Vyuo vya Tanzania vyafanya vibaya kwenye Takwimu za kimataifa

Wale cjui udom mara st Augustne hv hawapo coz wanadai vyuo hivyo ni nondo sana. TUPE UKWEL MKUU SIAMIN KM HAWAPO HATA TOP TEN KWA WANAVYOIPONDA UDSM
 
Wale cjui udom mara st Augustne hv hawapo coz wanadai vyuo hivyo ni nondo sana. TUPE UKWEL MKUU SIAMIN KM HAWAPO HATA TOP TEN KWA WANAVYOIPONDA UDSM
Karibu ranks zote za kimataifa mara nyingi ni hivyo vyuo viwili nilivyotaja hapo ndo huonekana kwa hapa TZ
 
Professor Tanzania anasema huwezi kuchukua degree kupitia diploma yako kama huna cheti cha form six, unatakiwa urudie kwanza form 5 na six ndo uweze kuchukua diploma. Upandishaji wa Elimu Tanzania kupitia njia ya kuzeesha watu madarasani :D
 
Ni kweli vyuo vyetu haviwezi kuonekana kwenye rank za kimataifa kwani wafundishaji yaani maprofesa wameteuliwa kushika nafasi za kisiasa badala ya kuachwa vyuoni kufundisha.
Sababu nyingine ni aina ya ufundishaji pamoja na tafiti zinazofanyika kutokutumika zaidi ya kutupwa store au kuchomwa.
Mtu unafanya research kwa mwaka mmoja na unapewa alama nzuri tu, matokeo yake haitumiki hata maktaba ya chuo tu!
Sababu ya mwisho ni muda wa kustaafu maprofesa kuwa sawa na wafanyakazi wa kada nyinginezo. Hili halijakaa vyema kwani japo wamechoka kimwili, bongo zao bado zipo sawa. Nchi kama Japan, Finland na hata Germany process hastaafu na huendelea na kazi kufundisha na kutafiti hadi umauti wao. Kwetu hatujui na au hatuwathamini na kuwaona kama kitu adimu.
Tumefika hapa kwasababu ya siasa zisizo na tija kwenye Elimu yetu na wakati mwingine kuwapuuza walimu wetu.
Hebu siasa ijitenge na mambo ya kitaaluma na maprofesa wasiruhusiwe kustaafu.

Mimi siyo profesa bali najaribu kuuona umuhimu wao na jinsi tunavyowatreat.
 
Kwani kujua ubora wa vyuo mpaka Takwimu za hao angalia tu matamko tu yanayotoka katika watendaji waliotoka katika hivyo vyuo utajua kama Ubora upo au laa...ni bora ukwa na Postgraduate ya UNISA kuliko Phd za Bongo ni magumashi tuu..
 
Hapana kwa kweli llazima tujiangalie hiwezekani Makerere wawe na uwezo wa kutengeneza gari inayotumia umeme wa jua project ambayo imewapaisha sana halafu sisi turidhike yaaani.

Hahaha embu tutoke kwenye ndoto za mchana gari ya umeme Africa la kazi gani labda.... Woiii tunamatatizo makubwa zaidi ya kushughulikia gari lifikiriwe ukiwepo umeme wa uhakika, prototype zipo sio kwamba ni kitu cha kugundua tufanyie kazi matatizo yetu kwanza, kuna mifumo mingi inagunduliwa kwenye kilimo, uzalishaji wa umeme, nadhani tupambane naizo kwanza japo hazina kick kuliko gari la umeme ambalo limeishia kuwa chombo cha maonyesho.
 
Tuangalie taarifa kama hizi zinatolewa na nani na kwa sababu gani. Viko vyuo kila leo migomo na product zao tunafanya nazo kazi. Hamna chochote. Tanzania wahitimu wake wanang'ara dunia nzima.
Naona humu watu ambao hata shule zao zinatia shaka wanacomment kuhusu elimu ya chuo kikuu.
Sisi tunaotembelea vyuo vya ndani na nje tunajua uwezo wa vyuo vyetu na tunawaambia tupo juu.

penye ukweli tukubali tu...changamoto ni nyingi mno vyuoni mwetu...Lakini tukijifunga kibwebwe tutafika tu!
 
Back
Top Bottom