha mazuri,Maana walikuwa wakirudi kijijini ilikuwa ni full kijiona na masifa kibao.Baadaye nikaja kugundua kuwa wale jamaa sivyo nilivyowadhania na hii ni baada ya kuwatembelea baadhi yao.
 
Ndiyo maana ukienda ubalozini kwenda kuomba visa ya Marekani unapigwa maswali ukibwabwaja wanakutimua wanajua wew ni mzamiaji!
 
Teh!teh!,teh!,mkuu umenikumbusha nikiwa mdogo nilikuwa ninajua kuwa kila anayesema anaishi mjini ana maisha mazuri,Maana walikuwa wakirudi kijijini ilikuwa ni full kijiona na masifa kibao.Baadaye nikaja kugundua kuwa wale jamaa sivyo nilivyowadhania na hii ni baada ya kuwatembelea baadhi yao.

Cha msingi town nenda kwa nduguyo kwa mipango kama akutafutie kaajira hapo sipingi coz na ww utajitegemea,ila kusalimia mpaka miezi 4 sio ishu na humnasi Lara 1 kibwegebwege hivyo,ana level zake yule.
 
Cha msingi town nenda kwa nduguyo kwa mipango kama akutafutie kaajira hapo sipingi coz na ww utajitegemea,ila kusalimia mpaka miezi 4 sio ishu na humnasi Lara 1 kibwegebwege hivyo,ana level zake yule.

Ukimkaribisha mtu kuna uwezekano akatembea na mkeo au bintiyo, kwanini kuleta balaa nyumbani ?
 
Mimi naishi kijijini,tangu nikiwa mdogo nilikuwa natamani siku moja nikasalimie ndugu mjini!! Maskini siku nilipotembelea kwa baba mdogo Mwanza akifanya kazi shirika la reli (Mwanza South) mlo tu wa siku moja kesho yake nilimuaga kwani bahati nzuri sikumwambia idadi ya siku nitakazokaa pamoja na furaha yake kubwa kwa kuniona. Alijitahidi kunitembeza ofisini kwake lakini mawazo yangu ni viazi vya kuchoma na maziwa mgando Nyumbani. Tangy siku hiyo nikimtembelea ndugu wa mjini ni siku mbili nikiwa na shuka langu,net ya mbu na nauli. Wengi wa ndugu zangu washanibandika jina la Mzungu mweusi.
 
Back
Top Bottom