W. Malecela na Nape mnaiua CCM, Chama siyo mali yenu

Muke Ya Muzungu

JF-Expert Member
Jun 17, 2009
3,444
264
-Nikiwa Mwana CCM mkongwe, napenda nitoe dukuduku zangu kuhusiana na mienendo ya ndugu zetu Nape Nnauye pamoja na William Malechela ambao dhahiri wanakiangamiza chama siyo kwa kusimamia na kutetea ilani za chama chetu, bali kwa kutangaza propaganda zisizo na mshiko.

-Bwana Malechela amekuwa mshabiki mkubwa wa Mh. Wildroad Slaa kwa muda mrefu. Alifikia hatua ya kumuita Dr. Slaa Rais wake na kumwagia sifa kemkem za kumsifia. Kipindi hicho, bwana malechela alikuwa akimnanga na hata kumtukana Rais Kikwete, leo baada ya maisha kumshinda ulaya, alirudi Tanzania na kuanza kuimwagia CCM misifa, huku akimkashifu rais wake na watenda kazi wa Chadema.

-Nape kwa upande wake, pia amekuwa mshabiki mkubwa wa vyama vya upinzania. Tunaweza kumuita Muasi ndani ya CCM alipewa wadhifa kutokana na fadhila Fulani. Kwani baba yake nape. Mzee Nnauye alikuwa kada mkubwa wa CCM. Nape ni mwanzilishi wa CCJ na ushahidi zaidi tunao na tutazianika muda muhafaka.

-Kiongozi nikioo cha jamii. Kwa sasa hawa jamaa wawili haenezi sera za CCM, bali wanapanda chuki kejeli na ujinga. Mambo wanayoandika ni mambo ambayo yanazidi kuichafua chama chetu kikongwe. Mtaani, kijana wa malechela ndio gumzo. William anajulikana kama mzee wa mabinti. Jamanii inasaidia au inabomoa chama chetu? Nchi nyingine msingepata nyadhifa kwenye serikali kwani you do not have the necessary charactes to be leaders.

-Lakini kwa vile mmerithishwa madaraka, mnaiona nchi kama yenu. Tafadhali mbadilike kwani mmefika kukosa adabu hata kwa baba zenu. Mnamtukana Dr. Slaa ambaye ni sawa na baba yenu. Tafuteni Adabu ilipo. Kama hamuwezi kujibu hoja za wapinzani wenu, basi hamfai kuwa wanasiasa, kwani viroja vyenu na mipasho inazidi kuibomoa chama chetu
 
Ni dhahiri hao wawili wana njaa kali.
Unakosea kuwashauri wenye njaa kali wasile ubwabwa licha ya kushauriwa ubwabwa umetiwa sumu.
Waache wale washibe.
 
Wote vigeugeu na waropokaji isipokuwa malecela tapeli
 
Wote wamerithi,sisi tutawekwa wapi wakti wazazi wetu ni wakulima? LE MUTUZ na umri alonao mpaka leo ni mtoto wa mama.
 
Nape Mtoto wa baba mariam na mwalimu wa ukakamavu miaka ya mwanzo ya uhuru - hana jipya. Hata hapa atatukana. Aliowaajiri kujibu hoja nao wameingia mitini!
 
Afadhari hata ya NAPE akibanwa sana huwa anaweza akaelewa somo. Lakini huyu malecela ni kama alishawahi kuvuta bangi vile. Ni mkurupukaji na mropokaji aliyepitiliza. Huwa hata najiuliza alitoa wapi gut ya kugombea ubunge wa Africa mashariki.

Ukiangalia uwezo wa hawa ndugu wawili katika kujenga hoja, unagundua kwamba kinachowafanya wavume kwenye siasa za Tanzania hivi sasa, si uwezo wao wa kisiasa bali ni majina ya wazazi wao.
 
Nape na Wiliam ni kopo na kifuniko chake. Ccm ni jalala la mbagala, kila aina ya uozo hupatikana hapo! Vijana kwa umri, lakini akili zao zimechoka kuliko za kingunge.
 
mmh ni mara mia afadhali Nape bado ana utu kwa mbaaaali kuliko Le Mutuz, huyu kashapinda mpaka kanyongoroka na umri nao umemtupa mkono.He is irreversible...
 
Mtoa mada umenena. Yaani ukisoma wanayoandika yanaonyesha hawana kitu vichwani. Mambumbumbu eti viongozi watetezi wa chama. Ccm ya mazoea yaani mzazi alikuwa na cheo hivyi lazima mwanae aridhishwe. Si mnakumbuka Arumeru Mashariki? Kwa kuwa tunatawaliwa na ujinga, basi ndiyo hivyo tena. Ni mpaka ccm ifukiwe udongo mwingi tu ndipo wenye chama chao watakapoju sii kila kiongozi anazaa na kulea kiongozi wa kumrithi. Nape na William wamedhihirisha hilo. Waambie wafiche kupe zao Dr. Slaa ni baba yao na watanzania wenye akili timamu wanamheshimu kwani wanajua anachokifanya. Mbona hatumsikii hata JK mwenyewe akimbeza sembuse hawa wajinga?
 
Duh....inaonekana hawa jamaa wamekua hatari mpaka watu wanaanzisha thread kuwataka waache mashambulizi.
Oyaah..hebu ongezeni kidogo speed nataka nione wangapi wanaondoka kwa pressure .
 
Zionist Ama kweli CDM mmeishiwa propagander hadi mnacopy na kupesti
 
Last edited by a moderator:
Le Mutus aka King of all media network in Tanzania pamoja na Nnape Jnr kumbe ni mwiba kwa Chadema?, safi sana.

Waswahili walisema mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu, na pia ni kweli kwamba nyani haoni kundule.

Kabla ya kuanza kuwatupia madongo hawa vijana wawili ni hekima pia kujiangalia upande wenu, je mnajibu hoja kwa hoja?.
 
-Nikiwa Mwana CCM mkongwe, napenda nitoe dukuduku zangu kuhusiana na mienendo ya ndugu zetu Nape Nnauye pamoja na William Malechela ambao dhahiri wanakiangamiza chama siyo kwa kusimamia na kutetea ilani za chama chetu, bali kwa kutangaza propaganda zisizo na mshiko.

-Bwana Malechela amekuwa mshabiki mkubwa wa Mh. Wildroad Slaa kwa muda mrefu. Alifikia hatua ya kumuita Dr. Slaa Rais wake na kumwagia sifa kemkem za kumsifia. Kipindi hicho, bwana malechela alikuwa akimnanga na hata kumtukana Rais Kikwete, leo baada ya maisha kumshinda ulaya, alirudi Tanzania na kuanza kuimwagia CCM misifa, huku akimkashifu rais wake na watenda kazi wa Chadema.

-Nape kwa upande wake, pia amekuwa mshabiki mkubwa wa vyama vya upinzania. Tunaweza kumuita Muasi ndani ya CCM alipewa wadhifa kutokana na fadhila Fulani. Kwani baba yake nape. Mzee Nnauye alikuwa kada mkubwa wa CCM. Nape ni mwanzilishi wa CCJ na ushahidi zaidi tunao na tutazianika muda muhafaka.

-Kiongozi nikioo cha jamii. Kwa sasa hawa jamaa wawili haenezi sera za CCM, bali wanapanda chuki kejeli na ujinga. Mambo wanayoandika ni mambo ambayo yanazidi kuichafua chama chetu kikongwe. Mtaani, kijana wa malechela ndio gumzo. William anajulikana kama mzee wa mabinti. Jamanii inasaidia au inabomoa chama chetu? Nchi nyingine msingepata nyadhifa kwenye serikali kwani you do not have the necessary charactes to be leaders.

-Lakini kwa vile mmerithishwa madaraka, mnaiona nchi kama yenu. Tafadhali mbadilike kwani mmefika kukosa adabu hata kwa baba zenu. Mnamtukana Dr. Slaa ambaye ni sawa na baba yenu. Tafuteni Adabu ilipo. Kama hamuwezi kujibu hoja za wapinzani wenu, basi hamfai kuwa wanasiasa, kwani viroja vyenu na mipasho inazidi kuibomoa chama chetu

- Le Mutuz huwa ni mtu wa kusema ukweli na huwa hachagui Kiongozi wa kumpa ukweli, Kuna wakati Slaa alikuwa na hoja nzito za kulisaidia Taifa, yes alikuwa anamuunga mkono kwa hoja lakini sio kwa Slaa as Slaa, Majuzi tu hapa tumeona Le Mutuz akimchana Mukama, na mpaka magazeti ya bongo Kuibeba ile habari toka na kuiweka kila mahali na leo Mukama sio KAtibu tena wa CCM meaning kwamba CCM wana Tabia za kusikiliza wakiambiwa ukweli, sawa sawa na hata kwa Rais wa Jamhuri Le Mutuz hajawahi kum-spare hasa huko nyuma, matokeo leo Rais amefanya mabadiliko mengi sana ambayo yanatia moyo na infact mpaka leo ameifunika Chadema imekuwa kama imekufa, Le Mutuz hawezi kumsifia Slaa kwa kuwa na kadi ya CCM huku anailipia kila mwezi, wakati ni Kiongozi wa Chadema, hilo knowing as I do hawezi na ndilo hasa linalokuuma mleta Mada, ni kwamba wewe ni Chadema sasa the idea kwamba Slaa Rais wako ana kadi ya CCM na anilipia kila mwezi limekushangaza sana na kwa sababu Slaa ndiye tegemeo lako kushika power bongo, huamini kwamba unaweza kumrekebisha Slaa, sisi CCM tunarekebishana sana na tunaambiana ukweli all the times!, Mnasema maneno mengi sana kuhusu LE Mutuz lakini ukweli ni kwamba he seems to be bigger than you all in this game of social media kwa sababu badala ya kujibu hoja kwa nini Slaa ana kadi ya CCM na anailipia kila mwezi, badala yake mnatafuta uchawi wa kumsingizia Le Mutuz, inashangaza sana kwa Great Thinkers ambao wengi wenu mmeaamua kwamba ni Chadema wa damu, hoja ndogo tu hizi zinawatisha mnakosa hata utu wala uvumilivu? Sasa mkipewa nchi itakuwaje?

- Mh. Nape, na yeye pia siku zote hajawahi kujikomba kwa mtu alipokuwa anapigana na mafisadi haikuwa kwa sababu anawaunga mkono Chadema, naona nyinyi kiongozi yoyote wa CCM akipigana na uozo ndani ya CCM mnadhani anawaunga mkono, no ni mawazo potofu sana na ndio maana sasa CCM imekaa vizuri na kuwa na umoja wa ajabu sasa mnhangaika kila mahali hamjui la kufanya, Nape ni Kiongozi wa Taifa wa CCM so is Le Mutuz, sasa naona mnakwazika kwa sababu ambazo hazina hata msingi, teteeni hoja au sera za chama chenu lakini sio kutafutana na personal kama mleta mada unavyofanya, ni dalili za ukoseavu wa ukomavu wa kisiasa, Nape amekuwa mwiba sana kwenu kwa sababu mlizoea siasa za kutukana bila kujibiwa sasa mnajibiwa tena kwa lugha mnayoijua vizuri mnaanza kulia lia kama watoto wadogo, tulizeni boli, CCM haitakuwa kama zamani tena, sasa ni hoja kwa hoja na viroja kwa viroja!!

- Again, mtoa mada umeonyesha uoga wako kwamba unawaogopa hao wawili, kama nilivyoema juzi tupo kwenye vita vy akitikadi sasa kama huwezi kutetea chama chako kaaa pembeni waachie wengine lakini usilete kulia lia hapa hakuna wa kukusaidia, wembe ni ule ule na sisi wengine tunaounga mkono CCM tutaendelea kama kawaida CCM ikikosea tutaichana na Chadema ikikosea tunaichana hakuna msamaha hapa,

- now again Slaa as Kiongozi wa Chadema kuwa na kadi ya CCM na kulipia kila mwezi ni makosa makubwa sana amepoteza moral authority ya kuongoza, sasa uamuzi ni wenu kuendelea kumtetea au kumwambia ukweli airudishe, sisi hatutaki ajiuzulu hapana maaan hakutakuwa na mwingine huko wa kuwaongozeni we know that, na sisi tunataka chanagamoto za kutusaidia CCM, maana sometimes huwa ana hoja nzuri kwetu CCM, lakini kwa hili la kuwa na kadi ya CCM amechesha big time, dawa ni kuirudisha kadi ya CCM now kabla it is too late!!

- KIDUMU CCM!

eS!
 
Inatisha sana kwa kiongozi mkubwa wa chama kuwa na kadi hai ya chama cha upinzani. Chadema hili suala si la kulichekeachekea hata kidogo. Hapa ni sawa na Waziri mkuu wa Israeli kuwa member hai wa HAMAS.

Haiwezekani na wala haitawezekana kabisa kwa Jakaya kuwa na kadi ya chadema na anailipia kila mwezi then bado anakuwa kiongozi mkubwa wa CCM.

Dr Slaa, this is out of order na unafiki wa hali ya juu. Ni hatari kuliko sumu ya nyoka.
 
WanaCCM bana,
Huyu naye kwa kutoa tuhuma kwa kupitia mitandao huku akidai ni mwanachama wa CCM wa muda mrefu hajui kama anafanya makosa yaleyale katika macho ya katiba kwenye kipengele cha kanuni na taratibu za chama kama zilivyoanishwa katika sehemu ya pili, fungu la 1 (1-6). Kwani hujui kama kuna taratibu ndani ya chama katika kushughulikia malalamiko.

Mambo haya yanajitokeza kwa sababu chama kwa sasa kina viongozi na wanachama wasiojua katiba, kanuni na taratibu za utekelezaji wa majukumu ya chama.

Halafu maelezo yako yamebeba ujumbe kama vile chama ni 'Malechela', Makamba & Nape bila kuangaliai picha kwa upana na urefu huku ukidai chama cha CHADEMA kina Rais wake.btoka lini CHADEMA ikawa na Rais.

Ndiyo, kila binadamu ana upungufu na mengi wanayofanya viongozi wa vyama na serikali sikubaliani nayo lakini kile ulichokileta hapa janvini kinaonekana kama ni majungu na personal attack kwa sababu unazozijua mwenyewe wakati katiba ya chama chako sehemu ya tano, kipengele cha 200 (1-9) inakataza mizengwe kama hii.

Kwa msaada zaidi na kwa faida yako, CCM imeanza kufa pale tu kilipojivika kitanzi cha mabadiliko kule Zanzibar wakati wa awamu ya pili ya uongozi wa chama na serikali na siyo kwa ujio au shughuli za hawa watu uliowataja kama unaopenda ijulikane hivyo.

CCM kwa sasa imebakiwa na nyumba isiyokuwa na msingi imara ambao hauwezi kuhimili upepo wa mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi na kujamii mpaka hapo itakapoirudia falsafa yake kuu.

Hivi unafahamu kama katiba ya chama chako sehemu ya kwanza, kipengele cha 4(3) bado kinasema Ujamaa na Kujitegemea ndiyo njia pekee ya kujenga jamii ya watu walio sawa na huru wakati kinachofanyika ni kinyume cha hivyo.

Ama kweli kwa sasa vyama vya siasa vina wanachama.
 
- Le Mutuz huwa ni mtu wa kusema ukweli na huwa hachagui Kiongozi wa kumpa ukweli, Kuna wakati Slaa alikuwa na hoja nzito za kulisaidia Taifa, yes alikuwa anamuunga mkono kwa hoja lakini sio kwa Slaa as Slaa, Majuzi tu hapa tumeona Le Mutuz akimchana Mukama, na mpaka magazeti ya bongo Kuibeba ile habari toka na kuiweka kila mahali na leo Mukama sio KAtibu tena wa CCM meaning kwamba CCM wana Tabia za kusikiliza wakiambiwa ukweli, sawa sawa na hata kwa Rais wa Jamhuri Le Mutuz hajawahi kum-spare hasa huko nyuma, matokeo leo Rais amefanya mabadiliko mengi sana ambayo yanatia moyo na infact mpaka leo ameifunika Chadema imekuwa kama imekufa, Le Mutuz hawezi kumsifia Slaa kwa kuwa na kadi ya CCM huku anailipia kila mwezi, wakati ni Kiongozi wa Chadema, hilo knowing as I do hawezi na ndilo hasa linalokuuma mleta Mada, ni kwamba wewe ni Chadema sasa the idea kwamba Slaa Rais wako ana kadi ya CCM na anilipia kila mwezi limekushangaza sana na kwa sababu Slaa ndiye tegemeo lako kushika power bongo, huamini kwamba unaweza kumrekebisha Slaa, sisi CCM tunarekebishana sana na tunaambiana ukweli all the times!, Mnasema maneno mengi sana kuhusu LE Mutuz lakini ukweli ni kwamba he seems to be bigger than you all in this game of social media kwa sababu badala ya kujibu hoja kwa nini Slaa ana kadi ya CCM na anailipia kila mwezi, badala yake mnatafuta uchawi wa kumsingizia Le Mutuz, inashangaza sana kwa Great Thinkers ambao wengi wenu mmeaamua kwamba ni Chadema wa damu, hoja ndogo tu hizi zinawatisha mnakosa hata utu wala uvumilivu? Sasa mkipewa nchi itakuwaje?

- Mh. Nape, na yeye pia siku zote hajawahi kujikomba kwa mtu alipokuwa anapigana na mafisadi haikuwa kwa sababu anawaunga mkono Chadema, naona nyinyi kiongozi yoyote wa CCM akipigana na uozo ndani ya CCM mnadhani anawaunga mkono, no ni mawazo potofu sana na ndio maana sasa CCM imekaa vizuri na kuwa na umoja wa ajabu sasa mnhangaika kila mahali hamjui la kufanya, Nape ni Kiongozi wa Taifa wa CCM so is Le Mutuz, sasa naona mnakwazika kwa sababu ambazo hazina hata msingi, teteeni hoja au sera za chama chenu lakini sio kutafutana na personal kama mleta mada unavyofanya, ni dalili za ukoseavu wa ukomavu wa kisiasa, Nape amekuwa mwiba sana kwenu kwa sababu mlizoea siasa za kutukana bila kujibiwa sasa mnajibiwa tena kwa lugha mnayoijua vizuri mnaanza kulia lia kama watoto wadogo, tulizeni boli, CCM haitakuwa kama zamani tena, sasa ni hoja kwa hoja na viroja kwa viroja!!

- Again, mtoa mada umeonyesha uoga wako kwamba unawaogopa hao wawili, kama nilivyoema juzi tupo kwenye vita vy akitikadi sasa kama huwezi kutetea chama chako kaaa pembeni waachie wengine lakini usilete kulia lia hapa hakuna wa kukusaidia, wembe ni ule ule na sisi wengine tunaounga mkono CCM tutaendelea kama kawaida CCM ikikosea tutaichana na Chadema ikikosea tunaichana hakuna msamaha hapa,

- now again Slaa as Kiongozi wa Chadema kuwa na kadi ya CCM na kulipia kila mwezi ni makosa makubwa sana amepoteza moral authority ya kuongoza, sasa uamuzi ni wenu kuendelea kumtetea au kumwambia ukweli airudishe, sisi hatutaki ajiuzulu hapana maaan hakutakuwa na mwingine huko wa kuwaongozeni we know that, na sisi tunataka chanagamoto za kutusaidia CCM, maana sometimes huwa ana hoja nzuri kwetu CCM, lakini kwa hili la kuwa na kadi ya CCM amechesha big time, dawa ni kuirudisha kadi ya CCM now kabla it is too late!!

- KIDUMU CCM!

eS!

wee jamaa kichwa maji kweli.. kwaio unakubali kuwa ccm imeoza ndio maana Nape alipambana nao?? kichwa maji aisee. Nani kakwambia kuwa kitu kikioza kinaweza kurudia kuwa fresh?? ubaya wa pro-ccm ni vichwa maji kwaio cdm wamepata pa kutokea
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom