M-pesa
JF-Expert Member
- Sep 4, 2011
- 602
- 151
Wadau nimesha deal na vyuo vikuu vifuatavyo;
University of Dar Es Salaam, Open university, Istitute of Finance Management (IFM) na Mzumbe University. Nilichokumbana nacho si mfano bora, na hasa ukizingatia hawa ndo wanao waandaa vijana wetu kuingia kwenye soko la ajira.
Kwa kifupi sana nimeshuhudia mambo yafuatayo:
University of Dar Es Salaam, Open university, Istitute of Finance Management (IFM) na Mzumbe University. Nilichokumbana nacho si mfano bora, na hasa ukizingatia hawa ndo wanao waandaa vijana wetu kuingia kwenye soko la ajira.
Kwa kifupi sana nimeshuhudia mambo yafuatayo:
- Sehemu ya maulizo (enquiries) wameweka watu wasio na uzoefu au wamezoea kazi, hii hupelekea wakujibu watakavyo au kutoa taarifa zisizo sahihi. Hili nimelishuhudia Mzumbe na IFM.
- Vyuo vyote havijibu emails; sasa najiuliza kwanini wameziweka kwenye website zao au kwenye business cards zao?
- Teknolojia ni mbovu ajabu; nimekwenda UDSM nimekuta bado kuna idara zinatumia typwriters za miaka ilee, filing system ndo usiulize.....shida hapa naona hakuna mahusiano mazuri ya departments ndani ya chuo.
- Wahadhiri ndo usiseme wameshajikatia tamaa; they are not happy anymore, hata mazungumzo yao si ya kukutia nguvu ujiunge na vyuo vya Tanzania. Kwa kifupi wanasogeza siku ziende huku wakijikita zaidi kwenye shughuli binafsi.
- Tel. +255 (0)22-2668820, +255 (0)22-2668835, +255 (0)22-2668445, +255 (0)22-2668960, +255 (0)22-2668992